MAGARI BEI POA KABISA

Thursday, July 9, 2009

Unahitaji kuuza gari lako au kununua gari kwa bei nafuu hapa nyumbani,kama ndio tembeleahttp://www.magaribeipoa.blogspot.com/kwa wale wanaouza magari yao wanaweza kututumia picha na maelezo ya magari yaKo wakiambatanisha namba zao za simu na sisi tutaweka matangazo yao kwenye blog bila gharama yoyote.
Magaribeipoa Team
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, July 09, 2009 | | Permalink | Maoni 0

libeneke la ki africa reading


BONGODJS INAWELETEA LIBENEKE LA KIAFRIKA READING 18/07/09 KUANZIA SAA 5 USIKU MPAKA 11 ASUBUHI .NI USIKU WA KUKATA NA SHOKA WOTE MNAKARIBISHWA TULE TUNYWE NA TUCHEZE
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, July 09, 2009 | | Permalink | Maoni 0

wahi tiketi yako mapemaaaa.!


STEERS - MILLENIUM TOWERZ.
STEERS - SAMORA AVENUE.

WHITE PAMBA - SINZA MAKABURINI.

TCC CLUB - CHANG'OMBE.

MILE PAMBA - MWENGE.

ENGEN PETROL STATION - MBEZI BEACH.

ZIZZOU FASHIONS - SINZA & VICTORIA.

MINI ARGOS STORE - MSASANI.

FLAMINGO PHARMACY - TABATA

ROBY ONE FASHIONS WEAR - KINONDONI STUDIO.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, July 09, 2009 | | Permalink | Maoni 0

huu ndio ujio mpya wa q-chila kwa sasa



Mwanamziki mwenye sauti zenye kuwafanya watu waache kazi zao pale mziki wake wa Ubongo wenye akili yaani BONGO FLAVA Q Chief a.k.a Q Chilla kichwa chake sasa ni cheupe kama kiganja cha mkono kwa kuwa ameamua sasa rasta basi na kuonyoa nywele zake zote na kubaki na kialaza. Hivi sasa anatamba na kibao chake cha mnanda ambao pia unajulikana kama mchiriku.
Kuonesha upara huo unakwenda sambamba na mabadiliko yake makubwa katika fani ya muziki wa kizazi kipya,amejiunga ndani ya lebo ya studio za Bongo Records ilioko chini ya Prodyuza mahiri kabisa hapa bongo aitwaye P-Funk a.k.a Majani a.k.a Kinywele kimoja.
Sasa hivi bongo Records ina vichwa vipya kabisa,akiwemo Mangwear,Q-Chilla,C-Pwaa na wengine kibao,kama vile haitoshi ameongeza maprodyuza wengine wakali akiwemo Producer Q na Antonio.Baada ya hapo wadau wa muziki wa bongofleva kaeni mkao wa kula Jamvini.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, July 09, 2009 | | Permalink | Maoni 0

alitangaza kustaafu mwaka 2002 na akarudi kwa kishindo mwaka 2004,kwanini ?


Huwezi kuthubutu kuzungumzia muziki wa kizazi kipya au Bongo Flava kama unavyojulikana kote ulimwenguni bila kumzungumzia na kumuhusisha moja kwa moja na muziki huo,Joseph Mbilinyi(pichani) ambaye kisanii tulianza kwa kumjua kama 2 Proud kabla hatujamuita Mr.II na baadaye Sugu.


Sugu sio tu alichangia kuipa Bongo Fleva utambulisho rasmi katika jamii,bali pia ni miongoni mwa wasanii “waasisi” walioamua kwa makusudi kuanza kutumia lugha ya Kiswahili katika kughani(rap) huku wakiwa na ujumbe ambao uligusa jamii inayowazunguka badala ya ile ya kusimuliwa au kuona katika luninga.Ukipenda unaweza kumwita “mwanamapinduzi”.


Hivi karibuni tulipata nafasi ya kufanya naye mahojiano.Katika mahojiano haya Sugu anabainisha mambo kibao yakiwemo masuala kama vile alipo na anachokifanya ,ushauri wake kwa wasanii wenzake katika masuala ya haki zao nk.Pia Sugu anajibu swali ambalo wengi wanaliogopa;je muziki wa bongo fleva uko katika njia sahihi?Kuna tofauti gani katika muziki huu tangu walipoanza na walipo hivi sasa?


Kubwa ya yote ni kwamba Sugu ameamua kuwapa zawadi maalumu mashabiki wake. Anakuja na albamu mpya! Ukisoma mahojiano haya mpaka mwisho utaweza kusikiliza single mpya kutoka kwake inayokwenda kwa jina Kambarage.
Ukitaka kujua zaidi mtu mzima Sugu kaongea sumu gani ingia bongocelebrity.com
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, July 09, 2009 | | Permalink | Maoni 0

mie mjumbe tu wa haya wanajamvini

Mambo vipi kaka?

Hongera sana kwa kazi nzuri sana naomba unitolee hii ili nipate mawazo ya wadau wengine.

Nimesikia sana libeneke la VISACARDS za crdb kuwa unaweza kuzitumia online lakini kuna mdau mmoja anasema ni hatari sana pale unapojaza hizo form ukiweka tu zile no nyuma ya card mtu ana uwezo kwa kudraw visenti vyako vyote,sasa mimi nataka kujua wanadraw vipi na mtu utajuaje kuwa hii ni kampuni halali na hii ni fake?
Na kuna jingine mi linanisikitisha sana khusu hii bank ya CRDB yaani ukidraw pesa tu wanakukata sh 400 sasa kwa mfano kwa mwezi ukidraw pesa labda mara 20 almost elfkumi,
Sasa mi najiuliza hivi hii bank kumbe kila siku mtaji wake unakuwa kumbe kwa kutumia migongo ya sisi walala hoi na hiyo ni savings account,ya mimi mfanyakazi wa kima cha chini je mfanyabiashara au mtu unajenga na pesa yako iko hapo labda kila siku unadraw mara tano yaani kwa mwezi wanaingiza sijui billion ngapi?
Na hapo bado sijajua kuhusu hizo account nyingine naomba jamani mnijulishe na hasa hii account ya Malaika maana wanaitangaza sana.Mimi binafsi narudi bank yangu toka shule NMB ingawa nao network zao sijui za makete.
ASANTE SANA KAKA.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, July 09, 2009 | | Permalink | Maoni 3

pumzika kwa amani michael jackson

Wednesday, July 8, 2009
Kwa wale ambao hawakuweza kushuhudia utoaji wa heshima za mwisho kwa Marehemu Michael Jackson kupitia vyombo mbalimbali vya Luninga ikiwepo TBC1 hivi ndivyo mambo yalivyokuwa kwa ufupi katika ukumbi wa Staples Center jijini Los Angeles Marekani ambapo zaidi ya watu 80.000 walihudhuria utoaji waheshima za mwisho wakiwemo watu maarufu mablimbali katika picha kama unavyoona, ni ndugu wa Marehemu Michael Jackson wakitoaJ eneza la Marehemu mara baada ya kutoa heshima za mwisho kwa marehemu Jackson ,mwanamuziki huyo alifariki juni 25 nchini marekani na kwa mujibu wa vyombo vya habari vya kimataifa anatarajiwa kuzikwa leo mara baada ya mwili wake kuagwa rasmi jana (picha kwa hisani ya mtandao).

Dada wa marehemu marehemu Michael Jackosn, Jannet Jackson akiwa na watoto wa marehemu, kulia Catherine na Paris na ndugu zao wengine.

Ndugu na jamaa wa Marehemu Michael Jackson wakiwa wamekaa wakati wa kutoa heshima za mwisho kwa marehemu Michael Jackson kabla ya mazishi.

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Wednesday, July 08, 2009 | | Permalink | Maoni 1

FREE FREE/BURE KUPARTY KILA JUMAPILI WASHINGTON DC

KAMPUNI MAARUFU YA BURUDANI DMK GLOBAL PROMOTIONS INAWALETEA BURUDANI KILA JUMAPILI KAMA IFUATAVYO **FREE *** KILA JUMAPILI ( EVERY SUNDAY)
KIINGILIO BURE ( FREE ALL NITE NO COVER) VINYWAJI HALF OFF (DRINKS HALF OFF FROM 6PM-11PM
NJOO UPARTY HADI SAA NANE -PARTY UNTIL 2- AM** ***MUZIK NA DJ JOE OF 93.9 WKYS FM PIA DJ MARK- PLAYING-RAGGAE,AFRICANS,BOLINGO,BONGO FLAVOR & ALL SPECIAL REQUESTS
PIA KILA IJUMAA WANAKULETEA -INTERNATIONAL VIP FRIDAYS KWA IJUMAA NI FREE KAMA UPO KWENYE GUEST LIST AU $10 KAMA HAUPO KWENYE LIST-SUNDAY NI FREE ALL NITE. ***GUEST LIST NITUMIE MAJINA-
RSVP@DMKPROMOTIONS.COM AU SIMU # 301-661-6207 PIA VISIT WWW.DMKGLOBALPROMOTIONS.COM/WWW.DMKPRODUCTION.COM/WWW.DICKSONMKAMA.COM
CLUB - OZIO VIP LOUNGE

1813 M STREET,WASHINGTON,DC
CLUB INA FLOOR 4, FLOOR YA NNE NI NONE SMOKING
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Wednesday, July 08, 2009 | | Permalink | Maoni 0

Jamanieee wahusika wa mitandao ya simu za mikononi naweni uso.!

Jamanieee..!! hali ishakuwa si hali tena.! wahusika wa mitandao ya simu matamko yenu bado hayajasikika vyema kwa wakala wenu wa vocha (wauzaji vocha za simu za mikononi),kiwango kilichoongezwa bado kimekuwa kero kubwa kwa watumiaji wake ,baadhi yao wamefikia hata kushikana mashati kutokana na hali hii ambayo inaonekana kama inachukuliwa kimzaha mzaha hivi.!,Serikali nayo inapaswa kuchukua hatua zaidi na kuonesha mfano kuhusiana na hili,vinginevyo kuna uwezakano mkubwa wa kuibuka songombingo ambalo litapelekea kesi zake kutokuisha kwenye vituo vyetu vya usalama wa kiraia kiukweli.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Wednesday, July 08, 2009 | | Permalink | Maoni 0

Radio Voice of America(VOA) kumrusha hewani Ras Makunja


Radio Voice of America idhaa ya kiswahili inayorusha matangazo yake kutoka mjini Washington DC, inawaletea mahojiano maalumu na kiongozi wa The Ngoma Africa band,Ebrahim Makunja aka Ras Makunja "Bw.Kichwa Ngumu",mahojiano hayo yatasikika wakati wowote leo hii jumatano 8-07-2009 kwa wasikilizaji wa Afrika mashariki na kati,Mtangazaji wa radio VOA Bw.



Abdushakur anamuhoji Ras Makunja kuhusu nafasi ya mziki wa dansi katika soko la kimataifa?Pia Misukosuko na mitihani gani? iliyokumbana na bendi hiyo hadi kufikia mafaniko ya kuhurudisha mziki wa dansi kwa kasi kubwa katika imaya ya jamii na washabiki wa ulaya ambako mziki huo wa dansi kwa sasa unatamba! mtangazaji wa VOA Bw.


Abdushakur ambaye pia bingwa wa maswali alimuhoji mengi Ras Makunja kuhusu mziki na nyimbo za ngoma africa ambazo mara nyingi zimekuwa na ujumbe au ushauri muhimu kwa jamii,pia miziki wa dansi kwa nini ?umeelekeza kasi kubwa ulaya?


Ili kusikiliza mahojiano hayo na majibu ya Ras Makunja pia unaweza kusikiliza katika mtandao wa radio VOA http://www.voanews.com/swahili ingia katika mziki kutoka Afrika.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Wednesday, July 08, 2009 | | Permalink | Maoni 2

magomeni nusura ipate maafa makubwa kwa wakazi wake leo

Tuesday, July 7, 2009
Muathirika wa dhahma ya umeme akikimbizwa hospitali na wasamalia wema,tukio hili limetokea leo mchana maeneo ya moroco-magomeni jijini Dar.
Ebwanaaee kuna jamaa alikuwa juu ya hili boti,kufuatia shoti hiyo alirushwa toka juu mpaka chini na baadaye akaokotwa na wasamaria wema na kumkimbiza hospitali,kwani tayari alikuwa keshapoteza fahamu.
Baadhi ya vijana wakijiandikisha majina yao mara bada ya kusaidia kuuzima moto huo kwa ndoo,yote hiyo wakitaka walipwe kwa kazi waliyoifanya.
Palikuwa hapatoshi leo mchana magomeni
Tela lililobeba hilo boti likiwa limesimama huku nyaya za umeme zikiwa zimegusa kabisa bodi la boti hiyo.

Baadhi ya watu mbalimbali wakikimbia hovyo mara baada ya mlipuko kutokea.



Mchana wa leo kuliibuka bonge la sekeseke maeneo ya moroco-magomeni jijini Dar baada ya gari moja kubeba 'boti'ambalo kutokana na ukubwa wake liligusa nyaya za umeme na kusababisha milipuko,na kupelekea watu kukimbia hovyo hovyo,inaelezwa gari hilo pia lilikuwa limebeba mitungi kadhaa ye gesi.
Kutokana na mashuhuda waliokuwa eneo hilo walisema kuwa gari hilo lililokuwa na tela lake lilianza kuwaka moto na kupelekea baadhi ya watu waliokuwa eneo hilo,kuhatarisha maisha yao kwa kuuzima moto huo kwa kutumia maji,lakini kwa bahati nzuri gari ya zimamoto nalo liliwahi eneo la tukio na umeme ukazimwa kwa muda kuhakikisha usalama unakuwepo eneo hilo.

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, July 07, 2009 | | Permalink | Maoni 3

kokotozzz zinauzwa!

Kokotozzzz zinauzwa hizi, ila mtanisamehee bure nimesahau kuulizia bei,hapa ni kituoni mwembeni kama unakwenda Msasani Beach.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, July 07, 2009 | | Permalink | Maoni 0

yote haya na mengineyo yanapatikana zizzou fashions & barbershop

Umecheki mmechisho wamtu mzima Bushoke ulivyotulia
aah steve nae kumbe shabiki wa nanihiiiii,ameng'aa lakini
Mr Blue anang'ara




Steve ametoka chicha ndani ya pozi la nne

Ngwair ametoka pina ile mbaya


mmechisho uliotulia

Kampuni ya ZIZZOU ENTERTAINMENT inayomilikiwa na mjasiliamali mahiri hapa bongo,Athuman Tippo ambaye pia ni mmiliki wa maduka ya mavazi na vipodozi ya Zizzou Fashions &Barbershop,amekuwa mstari wa mbele kuwang'arisha vijana wengi hapa mjini wakiwemo wasanii mbalimbali kupitia mambo ya mavazi.
Msanii yoyote akitaka mambo ya mmechisho ama kutoka chicha jukwaani hata mbele ya watu,hana haja ya kusita wala kujiona amekosa mahala pa kupata viwalo vya kumfanya aonekane nadhifu na jasili, Tinga ndani ya maduka ya ZIZZOU FASHIONS yaliyopo Sinza Afrika Sana na Victoria-Mwenge Kijitonyama,ukitoka tu utajiona mpya kila mahali.
Kwa mawasiliano zaidi cheki contact zake juu ama gonga no +255 0774 770077
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, July 07, 2009 | | Permalink | Maoni 0

ajali michezoni





picha za ajali za kweli michezoni tungependa tushee na wadau wengine,ukitaka kuona nyingine zaidi ingia link hii
http://www.nifahamishe.com/album_preview.aspx?AlbumId=425753

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, July 07, 2009 | | Permalink | Maoni 0

wanaume tmk family waunganisha nguvu za pamoja na tip top conections

Monday, July 6, 2009
" Time ishafika na hali ya hewa inaruhusu kama vipi tujikatae"msanii wa muziki wa kizazi kipya Chege Chigunda kutoka kundi la Wanaume TMK family wakicheki 'vidonda vyao leo mchana na Adam Mchomvu baada ya hali hewa kuwa ya baridi baridi hivi na kamvua kwa mbaali jioni hii.
Meneja Fella,Adam Mchomvu na Mkurugenzi Abdul Bonge wakishoo love leo mchana mjengoni.
Mtangazaji wa Clouds Fm (kati) Adam Mchomvu akiyapongeza makundi haya mawili (Wanaume TMK Family na Tip Top Conections) kwa kuziunganisha nguvu zao za pamoja na kufanya kitu bomba kabisa.pili toka shoto ni Dj wa Clouds Fm Dj Bulla.
Baadhi ya wadau wa muziki wa kizazi kipya alias bongofleva wakiwa wamepozi kwa pamoja leo mchana,Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa kundi la muziki wa kizazi kipya Tip Top Conections Abdul Bonge a.k.a Bonge,Meneja wa kundi la Wanaume TMK Family Said Fella a.k.a Mkubwa Fella,Meneja wa Tip Top Conections Babu Tale pamoja na Dj wa kundi la Tip Top atwaye Kwembe.
Makundi haya yamekutana kwa pamoja kwa minajili ya kutoa albamu yao pamoja, ambapo kwa sasa tayari wamekwisha toa singo yao ya kwanza na kuisambaza kwenye vituo mbalimbali vya leo mchana,singo hiyo inaitwa Chama Kubwa iliyorekodiwa ndani ya studio za Mj Records.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, July 06, 2009 | | Permalink | Maoni 1

Bei ya Vocha za muda wa maongezi za voda hazijapanda


Dar es Salaam July 6, 2009:
Kampuni ya simu za mkononi, Vodacom Tanzania, haijapandisha bei za vocha za muda wa maongezi kwa wateja wa jumla na hivyo bei sokoni haitakiwi kupanda.
Akizungumza Jijini mchana huu, Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano cha Vodacom Tanzania, Mwamvita Makamba alisema kilichotokea ni kwamba Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imebadilisha mfumo wa wa ukusanyaji wa kodi ya ongezeko la thamani (VAT) ambao umesababisha badiliko dogo katika gharama za usambazaji kwa wateja wa jumla.
Alisema mabadiliko hayo ya mfumo wa ukusanyaji wa kodi hayatakiwi kuleta mabadiliko katika bei ya uuzajiwa vocha sokoni.
Mwanvita alitoa ufafanuzi huo kufuatia hatua ya baadhi ya wauzaji wa rejareja wa vocha za muda wa maongezi kupandisha bei ya vocha hizo kwa kati ya shilingi 100 na 200, mathalani vocha ya Sh,1000 inauzwa kwa bei ya shilingi 1200, Sh.2000 inauzwa kwa Sh.2200. Sh.5000, inauzwa kwa Sh.5200 au zaidi.
“Kubadilika kwa mfumo wa ukusanyaji wa kodi ya ongezeko la thamani hakupaswi kubadilisha bei kwa wauzaji wa rejareja, natoa wito kwa wauzaji hao kuacha kupandisha bei ya vocha hizo kwani mabadiliko madogo ya kodi yaliyofanywa hayana madhara kwao,” alisema.
Mwanvita.
Alifafanua kwamba Vodacom hivi sasa inakutakana na wauzaji wa jumla wa vocha ili kuhakikisha kwamba bei za vocha zinabaki na thamani kama zinavyotakiwa sokoni, yaani vocha ya 1,000 inauzwa kwa 1,000 na si vinginevyo.
Baadhi ya wateja wa Vodacom wamekuwa wakilalamika kufuatia kupanda huko kwa bei kwa madai kwamba hakuna tangazo lolote la Vodacom lilowataarifu mabadiliko hayo ya bei na kwamba kupanda huko kunawaumiza.
Vodacom Tanzania ndiyo mtandao unaoongoza hapa Tanzania ukiwa na wateja zaidi ya milioni 6 na ukiwa umesambaa nchini nzima.
Imetolewa na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano
Mwamvita Makamba
Kwa niaba ya Vodacom Tan
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, July 06, 2009 | | Permalink | Maoni 0

Haleluya Collection Volume 5 iko sokoni sasa


Ile albamu ya muziki wa Injili Haleluya Collection Volume 5 imetoka leo na tayari imekwisha sambazwa madukani ikiwa imesheni nyimbo kibao za wanamuziki wa nyimbo hizo za kiroho.
Albamu hiyo ambayo imeandaliwa na kusambazwa na MSAMA PROMOTION,Kwa mahitaji ama manunuzi ya albamu hiyo bofya no +255 22 2669066 au +255 0713 383838 Email:msamapromo@yahoo.com Fax +255 22 2669066
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, July 06, 2009 | | Permalink | Maoni 0

mwanaume kazi eeh!


 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, July 06, 2009 | | Permalink | Maoni 4

Ulishaona Gari yenye matege wewe ??!


Mdau,Bro Willy wa Wil'na Interanational kanitumia picha za gari hii ambayo kiukweli lingekuwe kwenye barabara zetu za kibogo lisingefua dafu au mnasemaje wadau.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, July 06, 2009 | | Permalink | Maoni 1

mwanajamvini adai hata japan Vimwana wapo !


Mwanajamvini kanirushia picha hizi akiwa amepozi na vimwana wa Kijapan.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, July 06, 2009 | | Permalink | Maoni 0

UHURU WEAR IKO MTAANI

Sweatshirt Blue
Uhuru White


Grey Uhuru
T-Shirts za Shujaa na Uhuru Wear chini ya lebo ya DEAN SPACE ENTERTAINMENT sasa ziko available kitaani, pata kiwalo chako sasa
pecial delivery bila malipo Tafadhali wasiliana na:
Dean +255 786 940094 Dar es Salaam na
Has T +255 767 650033 - Zanzibar

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, July 06, 2009 | | Permalink | Maoni 0

TANZANIAN COMMUNITY ITALY YAFUNGUA TAWI ROME


Mara baada ya kikao cha uchaguzi na ufunguzi wa tawi la jumuiya ya Watanzania Italy siku ya jumamosi tarehe 4/7/2009 ROME. kutoka kushoto, Ndugu ANDREW MHELA (KATIBU) MH.BALOZI KARUME, BI ZUHURA A.KIRRO (MWENYEKITI),MAMA BALOZI NA NDUGU AWADH AMBAE ALICHAGULIWA LUWA MUWEKA HAZINA (photo by GEORGE MAYAKA (Rome)
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, July 06, 2009 | | Permalink | Maoni 1

mdau anaomba kujua mastaa hawa wako wapi?

Ebwana kaka mambo vipi?
Naomba unitolee hii ili nisaidiwe kujua hawa mastaa wa zamani wako wapi?George Masatu,Mwameja na waigizaji Mama kibakuli,Lily na kadada kadogodogo kalokuwa kanaigiza na akina kibakuli.
Asante sana kaka
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, July 06, 2009 | | Permalink | Maoni 1

XXL BAK 2 SKOOL BASH la kukata na shoka wekend hii




 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, July 06, 2009 | | Permalink | Maoni 0

e.tarimo na libeneke lake jipya


Baadhi ya watu watakuwa wamemsoma Mhandisi na Mwelimishaji ndugu Sabato E. Tarimo katika gazeti la MsemaKweli kwenye makala zake mbalimbali. Sasa amejikita katika ulimwengu wa blogu ili kuwafikia wengi zaidi hasa wale wanaoishi nje ya Tanzania.
Jina la Blogu ni tanzaniachristianheritage.blogspot.com Makala alizoandika hadi sasa na zinazotia changamoto ni zile zinazohusu
URITHI na MAVAZI kama vile:URITHI: Mahakama ya kufungulia mirathi
URITHI: Urithi kwa watu wasio na undugu na marehemu...
URITHI: Kumnyima mtu haki ya urithi
URITHI: Umuhimu wa wosia
URITHI: Je, urithi ni haki au ni fadhila?
URITHI: Biblia inasema nini kuhusu watoto wa kambo..
.URITHI: Sheria za mirathi
URITHI: Kwanini mzaliwa wa kwanza alipendelewa?
URITHI: Ni wakati gani wa kurithisha au kurithi?
URITHI: Nani anastahili kurithi?
URITHI: Kiini cha makalaNi vitu gani sisi wanadamu tunavyoweza kurithishan...
URITHI: HAKI NA WAJIBU WAKO pamoja na MKRISTO NA MAVAZI: Mavazi yasiyofaa ni yapi?
MKRISTO NA MAVAZI: Mavazi yatamanishayo ni tishio ...
MKRISTO NA MAVAZI: Dhambi ya Bath-sheba
MKRISTO NA MAVAZI: Makanisa ya kimadhehebu yamepot...
MKRISTO NA MAVAZI: Eti Mungu anaangalia moyo tu?
MKRISTO NA MAVAZI: Mavazi yasiyofaaTafadhali unaombwa kukosoa na kuchangia maoni yako.
Wasalaam Subi, nukta77!
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, July 06, 2009 | | Permalink | Maoni 0

EAST AFRICAN SUMMER COCKTAIL & CHAMPAIGNE PARTY AT ONE OF EXECLUSIVE VENUE IN EAST LONDON




 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, July 06, 2009 | | Permalink | Maoni 1

dada teddy ameagwa rasmi usiku wa kuamkia leo.!

Saturday, July 4, 2009
Bibi harusi mtarajiwa na matroni wake wakiwa katika picha ya pamoja na kamati ya maandalizi iliyohakikisha shughuri ya dada Teddy inafanyika vizuri na kuisha salama wasalimin.
Hizi ni zile za enzi zile ambazo inaelezwa kwa sasa baadhi yao wanazipenda ile mbaya,ati zinawakumbusha mbaali.
Bibi harusi mtarajiwa akitabasamu kwa mbaaali
Matron akiwa ametulia tuliiii

Maharusi watarajiwa na wapambe wao wakipata msosi wa jioni kwa pamoja.
Bibi harusi mtarajiwa na matroni wake wakianza zoezi zima la kukata keki ya upendo na amani mbele ya wageni waalikwa usiku wa kuamkia leo kwenye send off yake ndani ya ukumbi wa banora.
Walipendeza wenyewe na sura zao zikiwa zimejaa tabasamu nene na safi kabisa.
Mc Ephraim Kibonde ndiye aliyekuwa nahodha wa shughuri nzima ya kumuaga dada Theresia usiku wa kuamkia leo.Ukimuhitaji Mc mahiri huyu mpigie no yake ya kiganjani 0713 329234.
Bibi harusi mtarajiwa 'Teddy' na matron wake wakiwasili ndani ya ukumbi wa Banaora usiku wa kuamkia leo
Jukwaa la bibi harusi mtarajiwa na matroni wake palivyopendeza usiku wa kuamkia leo.
Usiku wa kuamkia leo nilikuwa kwenye mnuso wa kumuaga bibi harusi mtarajiwa,dada Theresia alias Teddy kwenye hafla murua kabisa iliofanyika katika ukumbi wa Banora jirani na mlimani City,mwenge jijini Dar.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, July 04, 2009 | | Permalink | Maoni 1



THIS SATURDAY,4TH OF JULY,KUANZIA SAA 3 USIKU AT ZHONG HUA GARDEN,GROOVEBACK nITEWithDJ PETER MOE/KELVIN/RANKIM

Wanakuletea ‘’BACK TO THE 80S SPECIAL’’KAMA NI MKALI WA KU DANCE MIONDOKO YA 80S (MJ) COME N KICK WITH US,NA UJISHINDIE LAKI MOJA.


AND OTHER HUNDRED THOUSAND,KWA ATAKAYE VALIA
MTOKO WA KIZAMANI………

Kwa KIINGILIO CHA SH 5000/=TU..
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, July 04, 2009 | | Permalink | Maoni 0

adamu wa visual lab aula M-Net


Adam Juma, mzee wa Visual Lab amekula shavu kwenye tamthilia mpya ya CHANGES inayooneshwa na kituo cha televisheni cha M-NET. Visual Lab -Next Level- imejipatia umaarufu mkubwa katika siku za hivi karibuni kwa utengenezaji wa video za muziki wa kizazi kipya. Zinapooneshwa video 10 kwenye TV, 8 zimetengenezwa na Visual Lab. Je, kuingia kwenye TV hakutoathiri kazi yake ya utengenezaji video? Ndo swali wanaweza kujiuliza wasanii wa muziki kwa sasa!!! Habari kwa hisani ya abdallah mrisho
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, July 04, 2009 | | Permalink | Maoni 0

albamu kwa ajili yako iko sokoni sasa

Albamu safi ya kwa ajili yako toka kwa msanii Hussein Machozi imeingia sokoni hivi karibuni,inapatikana katika mfumo wa Cassete na Cd, ukihitaji gonga no 0713 131073
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, July 04, 2009 | | Permalink | Maoni 0
Idadi ya watu