JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


NAIBU WAZIRI MKUU, DK BITEKO KUFUNGUA MAONESHO WIKI YA NISHATI JADIDIFU DAR ES SALAAM

Share This



Jumuiya ya Wadau wa Nishati Jadidifu Tanzania (TAREA), kwa kushirikiana na Wizara ya Nishati kwa udhamani mkuu wa SUN KING, inawaalika Wananchi wote katika Maonesho ya Kitaifa ya Nishati Jadidifu (Renewable Energy)  yatakayofunguliwa Alhamisi Juni 6 na Naibu Waziri Mkuu na Waziri Nishati, Dk Doto Biteko na kufungwa na Waziri wa Kilimo, Husein Bashe Ijumaa, Juni 7, mwaka huu. 

Kaulimbiu ya Mwaka huu ni: NISHATI JADIDIFU KWA UCHUMI SHIRIKISHI NA WA KIJANI (RENEWABLE ENERGY FOR INCLUSIVE AND GREEN ECONOMY)

Wiki ya Nishati Jadidifu itakuwa na maonesho yanayohusisha Umeme wa Jua yaani Sola, Upepo, Joto-ardhi na majiko banifu sambamba na warsha yenye mada mbalimbali kuhusu nishati jadidifu. 

Wadau wa maendeleo, kampuni na taasisi binafsi na serikari watakuwa katika mabanda kutoa elimu na kuuza bidhaa mbalimbali za nishati jadidifu kutoka kwa wataalamu waliobebea.

Wadhamini wengine wa Maonesho hayo yatakayofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere Posta, Dar es Salaam ni Jumuiya ya Umoja wa Ulaya (EU), Expertise France, Ensol, GOGLA, Tanesco, Wakala wa Nishati Vijijini (REA), AECF na UNDP

HAKUNA KIINGILIO.

WOTE MNAKARIBISHWA.

Kwa taarifa zaidi piga 0765 098 462.


Tanzania Renewable Energy Association(TAREA)

Plot 1080, Mandela Road, Mabibo External,

Export  Processing Zone Authority

Shopping Arcade 17,

P.O. Box 32643,16106 Dar es Salaam, Tanzania.

Email address: info@tarea-tz.org


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad