JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


MAKALA YA SHERIA: NINI UFANYE KISHERIA UNAPOHISI MWENZAKO KATIKA NDOA ANATAKA KUUZA NYUMBA/KIWANJA BILA RIDHAA YAKO.

Share This

Upo wakati kwenye ndoa ambapo mmoja wanandoa anaweza akawa anataka kuuza au kubadili jina la nyumba/kiwanja bila ridhaa ya mwenzake ilihali nyumba hiyo ni ya familia. Lakini pia nje ya hilo kuna mazingira ambayo mtu anaweza kuwa si mwanandoa lakini ana maslahi katika nyumba au kiwanja cha mtu fulani na anataka kuzuia nyumba/ kiwanja hicho kisibadilishwe jina au kisiuzwe. Kisheria jambo hilo linaruhusiwa na huitwa zuio( Caveat).

Hili sio zuio la kwenda mahakamani kama mazuio tuliyoyazoea.Hili ni zuio jingine kama nitakavyolieleza. Aidha kuzuia hati isibadilishwe kimsingi ni sawa na kuzuia nyumba isiuzwe. Hii ni kwakuwa hakuna namna ambavyo mnunuzi anaweza kununua kitu ambacho hakiwezi kubadilika na kuingia katika jina lake. Ikiwa mke ana wasiwasi kuwa mume anaweza kumzunguka na kuuza mali ya familia au mume ana wasi wasi juu ya uwezekano wa mke kuuza basi wanayo ruhusa ya kuweka zuio ili hati ya nyumba isibadilishwe. Yapo mambo mengi kuhusu hili nitaeleza baadhi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad