Upo wakati kwenye ndoa ambapo mmoja wanandoa anaweza akawa
anataka kuuza au kubadili jina la nyumba/kiwanja bila ridhaa ya
mwenzake ilihali nyumba hiyo ni ya familia. Lakini pia nje ya hilo
kuna mazingira ambayo mtu anaweza kuwa si mwanandoa lakini
ana maslahi katika nyumba au kiwanja cha mtu fulani na anataka
kuzuia nyumba/ kiwanja hicho kisibadilishwe jina au kisiuzwe.
Kisheria jambo hilo linaruhusiwa na huitwa zuio( Caveat).
Hili sio zuio la kwenda mahakamani kama mazuio tuliyoyazoea.Hili ni
zuio jingine kama nitakavyolieleza. Aidha kuzuia hati isibadilishwe
kimsingi ni sawa na kuzuia nyumba isiuzwe. Hii ni kwakuwa hakuna
namna ambavyo mnunuzi anaweza kununua kitu ambacho hakiwezi
kubadilika na kuingia katika jina lake. Ikiwa mke ana wasiwasi kuwa
mume anaweza kumzunguka na kuuza mali ya familia au mume ana
wasi wasi juu ya uwezekano wa mke kuuza basi wanayo ruhusa ya
kuweka zuio ili hati ya nyumba isibadilishwe. Yapo mambo mengi
kuhusu hili nitaeleza baadhi.



No comments:
Post a Comment