wadau mgeni kaingia tumpokee

Monday, December 21, 2009

Pole sana na kazi yako nzito ya kutupa taarifa mbalimbali kwa kupitia blogu yako bab’ kubwa

.Kwa niaba ya kampuni ya King Kipf Productions ya jijini Dar es Salaam, na Blogu ya
http://www.kingkif.blogspot.com/ ninakuomba ututangazie blog yetu hii ya:kingkif.blogspot.com.Kwenye blog yako ili tuweze kuwafikia wanaulimwengu wenzetu mbalimbali ili waweze kupata taarifa ya mambo mbalimbali yanayoendelea kwenye sayari hii.

Kufanikiwa kwa jambo hili itasaidia kwa namna moja ama nyingine watu kupiga hatua kubwa. wako Mkurugenzi King Kif ProductionsSigfred Peter.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, December 21, 2009 | | Permalink | Maoni 0

24 DEC 09 XMASS EVE PARTY READING !!!!!


bongodjs presents xmass eve party on thurs24thdec2009 @the only place 2 be face nite club reading berks rg1 7je from 10pm till 5 o'clock in the morning lets party together entry £10 pls pass msg to others this show sponsored by bongotimes.com for more details contact 078553482158 or 07737800606 dont miss!!!!!!!
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, December 21, 2009 | | Permalink | Maoni 0

Tshalla Muana aifagilia na kuishukuru Club E kwa kumleta nchini Tanzania

Kapt.G Habash akihitimisha mwisho wa onesho la Tshalla Muana kwa wageni waalikwa wa Club E usiku wa kuamkia leo katika hotel ya Naura Springs mjini Arusha
Baadhi ya wafanyakazi wa sigara TCC,mara baada ya kufanya kazi yao ya nguvu walipata wasaa wa kuburudika kama uonavyo pichani
Tshalla akilongoza skwadi lake zima usiku wa kuamkia leo kuwaburudisha washabiki na wanachama wa Club E ndani ya ukumbi wa Kilimanjaro,kwenye hotel ya Naura Springs mjini Arusha
Dansa mahiri wa Tshalla Muana akionesha mcharuko wake jukwaani akiwa hewani
Wanachama na washabiki wa Club E wakiburudika taratiibu huku mwanamama Tshalla Muana akiwatumbuiza kwa nyimbo zake za kimutwashi
Kifaa hiki kinaimba na kucheza ile mbaya,baadhi yao wanasema Tshalla anamuandaa kuwa mrithi wake hapo baadaye,jina lake la kisanii anaitwa MG 30,na kweli MG 30 si masikhara ati
Ama hakika ulikuwa usiku murua kabisa kwa wanachama wa Club E na wageni waalikwa wengine,kwani Tshalla alionesha umahiri mkubwa wa kuimba na cheza na pia kuwaonesha kuwa bado yuko fiti.Mwanamuziki hiyo mwenye madoido kibao jukwaani ameishukuru Club E kwa kumleta hapa nchini na kumfanyia maandalizi mazuri,kama vile haitoshi ailiifagilia sana hoteli yaNaura Springs kwa ukarimu wa wafanyakazi wake pamoja na huduma safi kabisa iliyokuwa akiipata hotelini hapo.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, December 21, 2009 | | Permalink | Maoni 0

ilkuwa ni full mcharuko kwa mashabiki

a






Mashabiki nao hawakukubali kabisa,waliamua kujiachia vilivyo na mmoja wa aimbaji mahiri wa Tshalla ajulikanaye kwa jina la kisanii MG 30 nae bila hiyana aaha safi kabisa
Kupagawa kimtindo kulikuwepo kama hivi,wapiga vyombo wa Tshalla Muana wakiwa wamepandwa na mzuka kiaina
Tshalla Muana akitumbuiza usiku wa kuamkia leo mbele ya wanachama wa Club E na wageni waalikwa wengine

Shoo ilianza na jukwaani palikuwa hapatoshi,madansa wa Tshalla Muana wakilivamia jukwaa kwa namna ya kipekee kabisa
Modozz wa Club E,wako safi ile mbaya
Baadhi ya wafanyakazi wa Naura hotel wakijiburudisha mara baada ya kumaliza kazi
Wageni waalikwa tayari wakiwa ndani ya ukumbi wa kilimanjaro,kumshuhudia malikia wa rhumba usiku wa kuamkia leo
Walimbwende wa Club E wakiwakaribisha wageni waalikwa mbalimbali kwenye onesho hilo lililoambatana na chakula cha usiku
Pichani ndivyo namna ya jukwaa la Tshalla Muana lilivyokuwa kabla ya shoo kuanza
baadhi ya wanachama wa Club E waibadilishana mawazo huku wakipata vinywaji taratibu
Pichani ni Kapt.G Habash akiwakaribisha wanachama wa Club E na wageni waalikwa walipokuwa wakipata chakula cha usiku pamoja na vinywaji

Usiku wa kuamkia leo mwanamuzki mahiri kabisa katika miondoko ya rhumba na mutwash toka jamhuri ya Kongo DRC,Tshala Muana na skwadi lake zima,waliwaburudisha kwa namna ya kipekee wanachama wa Club E walioko mjini hapa Arusha na wageni waalikwa,onesho hilo ambalo liliwavutia wengi lilifanyika katika ukumbi wa mikutano wa Kilimanjaro ndani ya hotel ya Naura Springs usiku wa kuamkia leo.Kampuni ya sigara ya TCC kupitia bidhaa yake ya Embassy ifikapo mwisho wa mwaka huandaa pati/hafla kwa ajili ya kuwashukuru watu mbalimbali wakiwemo wanachama wa Club E
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, December 21, 2009 | | Permalink | Maoni 0

mzigo mpya umeingia MANHATTAN MEN'S WEAR HOUSE

Sunday, December 20, 2009
Men's Shoes
Snikazz
Under Wear
shirts
MANHTATTAN MEN'S WEAR HOUSE
speciallized in Men's Attire Large collection
Muhimbili Hospital round about near Muhimbili Tax/Daladala Stand Next to NMB BANK opposite to NBC Muhimbili Branch.
TEL:+255 712 532777,0754 866434,0715 030090
"All high quality and authetic (Original) from world most famous Designers,Roca Wear,Sean John,Phat Pham,Mecca,Ecko,Nike,Reebok,Adidas,Tommy Hilfiger,Timberland etc.
All size available from little boys to adults,xxxl size are also available
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Sunday, December 20, 2009 | | Permalink | Maoni 4

swimming pool ya naura hotel ndani ya a town

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Sunday, December 20, 2009 | | Permalink | Maoni 0

mie na Jb mpiana

Da wadau nilipata picha ya pamoja na Jb Mpiana alipowasili jijini Dar hivi karibuni ,na kufanya onesho lake la nguvu sambamba na mwanamama matata sana katika mambo ya rhumba Tshalla Muana,raha zote hizo zilipatika ndani ya ubungo plaza baada ya kuletwa na kampuni ya sigara ya TCC kupitia bidhaa yake ya Embassy,ambapo wanachama wa Club E walipata kuburudika ile safi bin sawia.Kama vile haitoshi Tshalla Muana na skwadi lake zima wako mjini Arusha leo kuwatumbuiza Wanachama wa Club E usiku wa leo ndani ya hoteli ya Naura
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Sunday, December 20, 2009 | | Permalink | Maoni 1

New Year's party

Hi all,
Please come and celebrate with us as we start the New Year.. 2010...
It's gonna be awesome enjoy the moment all together!
Spread the word..come one, come all...


New Year’s Party in N.E

WHEN: Saturday, January 2nd
WHERE: CHARLIE’S PUB
14 Cabot St
Lowell, MA 01854

Tel: 978 937 3737

Email: pubchalies@yahoo.com

ADMISSION: $10

Drinks: Cash bar

Door open at 8pm till 2am

RSVP:
INNOCENT (978) 966 7690
STEVEN (603) 320 3220
PERFECTUS (603) 953 3343

Cheers,
Steve.
Note: Please see the attachment for directions/location/time
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Sunday, December 20, 2009 | | Permalink | Maoni 0

serikali kujenga nyumba nane kwa waathirika wa maporomoko wilayani same



SERIKALI imeahidi kujenga nyumba nane kwa ajili ya waathirika wa maporomoko ya Goha wilayani same ambayo yalisababisha watu 24 kufa.Kijiji cha Goha kipo kata ya Mamba Miamba wilayani Same.

Aidha serikali imeahidi kuikarabati skimu ya Goha ambayo iliharibiwa vibaya kutokana na maafa hayo yaliyosababishwa na mvua kubwa zilizonyesha kwa siku tatu mfululizo kuanzia Novemba 9-11 mwaka huu.


Rais Jakaya Kikwete alitoa ahadi hizo jana baada ya kuwatembelea wananchi wa kijiji cha Goha na Kambeni kwa lengo la kuwapa pole wafiwa na kuwafariji sanjari na kujionea athari zilizotokana na tukio hilo.


Pichani JK akiweka shada la maua katika moja ya makaburi ya watu kumi na nne wa familia moja ya Shumbi waliofariki dunia kutokana na maporomoko ya udongo.
SOURCE:FREDDY MARO
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Sunday, December 20, 2009 | | Permalink | Maoni 0

CYTHIA AKAZUBA WA (RWANDA) anyakua taji la MISS EAST AFRICA 2009


Miss East Africa 2009 Cythia Akazuba(Rwanda) akiwa katika pozi mara baada ya kutangazwa mshindi wa shindano hilo lililofanyika usiku wa kuamkia leo kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam.
Miss East Africa Cynthia Akazuba(Rwanda) kati akiwa katika picha ya pamoja na mshindi wa pili Dalysha Doorga kutoka (Mauritius) na Victoria Martin(Tanzania) mshindi wa tatu, waliosimama nyuma ni Majaji ambao pia ni maafisa wa Miss East Africa.
Mkurugenzi wa Prime Time Promotions Juhayna Ajmi katikati akiwa katika picha ya pamoja na wadogo zake Mariam Kulia na Garina kushoto,wakilifuatilia shindano la Miss East Afrika kwa umakini mkubwa.Kwa picha zaidi bofya hapa
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Sunday, December 20, 2009 | | Permalink | Maoni 2

rais karume awatunuku nondo zao wanafunzi wa ifm zanzibar

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Amani Abeid Karume,akimtunuku Shahada ya Kawaida Bimaka Abdalla Moh’d,katika mahfali ya sita ya Chuo cha Uongozi wa Fedha ,Chwaka Mkoa wa Kusini.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Amani Abeid Karume,akimtunuku Shahada ya Kawaida Philemon Pius Mechel,katika mahfali ya sita ya Chuo cha Uongozi wa Fedha ,Chwaka Mkoa wa Kusini.
Baadhi ya wahitimu wa mahafali ya sita ya Chuo cha Uongozi wa Fedha Chwaka,wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Amani abeid Karume alipozungumza nao wakati alipowatunuku shahada jana.

Picha na Ramadhan Othman Ikulu.

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Sunday, December 20, 2009 | | Permalink | Maoni 0

Jb mpiana awakuna vilivyo wanachama wa Club e usiku wa kuamkia leo

Saturday, December 19, 2009
Jb Mpiana akiimba mbele ya wageni waalikwa na wanachama wa Club E
Wote mikono hewani kumpa tafu Jb Mpiana
Washabiki kila wakati walionekana kucharuka ile mbaya, na kuona viti vyao havifai tena kukaliwa,badala yake ni kusebeneka tu
Jb Mpiana akiimba moja ya nyimbo zake mbele ya umati mkubwa uliofika kumshuhudia live ndani ya ukumbi wa ubungo plaza usiku wa kuamkia leo
Skwadi zima la Jb jukwaani

Ilikuwa safi ile mbaya,Jb Mpiana akijituma jukwaani
Mashabiki wa Jb Mpiana wakionesha hisia zao dhahiri kabisa huku wakiimba baadhi ya nyimbo alizokuwa akiimba Jb
Dj Vencha pamoja na Ruge Mutahaba wote kutoka Clouds Fm wakilifuatilia tumbuizo safi kabisa la Jp Mpiana usiku wa kuamkia leo
Wageni waalikwa mbalimbali wakilifutitilia onesho la Jp Mpiana kwa umakini usiku wa kuamkia leo ndani ya ukumbi wa ubungo plaza
Mmoja wa madensa wa kiume wa Jp Mpiana akionesha umahiri wa kuyakata mayenu mbele ya umati mkubwa uliofika ndani ya ukumbi wa ubungo plaza kumshuhudia live Tshalla Muana na nguli huyo kutoka nchini Kongo DRC
Jb Mpiana na densa wake wakijituma jukwaani
Skwadi zima la Jb Mpiana likijituma mbele ya wageni waalikwa wa Club E ndani ya ubungo plaza usiku wa kuamkia leo
Densa wa Jp Mpiana akiwaonesha wanachama wa Club E waliofurika ndani ya Ubungo Plaza,namna ya kujiachia jukwaani,huku miluzi na mayowe yakiwa yametawala ukumbini
Umati wa Wanachama wa Club E wakiburudika vilivyo ndani ya ukumbi wa Ubungo Plaza usiku wa kuamkia leo,mara baada ya kuburudishwa kwa namna ya kipekee kabisa na mwanamuziki nyota kutoka nchini Kongo DRC Jp Mpiana
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, December 19, 2009 | | Permalink | Maoni 6

tshalla amuana akamua vilivyo usiku huu

Mwanamama Tshalla Muana akitumbuiza na densa wake mbele ya wageni waalikwa usiku huu
Madensa wa Tshala Muana wakitumbuiza jukwaani usiku huu mbele ya wageni waalikwa
Raha ndani ya raha usiku huu ndani ya ubungo plaza,kama uonavyo pichani mmoja wa madansa wa Tshalla Muana akijiachia vilivyo jukwaani usiku huu mbele ya mashabiki ambao nao hawakutaka kuketi vitini,badala yake wakaliunga libeneke, ama hakika shoo iko safi kabisa usiku huu,hii ni awamu ya kwanza ya Tshalla Muana
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, December 19, 2009 | | Permalink | Maoni 0

jb mpiana/tshalla muana kutoana jasho usiku huu ubungo plaza

Friday, December 18, 2009
Da' Lulu kutoka kampuni ya sigara TCC kupitia chapa ya Embassy akiwapa maelekezo mafupi walimbwende wa Club E usiku huu hapa ubungo plaza kwa ajili ya kuwapokea wageni waalikwa watakaohudhuria onesho la Jb Mpiana pamoja na Tshalla Muana
Dada Lulu kutoka kampuni ya sigara TCC kupitia chapa ya Embassy akiwaremba walimbwende wa Club E usiku huu hapa ubungo plaza kwa ajili ya kuwapokea wageni waalikwa watakaohudhuria onesho la Jb Mpiana pamoja na Tshalla Muana
Jukwaa ambalo litawaka moto usiku wa leo kati ya Jb Mpiana na skwadi lake pamoja na Tshalla Muana nae akiwa na skwadi lake zima,ndani ya ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar.
Pichani ni sehemu ya wageni waalikwa wa Club E watakapoketi na kushuhudia live onesho la Jb Mpiana sambamba na Tshalla Muana usiku wa leo,ambapo wanachama wa Club hii watajiachia kwa msosi safi kabisa na kuburudishwa na wanamuziki hao mahiri kutoka Kongo DRC

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Friday, December 18, 2009 | | Permalink | Maoni 2

ijumaa ya mjengoni leo mchana











Wafanyakazi wa kampuni ya Clouds Media Group/Prime Time Promotions leo mchana wamejiachia vilivyo na nyama choma ya mbuzi bila kusahau kitu cha kuku kwa ndizi pale mjengoni kwao,Mikocheni jijin Dar,ama kwa hakika ijumaa ya leo ilikuwa safi ile sawia,halafu na piaa leo ni mwanzo wa wikend hivyo watoto wa mjengoni walikuwa wanajibust mapema ikiwa ndiyo kwaanza kama vile kianzio cha muendelezo wa sikukuu zijazo.SAFI.!
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Friday, December 18, 2009 | | Permalink | Maoni 0

Sugu: Bado saa 144 za tambiko la Bogo Flava



Galacha wa Hip Hop nchini, Joseph Osmund Mbilinyi ‘Mr. II’ amebakiza siku sita au saa 144 kuzindua albamu yake ya 10, ambayo inaundwa na mawe 10 ya adabu na muda ukifika, itakatiza mtaani kwa jina la Veto.
Mr. II a.k.a Sugu ataitambulisha albamu hiyo Desemba 24, 2009 (Mkesha wa Krismasi), katika Ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam, katika shoo ambayo inachukuliwa kama tambiko la Bongo Flava, kwamba baada ya hapo muziki wa kizazi kipya utarudi kwenye chati yake.


Albamu hiyo, Sugu ameiandaa nchini Marekani, kwenye Studio ya S&S Records iliyopo Brooklyn chini ya maprodyuza, Stiggo na Puzo.Wana-Hip Hop wenye heshima Bongland kama Joseph Haule ‘Prof. Jay’, Msafiri Kondo ‘Solo Thang’, Hamis Mwinjuma ‘MwanaFA’, John Simon ‘Johmakini’ na Ahmed Dolla ‘Balozi’ kwa pamoja wameingiza vocal kwenye albamu hiyo.“Nataka watu waone harakati zetu na jinsi tunavyoutetea muziki wetu, Bongo Flava haiwezi kufa, wanaobisha waje Diamond Jubilee, waone jinsi tunavyoutambia muziki wetu kwenye Mkesha wa Krismasi,” alisema Sugu.Picha na habari kwa hisani ya Mrisho Blog
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Friday, December 18, 2009 | | Permalink | Maoni 0

patakuwa hapatoshi kesho pta

Bondia Francis Cheka akifanya mahojiano vyombo vya habari leo asubuhi kuhusiana na pambano lake la kesho dhidi ya mpinzani wake Enrique Areco kutoka Anjentina
Kulia ni bondia Festus Omondi kutoka nchini Uganda atakaye pambana na hasimu wake Mbwana Matumla (kulia) katika raudi 12,uzito wa Bantam Weight.Mbwana Matumla ana uzito wa Kg 53 na Festus Omondi ana Kg 51

Bondia Festu Omondi kutoka Uganda akipima uzito leo mchana ndani ya ukumbi wa Idara ya habari Maelezo
Mbwana Matumla naye akipima uzito tayari kwa pambano lao kesho jioni ndan ya ukumbi wa PTA,Sabasaba,Temeke jijini Dar

Pichani kati ni Rais wa chama cha ngumi za kulipwa Tanzania (PST),Emmanuel Mlundwa akizungumza mbele ya waandishi wa habari leo asubuhi ndani ya ukumbi wa Idara ya habari Maelezo kuhusiana na mpambano wa masumbwi utakaofanyika kesho jioni katika ukumbi wa PTA.Kulia ni bondia Mbwana Matumla na shoto ni Festus Omondi kutoka Uganda



Katika kuhakikisha kuwa inajikita kwenye burudani zote hapa nchini Tanzania, kampuni ya Prime Time Promotions Ltd imeandaa pambano kubwa la masumbwi ya kulipwa la kimataifa kugombea ubingwa wa dunia, litakalofanyika December 19 2009 (kesho) kwenye ukumbi wa PTA jijini Dar es salaam.

Kutakuwa na michezo miwili mikubwa, ambayo ni ya kugombea ubingwa wa dunia wa UBO, na WBC, ambalo litawahusisha bondia kutoka Morogoro Tanzania Fransis Cheka, dhidi ya bondia Enrique Areco kutoka nchini Argentina.Pamoja na pambano hilo, pia kutakuwa na pambano lingine kubwa, ambalo litawahusisha bondia toka Dar es salaam Tanzania Mbwana Matumla dhidi ya Festus Omondi kutoka Uganda, ambao watagombea pia mataji mawili, ambayo ni ICB na UBO.

"Sababu kubwa ya kugombewa kwa mataji hayo manne, mawili kwa kila mchezo, yanatokana na mabondia wote wanne kuwa na mikanda ambayo yote kwa pamoja inalazimika kuwekwa mezani, na mshindi atachukuwa mikanda yote miwili.Fransis Cheka ni bingwa wa dunia wa UBO huku Enrique Areco akiwa ni bingwa dunia wa WBC, kwa maana hiyo mabondia wote wawili wamekubali kuweka mikanda yao mezani ili igombewe, na kufanya atakaekuwa bingwa kufanya kazi kubwa ili kupata mikanda yote",Alifafanua Mlundwa.

Mbwana, bingwa wa zamani wa IBO wa dunia ambae ni bingwa wa ICB atapigana na bondia toka Uganda Festus Omondi katika kugombea ubingwa wa ICB huku UBO, Universal Boxing Organization Intercontinental ikitoa ofa ya mabondia hao pia kugombea ubingwa wao katika bantamweight pia siku hiyo .


Matumla ni bondia mzoefu akiwa na rekodi ya kuvutia akishinda mapambano 18 (10 kwa knockout) akipoteza 4 , na pia ni bingwa wa zamani wa WBA Intercontinental na ambae alishinda taji la IBO la dunia mwaka 2006 kwa kumchapa Eric Barcelona wa Philippines. Festus Omondi bondia wa Uganda anaeishi mjini Kurume Fukuoka nchini Japan, ana rekodi ya kushinda mapambano manane kati ya tisa.
Pambano hilo litakalokuwa la aina yake limedhaminiwa na kampuni ya simu za mikononi ya Zain,Red Bull pamoja benki ya CRB

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Friday, December 18, 2009 | | Permalink | Maoni 2

Wadau wakishoo love na Jb mpiana

JB Mpiana akiwa na Father Kidevu (kulia) na DJ Omy E-Master baada ya kuwasili kwa nyota huyo mahiri wa muziki wa dance kutoka DRC.
Mdau Jackson a.k.a suka akiwa amepozi na Mwanamuziki mahiri wa Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo DRC ,aiishie na kufanya kazi zake nchini Ufaransa JB Mpiana mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam 23:54 usiku wa kuamkia leo. Jb Mpiana anafanya onesho lake leo usiku ndani ya Ubungu Plaza na Nyota mwenzake Tshalla Muana kwa ajili ya kuwaburudisha wanachama wa Club E
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Friday, December 18, 2009 | | Permalink | Maoni 0

Diana Ibrahim ndiye kinara wa miss kisura Tanzania 2009


Mama Tunu Pinda (ambaye amechaguliwa kuwa mlezi wa kituo cha kulea watoto yatima cha mkoani Rukwa) akipokea hundi yenye thamani ya shilingi milioni mbili kutoka Kampuni ya bia Serengeti aliyopewa na Meneja uhusiano wa kampuni ya bia Serengeti, Teddy Mapunda,katikati ni Jaji mark Bomani mwenyekiti wa kampuni ya bia Serengeti akishuhudia tukio hilo. Fedha hizo zimetolewa kwa ajili ya kituo cha yatima kilichopo mkoani Rukwa na pia wamepewa mtaji wa kreti 20 za vita malta (kinywaji kisicho na kilevi) pamoja na cooler kama mtaji wa kuanzia kwa ajili ya kusaidia kuendesha kituo hicho.
Juddy ambaye ni mwandaaji wa Shindano la Kisura Tanzania akimkabidhi mshindi hundi yenye dhamani ya shilingi milioni tano mshindi wa kwanza wa shindano hilo Diana Ibrahim.
Mama Tunu Pinda akikabidhiwa zawadi ya maua na mshindi wa kwanza katika shindano la Kisura wa Tanzania 2009 Diana Ibrahim.Mshindi wa Miss Kisura Tanzania 2009 (katikati) Diana Ibrahim akiwa na washiriki wenzake waliofanikiwa kuingia tano bora.
John maprint print akiwa na wadau wengine hakuwa nyuma katika kushuhudia shindano hilo la kumtafuta kisura wa Tanzania 2009 iliyofanyikia katika hoteli ya movenpick jijini Dar es salaam. Huyu nae hakuwa nyuma katika kushuhudia shindani hilo.

Mgeni Rasmi mama Tunu Pinda akisoma hotuba yake katika shindano la Kisura wa Tanzania 2009 lililofanyika kwenye Hoteli ya Movenpick usiku wa kuamkia leo jijini Dar, kushoto ni Mwenyekiti wa Kampuni ya bia ya Serengeti Jaji Marck Bomani na kulia ni Teddy Mapunda Meneja uhusiano wa kampuni ya bia Serengeti.
Teddy Mapunda Meneja uhusiano wa kampuni ya bia Serengeti akisoma risala.

Mwanadada Vannesa kutoka Choice Fm 102.6 ndiye aliyekuwa mshereheshaji wa shindano la Miss Kisura Tanzania 2009.
Wageni waliohudhuria shindano la Kisura wa Tanzania 2009.

Wageni waliohudhuria shindano la Kisura wa Tanzania 2009.
Wageni waliohudhuria shindano la Kisura wa Tanzania 2009.
Mama wa mitindo Asia Idarous (wa pili kutoka kulia) nae alikuwepo kushuhudia tukio hilo.

Baby Madaha akionyesha umahiri wake katika kumiliki jukwaa kwenye shindano la Kisura wa Tanzania.

Belle 9 kutoka mji kasoro bahari akiwaburudisha wageni waliohudhuria shindano la Kisura wa Tanzania.

Kikundi cha ngoma na sarakasi cha Splendid nacho hakikuwa nyuma kutoa burudani.

Ally Rehmtullah (wa pili kutoka kushoto) mbunifu wa mavazi akiongoza jopo la majaji wa mashindano ya Kisura wa Tanzania 2009.

Wazee wa Goba Kalunde Band iliburudisha vya kutosha katika shindano hilo.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Friday, December 18, 2009 | | Permalink | Maoni 1

New Year Eve Bash in Canton Ohio---USA


TANZANIANS ASSOCIATION OF CANTON OHIO---USA INVITES YOU...

Tired of bringing in the new year in the same way every year?

Make this year a year to remember! The Tanzania Associan of Canton presents,

a New Year bash at Lollies Banquet hall of Belden Village.

$5.00 cover charge at the door. Food, drinks, and fun!

Music by DJ Kvelli of Columbus. Rap, Hip-Hop, and much more!

Call 330-418-6401 or 330-575-7148 for V.I.P and info.


Lolli's Restaurant and Banquet Center
4801 Dressler Road NW.
Canton, Ohio 44718
Call: 330.492.6846
Toll Free: 1.877.GOLOLLI
(1.877.465.6554)
Fax: 330.492.0836
lollisrestaurant@aol.com

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Friday, December 18, 2009 | | Permalink | Maoni 0

jb mpiana atua dar usiku huu tayari kuwaburudisha wanachama wa club e

Jb Mpiana akiwa amepozi na wadhamini wake,shoto ni Meneja msaidizi wa sigara ya Embassy Elizabeth Kirimbai Ndosi pamoja na Afisa masoko wa Embassy Joackim Kyula
Jb Mpiana na kundi lake walipiga picha ya pamoja mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam 23:54 usiku wa kuamkia leo. Kushoto kwake ni Meneja Msaidizi wa Sigara Embassy, Elizabeth Kirimbai Ndosi.
Mwanamuziki mahiri wa Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo DRC ,aiishie na kufanya kazi zake nchini Ufaransa JB Mpiana akipunga mkono kutoa salamu baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam 23:54 usiku wa kuamkia leo. Kushoto kwake ni Meneja Msaidizi wa Sigara Embassy, Elizabeth Kirimbai Ndosi.
Mwanamuziki nyota kutoka Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo DRC aiishie na kufanya kzi zake nchini Ufaransa JB Mpiana akiwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam mnamo majira ya 23:54 usiku wa kuamkia leo. Kushoto kwake ni Meneja Msaidizi wa Sigara Embassy, Elizabeth Kilimbai Ndosi akiwa na walimbwende wa Club E.
Mwanamuziki Mahiri wa Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo aiishie na kufanya kzi zake nchini Ufaransa JB Mpiana akiwa ameambatana na wadhamini wake mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaama mnamo majira ya saa 23:54 usiku wa kuamkia leo. Kulia kwake ni Meneja Msaidizi wa Sigara Embassy, Elizabeth Kirimbai Ndosina kushoto kwake ni Mwamama Yasmin aliyeambatana naye pamoja afisa masoko wa Embasy Joackim Kyula.


Jb Mpiana amewasili usiku wa kuamkia leo jijini Dar na kundi lake tayari kwa onesho lao la pamoja na mwanamuziki mwingine nyota kutoka Demokrasia ya Kongo Tshalla Muana ambaye aliwasili toka jana jioni akiwa na skwadi lake zima,tayari kwa ajili ya kuwaburudisha wanachama wa Club E na wadau wengine,onesho hilo litafanyika leo jioni Ubungo Plaza jijini Dar na Arusha,Wakazi wa Arusha kaeni mkao wa kula wana wa Club E wanawaletea burudani murua kabisa ya kufunga mwaka.Suala ama namna ya kupata tiketi yako angalia tangazo hilo hapo chini utabaini tiketi yako utaipataje.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Friday, December 18, 2009 | | Permalink | Maoni 0

KUMBUKUMBU YA MWAKA MMOJA YA MAMA YETU MPENDWA-KUTOKA KWA A.Y

Thursday, December 17, 2009

Leo ni Mwaka mmoja tangu Mama yetu mpendwa LIDYA ANANIA YESSAYAH alipotutoka ghafla hapa Duniani na kutuachia pengo lisilozibika katika Familia.


·Japokuwa haupo nasi hapa duniani lakini tupo nawe Kiroho kwa kuendeleza mema yote uliyotufundisha na kutuasa.Tunakukumbuka kwa Upendo, Busara, na Ukarimu uliokuwa nao kwa familia na marafiki.


·Daima unakumbukwa sana na watoto wako wapendwa John, Summa, Ambwene na Mage..Unakumbukwa na Baba yako, ndugu zako, washarika, majirani, jamaa na Marafiki zako wote.


MSHUKURUNI BWANA KWA KUWA NI MWEMA KWA MAANA FADHILA ZAKE NI ZA MILELE.

(Ufunuo 14:13)
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, December 17, 2009 | | Permalink | Maoni 1

mdau anaomba kufahamu zaidi kuhusu freemasons


Kuna mdau kanitilia maguu, anataka kujua namna hawa watu wenye imani za Freemasons ni watu wa aina gani na wana mahusiano gani na freemasons,na freemasons ni nini na imani zao zikoje?je tunao hapa bongo ? je ni mtu yeyote tu anaweza akajiingiza katika imani hizo ?Kumradhi wadau kwa wale wenye weredi wa haya mambo si vibaya wakatupa somo kuhusu yote yahusuyo freemasons.


NB:Mimi nilichoweza kumjibu,nilimwambia inawezekana wapo kwa sababu wana jumba lao (pichani) lilipo barabara ya Sokoine Drive jijini Dar,tena lipo jirani kabisa na Benki kuu
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, December 17, 2009 | | Permalink | Maoni 8

rais jk akizungumza na washiriki wa mis east afrika ikulu

Rais Jakaya Kikwete akizungumza na warembo kutoka mataifa mbalimbali wakati alipowakaribisha Ikulu jana kwa chakula cha jioni, warembo walipata nafasi ya kumuuliza rais maswali mbalimbali kuhusu mambo mbalimbali ya jamii uchumi michezo na mengine mengi.warembo hao kutoka mataifa saba wanatarajia kupanda jukwaani kesho katika kinyang'anyiro kitakachofanyika kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar ,ambapo mshindi wa shindano hilo atajinyakulia gari aina ya Toyota Celica Sports yenye thamani ya dolla 24.000.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, December 17, 2009 | | Permalink | Maoni 0

STILL BLAZIN' THE ALBUM THIS FRIDAY @ SWEET EASY


"ONE THING ABOUT GOOD MUSIC, WHEN IT HITS. YOU FEEL NO PAIN"
THIS FRIDAY @ SWEET EASY LOUNGE-OYSTERBAY, COME AND PARTY TO SOME SIZZLIN' TUNES, WITH EAST AFRICA'S FINEST DJ, AMO "THE NITRO" BLAZE & DA HOMEBOYZ SPINNING THE HOTTEST HIP HOP, Rn,B, RAGGA AND UTAKE (NEW AND OLD SKOOL) giving you a taste of the hottest mixtape.
PARTY STARTS @ 10PM FOR ONLY 5K
SEE U THERE.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, December 17, 2009 | | Permalink | Maoni 0

msiba greece


JUMUIYA YA WATANZANIA NCHINI GREECE INATANGAZA MSIBA WA NDUGUYETU MPENDWA BW.SAIDI MACHALA KILICHOTOKEA JUZI TAR 14/12/09 KTK HOSPITALI YA SUTIRIA MWENYE NGUO NYEUSI AMBAE ALIKUA KIPA WETU NO 1.MPANGO WA KUMSAFIRISHA MWILI WA MAREHEMU KWENDA NYUMBANI TANZANIA KWA MAZISHI UNAENDELEA.MWENYEZIMUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHARI PEMA PEPONI AMMIN.KWA LAZAIDI LITAKALOENDELEA TUTAPEANA TAARIFA,
BY HAJIEZ.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, December 17, 2009 | | Permalink | Maoni 1

Dj Young kim magomelo azikwa leo

Wadau mbalimbali wakimzika marehemu Dj Kim Abdulhakhim Magomelo leo jioni makaburi ya kisutu jijin Dar
Kutoka kulia ni Wakurugenzi wa Clouds Media Group Ruge Mutahaba na Joseph Kussaga wakiwa na wadau wengine wa burudani katika mazishi ya Dj Kim Abdulhakhim Magomelo yaliofanyika leo saa kumi jioni kwenye makaburi ya Kisutu, Kim alifariki jana jioni akisumbuliwa na matatizo ya ugonjwa moyo, pumu na homa ya matumbo Typhoid kwenye Hospitali ya Saint Monica iliyoko Manzese jijini Dar es salaam inayojishughulisha na kutibu magonjwa ya moyo na ameacha mke na watoto watatu.

Kim atakumbukwa na wapenda burudani kote nchini kwa mchango wake katika burudani alikuwa dJ mzuri na aliwahi kuandaa mashindano mengi ya kucheza Disco ambayo yaliwakutanisha wakali mbalimbali katika kucheza Disco wakiwemo akina Sammy Cool, Marehemu Black Mosses, Bob Rich na wengine wengi waliokuwa maarufu sana katika kucheza Disco zamani.

Kim Pia aliwahi kuandaa Bonanza lililokuwa likijulikana kama Yo Rap Bonanza lililokutanisha vijana wengi katika muziki wa Kughani

Mungu aiweke mahali pema peponi roho ya Marehemu Abdulhakhim Magomelo AMEN.


Waombelezaji wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa marehemu Abdulhakim Magomelo maarufu kama DJ Young Kim wakielekea katika makaburi ya Kisutu jijini Dar leo jioni
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, December 17, 2009 | | Permalink | Maoni 0
Idadi ya watu