jlogo

Karibuni Jamvini Wanajamii

topads

Post Top Ad

demo-image

SERIKALI YAAHIDI KUBORESHA MIUNDOMBINU KING LION

Share This

 Prof.Mkumbo katikati akisikiliza maelekezo  kutoka kwa Meneja wa King Lion Arnold Lyimo.WhatsApp%20Image%202025-03-27%20at%2010.12.03%20PM


WhatsApp%20Image%202025-03-27%20at%2010.12.04%20PM

WhatsApp%20Image%202025-03-27%20at%2010.12.21%20PM
Waziri Mkumbo  akiwa kwenye picha ya pamoja na wawekezaji wa Kampuni ya GFA Assemble

Na Khadija Kalili Michuzi TV 

WAZIRI  wa  Nchi ,Ofisi ya Rais Mipango Na Uwekezaji   Prof. Kitila  Alexander Mkumbo ametoa ahadi  kwa uongozi wa Kiwanda cha King Lion  kuwa Serikali  itajenga miundombinu  rafiki kwa wawekezaji hasa  ujenzi wa barabara, kuhakikisha umeme wa uhakika na kuwaunganisha na bomba la gesi .

Waziri Mkumbo amesema hayo  tarehe 26 alipotembelea Kiwanda cha King Lion na kuona namna wanavyozalisha bidhaa zao.

"Wawekezaji hawa wamewekeza kiasi cha   Bil.150 (Dola za Kimarekani Bil.90) ambapo wanatengeneza mabati meupe na  ya mgongo.

"Jambo la kujivunia kuona  hivi sasa mabati haya ambayo zamani tulikua tunayaita Msouth yanazalishwa nchini na hiki ndiyo  Kiwanda kikubwa barani Afrika na tayari wanauza mabati yao nchi za Rwanda, Burundi,Jamhuri  ya Kidemokrasia ya Congo (DRC)   na nchi zingine mbalimbali " amesema Mkumbo.

Mkumbo amesema kuwa anawapongeza King Lion kwa kuzalisha ajira 2,000 huku ajira 800 za moja kwa moja na  1,200 siyo za moja kwa moja.

 Aidha Prof. Mkumbo  amesema kuwa Serikali  inajivunia  matunda ya mafunzo ya VETA kutokana na wafanyakazi wengi wa viwandani wamepata mafunzo VETA.

Meneja wa Kiwanda cha King Lion  Arnold Lyimo amesema kuwa wanamshkuru Waziri Kitila kwa kufika  Kiwandani hapo na kuahidi kutatua changamoto zao  kubwa  ambazo ni umeme, barabara mbovu  pia umuhimu wa kuunganishwa  na bomba la asili.

Wakati huohuo Waziri Mkumbo ametembelea Kiwanda cha Kuunga magari kilichopo TAMCO Kibaha na kushuhudia  namna magari  hayo yanavyoungwa nankuingia sokoni.

Prof.Mkumbo amewapongeza  Kampuni ya GFA Assemble  na kuwataka  waongeze7 uungaji wa GFA   magari mengi zaidi.

 "Nimeelezwa kuwa GFA walianza kwa kuunga magari 100 na hivi sasa wameongeza idadi ya magari wanaunga magari 3,000" amesema.Prof Mkumbo.
Comment Using!!

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad