MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL MGENI RASMI SHEREHE ZA MKESHA WA MAULID MNAZI MMOJA DAR

Sunday, February 5, 2012
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi, wakati alipowasili kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja katika shambrashambra za mkesha wa sherehe za Maulid, jijini Dar es Salaam jana Februari 04, 2012 usiku.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal(katikati) Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi na Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowasa, wakiwa katika sherehe za mkesha wa Maulid, zilizofanyika usiku wa kuamkia leo, jana usiku Februari 04, 2012, katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiteta jambo na Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowasa, wakati wakiwa katika sherehe za mkesha wa Maulid, zilizofanyika usiku wa kuamkia leo, jana usiku Februari 04, 2012, katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Muumin wa dini ya kiislam kutoka Msikiti wa Suni Hanafi wa jijini Dar es Salaam, Muzamil Chaki, akiimba Qaswaida jukwaani kutoa burudani wakati wa mkesha wa sherehe za Mauilid zilizofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini jana usiku Februari 04, 2012
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Muumin wa dini ya kiislam kutoka Msikiti wa Suni Hanafi wa jijini Dar esSalaam, Muzamil Chaki, baada ya muumini huyo kumaliza kutoa burudani ya Qaswaida jukwaani, wakati wa mkesha wa sherehe za Mauilid zilizofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini jana usiku Februari 04, 2012. Picha na Muhidin Sufiani-OMR

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Sunday, February 05, 2012 | | Permalink | Maoni 0

rais kikwete AONGOZA MATEMBEZI MIAKA 35 YA CCM JIJINI MWANZA LEO

Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kiwkete akiwasalimu wananchi baada ya kufika mwisho wa matembezi hayo kwenye Viwanja vya Furahisha jijini Mwanza.
Rais Kikwete akimsalimia Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye kabla ya matembezi hayo kuanza.
Rais Kikwete akimsalimia Katibu Mkuu wa CCM mstaafu, Philip Mangula kabla yamatembezi kuanza Ofisi ya CCM mkoa wa Mwanza. Kulia ni Katibu Mkuu Mstaafu pia,Yussuf Makamba.


Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akiwasili kwenye Ofisi ya CCM mkoa wa Mwanza kuongoza matembezi ya mshikamano kwa ajili ya maadhimnisho ya miaka 35 ya CCM leo asubuhi. Anayempokea ni Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara),Pius Msekwa na wengine ni Spika wa Bunge Anna Makinda ambaye ni mlezi wa mkoa huo na Katibu Mkuu wa CCM,Wilson Mukama. Pamoja na Rais Kikwete ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mwanza Clement Mabina na Mkuu wa mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilllo.
Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, Mama Salma Kikwete wakiongoza matembezi hayo kutoka kwenye Ofisi ya CCM mkoa wa Mwanza hadi viwanja vya Furahisha jijini humo akiwa na viongozi wa ngazi ya juu wa CCM. Kutoka Ofisi hiyo hadi kwenye viwanja ni umbali wa kilometa tatu.
Wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya mkoa wa Mwanza wakiwa kwenye Ofisi ya CCM mkoa huo tayari kushiriki matembezi hayo.
Kijana Mussa aliyemwagiwa tindikali wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo jimbo la Igunga mwaka jana, akishiriki matembezi hayo. Wapili kushoto ni Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye.
Katibu Mkuu wa CCM Wilson Mukama akiwa na Makatibu wastaafu wa CCM, Yussuf Makamba na Philip Mangula kabla yamatembezi kuanza.
Sungusungu wakionyesha ukakamavu wao baada ya Kikwete kuwasili nba matembezi hayo kwenye viwanja vya Furahisha.
Matembezi yakiingia kwenye Viwanja vya Furahisha.
Wananchi wakiushangilia msafara wa matembezi hayo ulipopita eneo la mtaa wao.
Vijana wa Sungusungu wakijifua kabla ya matembezi kuanza.Picha na Bashiri Nkoromo.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Sunday, February 05, 2012 | | Permalink | Maoni 0

Sakata La Mgomo Wa Madaktari; Tafsiri Yangu


Ndugu zangu,

Mgomo wa madaktari wetu ni habari kubwa. Umeingia sasa kwenye wiki ya
pili. Hata kama ungekuwa ni wa siku mbili, bado ungesababisha madhara makubwa kwa nchi. Kwamba sasa una zaidi ya siku kumi na nne ni balaa kubwa kwa nchi yetu.

Tafsiri yangu;

Uliopo ni mgogoro kati ya madaktari na Serikali. Na kwenye mgogoro
kama huu, siku zote, wenye kuathirika zaidi ni wananchi walio wengi. Ni ukweli, kuwa karibu kila Mtanzania anayeamka asubuhi, ama ni mgonjwa au ana ndugu, jamaa au rafiki aliye mgonjwa.

Hivyo basi, kuna mamilioni ya Watanzania wenye kutaabika kila siku na
maradhi ya aina mbali mbali. Ni Watanzania wenye kutegemea sana huduma ya tiba inayotolewa na
madaktari wetu. Na katika nchi zetu hizi, daktari ni rafiki muhimu sana wa mwananchi.

Ni jambo baya sana, pale Serikali inapoingia kwenye mgogoro na
madaktari. Inapoingia kwenye mgogoro na marafiki wa wananchi. Hakuna mahali popote duniani wananchi wakatokea kuwachukia madaktari. Hivyo basi, ni balaa pia pale Serikali inaposhindwa kumaliza tofauti zake na madaktari wa wananchi kwa njia ya mazungumzo na hata kufikia hatua ya madaktari kugoma.

Katika nchi zetu hizi, mganga wa tiba aliyesomeshwa kwa fedha za
walipa kodi na kwa miaka mingi anahitajika sana. Mganga wa tiba msaidizi anahitajika sana. Na
hata kama angelikuwapo Msaidizi wa Mganga Msaidizi wa tiba , naye angehitajika sana. Vivyo
hivyo kwa wakunga wakuu na wasaidizi, wauguzi wakuu na wasaidizi wao. Wote hao wanahitajika sana.

Na katika nchi zetu hizi, Serikali hazipaswi kufikia hatua ya
kuwatisha na hata kuwafukuza kazi madaktari. Hilo la mwisho lifanyike tu pale ambapo njia nyingine zote za kumaliza tofauti na kusuluhisha migogoro na madaktari zitakapokuwa zimeshindikana. Na
kwanini ishindakane?

Tufanye nini sasa?

Taarifa kwamba Kamati ya kudumu ya Bunge inayohusika na masuala ya
huduma za jamii imepanga kukutana na madaktari wetu ni hatua njema na ya busara.
Maana, katika mgogoro huu taarifa zimekuwa zaidi za upande mmoja; upande wa Serikali. Ni
wakati sasa pande zote mbili zikasikilizwa na Kamati hiyo ya Bunge. Ndio, ni wakati pia hata
madaktari wetu wakapewa nafasi tuwasikie.

Huu si wakati wa kufanya ’ propaganda’ za kisiasa kwenye masuala ya
afya za wananchi. Na hata pale Waziri wa Afya alipokaririwa jana Bungeni akitamka kuwa
hali ya huduma za mahospitalini zimerejea katika hali yake ya kawaida ni mfano wa ’
Propaganda’ za kisiasa ambazo Watanzania hatuzihitaji kwa sasa.

Hivi ni hali gani hiyo iliyorejea kwenye kawaida yake
kwenye hospitali zetu baada ya mgomo huu wa madaktari unaoendelea
sasa? Kwamba askari wetu wa Jeshi la Wananchi wamelazimika kwenda kutibu wagonjwa
Muhimbili hiyo haiwezi kuwa ni ’ Hali ya kawaida’. Kwamba madaktari wameripoti lakini
hawaonekani mawodini hiyo haiwezi kuwa ’ hali ya kawaida’. Na kama ni kawaida, hivi ni nini
tafsiri ya ’ kawaida’?

Hapa kuna ukweli unaopaswa kusemwa, na si kitu kingine bali ni ukweli.
Watanzania tunataka kujua; ni kwanini watendaji wa Wizara husika wameshindwa kulitatua
suala la madaktari wetu na hata kutufikisha hapa tulipo?

Yumkini, kulikuwa na hali ya kuyapuuzia madai ya madaktari
katika hatua za awali. Yawezekana pia watendaji wa Wizara hawakuwa
karibu na wawakilishi wa madaktari hao ili kutoa fursa ya kuongea na kutafuta ufumbuzi wa
tatizo. Labda ndio maana tumefika mahali sasa mgogoro umekomaa na wahusika kuonyesha hali ya
kutunishiana misuli. Kuna mahali kosa limefanyika. Ni wapi?

Ndio hapa, kuwa hata kama Kamati ya Bunge itafaulu kusuluhisha mgogoro huu, bado
Watanzania tutahitaji iundwe Tume huru itakayochunguza namna watendaji
wa wizara husika walivyolishughulikia suala hili kwa upande wao.

Tume hiyo itusaidie kuupata ukweli mzima ili kama taifa, tujifunze. Na
wakati tume kama hiyo itakapokuwa ikifanya kazi yake, itakuwa ni busara, kwa watendaji wakuu
wa wizara husika wajiweke pembeni kwa maana ya kujiuzulu ili kupisha uchunguzi huo.

Kama Tume itabaini kuwa hakukuwa na mapungufu makubwa katika utendaji
wao na hususan walivyolishughulikia suala hili la mgogoro na madaktari, basi, itajulikana hivyo, na wana nafasi ya kurudi tena kwenye nafasi za utendaji Serikalini. Inahusu umma kurudisha imani yake kwa Serikali yao. Ndio maana ya umuhimu wa wahusika kupisha pembeni kuruhusu uchunguzi ufanyike. Maana, haitakuwa busara kuliacha suala hili likapita kama yanavyopita mengine ilihali
limegharimu maisha ya Watanzania.

Na kubwa zaidi kwa sasa, ni kwa pande zote katika mgogoro huu
kutambua; kuwa kwa sasa mvutano unaoendelea hautatoa mshindi, ni kwa vile, katika kilichotokea
na kinachoendelea kufanyika sasa, sote, kama taifa, tumeshindwa. Huu ni wakati wa kutanguliza busara na hekima. Tufanye yote, lakini, njia mujarab ya kutanzua mgogoro huu uliopo sasa ni mazungumzo katika mazingira ya kuheshimiana, basi.

Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Afrika.

Maggid Mjengwa,

Dar es Salaam,
Jumamosi, Februari 4, 2012
http://mjengwablog.com
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Sunday, February 05, 2012 | | Permalink | Maoni 0

rais kikwete AWASILI MWANZA TAYARI KWA SHEREHE ZA MIAKA 35 YA CCM

Saturday, February 4, 2012
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mtoto Maganga mwenye umri wa miaka mitatu ambaye pamoja na mama yake walikuwa katika mojawapo ya vikundi kadhaa vya ngoma za asili zilizomlaki uwanja wa ndege wa Mwanza leo January 4, 2012 alikotua tayari kwa kujiunga na wana CCM kusherehekea miaka 35 ya chama hicho tawala.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipokewa katika  uwanja wa ndege wa Mwanza leo January 4, 2012 alikotua tayari kwa kujiunga na wana CCM kusherehekea miaka 35 ya chama hicho tawala.Picha na IKULU.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, February 04, 2012 | | Permalink | Maoni 0

Vodacom Tanzania umeongeza offer kwa siku saba(7)zingine tena za kuendelea kunufaika na promosheni yao.

Ndugu wateja Mtandao wenu wa Vodacom Tanzania umeongeza  offer kwa siku saba(7)zingine tena za kuendelea kunufaika na promosheni ya kutuma SMS kwa Tsh 25 siku nzima kwenda mitandao yote nchini,Na Ongea kwa ROBO SHILINGI kwa sekunde Voda kwa Voda saa 4 usiku hadi 1 asubuhi,Tafadhal Piga*100#ujiunge. 
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, February 04, 2012 | | Permalink | Maoni 0

MH. NYALANDU ATEMBELEA UBALOZI WA TANZANIA, WASHINGTON, DC


 Kutoka kushoto ni Afisa Mindi Kasiga, Afisa Suleiman Saleh, Dr Switebert Mkama, Kiongozi wa kambi ya Upinzani Bungeni, Mh. Freeman Mbowe, Waziri kivuli wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mh. Ezekia Wenje, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mh. Lazaro Nyalandu, Afisa Kiju, Kaimu Balozi, Mh. Lily Munanka, Afisa Abbas Missana, Afisa Agnes Lusinde, Afisa Edward Masanja na Brigedia Jenerali Maganga wakiwa katika picha ya pamoja.
 Kushoto ni Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mh. Lazaro Nyalandu akiwa na Kiongozi wa kambi ya Upinzani Bungeni, Mh. Freeman Mbowe (CHADEMA).
Kushoto na Dr, Switebert Mkama akiwa na Afisa Mindi Kasiga.
 Kushoto ni Afisa Edward Masanja akiwa na Afisa Agnes Lusinde.
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara wa Tanzania, Mh. Lazaro Nyalandu (kulia) akiwa pamoja na Waziri kivuli Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Ezekia Wenje wakiwa kwenye mkutano na Maofisa wa Ubalozi wa Tanzania Nchini Marekani, Ijumaa February 3, 2012 katika Ofisi za Ubalozi wa Tanzania, Washington, DC.
Kaimu Balozi Mh. Lily Munanka (kulia) akiwa na Maafisa Ubalozi kutoka kushoto, Suleiman Saleh na Abbas Missana katika mkutano huo.
 Kutoka kushoto ni Maafisa, Brigedia jenerali Maganga, Mama Kiju na Suleiman Saleh wakiwa katika mkutano huo.
 Waziri wa Viwanda na Biashara, Mh. Lazaro Nyalandu akisaini kitabu cha wageni.
 Kiongozi kambi ya Upinzani Bungeni, Mh. Freeman Mbowe akisani kitabu cha wageni.
Waziri kivuli wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kiamtaifa, Mh. Ezekia Wenji akitia saini kitabu cha wageni.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, February 04, 2012 | | Permalink | Maoni 0

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AKAGUA UJENZI WA SHIRIKA LA ELIMU KIBAHA, AZINDUA TAASISI YA UTAFITI WA MARADHI YA MALARIA, BAGAMOYO

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, (katikati)akikata utepe kuzindua Kituo cha Taasisi ya utafiti wa maradhi ya Malariakilichopo Bagamoyo, wakati alipokuwa katika ziara yake ya Wilaya ya Bagamoyo, mkoa wa Pwani jana Februari 03, 2012
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,akitembelea na kukagua jengo la Shirika la Elimu Kibaha, wakati akimalizia ziara yake yaWilaya ya Kibaha Mkoa wa Pwani leo Februari 04, 2012. Kushoto ni Dkt. Isaack Lwali (wa pili kushoto) ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Elimu Kibaha, Dkt. Cyprian Mpemba.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungno wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Dkt. Isaack Lwali (wa pili kulia) wakati alipotembelea na  kukagua ujenzi wa Jengo la Shirika la Elimu Kibaha, wakati akiwa katika ziara yake yaWilaya ya Kibaha mkoa wa Pwani leo Februari 04, 2012. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Elimu Kibaha, Dkt. Cyprian Mpemba.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muunganon wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitembelea na kukagua ndani ya jengo la Shirika la Elimu Kibaha, wakati alipokuwa katikaziara yake ya Wialaya ya Kibaha Mkoa wa Pwani leo Februari 04, 2012
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akikagua jengo la Taasisi ya utafiti wa maradhi ya Malaria, baada ya kuzindua jengo hilo wakatiakiwa katika ziara yake ya Wilaya ya Bagamoyo mkoa wa Pwani jana Februari 03, 2012. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, February 04, 2012 | | Permalink | Maoni 0

gazeti lako makini la habari za michezo heka heka liko sokoni sasa kwa sh 400 tu.



 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, February 04, 2012 | | Permalink | Maoni 0

In new window Print all Kamati ya Tanzania Film Critics Association-TFCA

KAMATI YA WATU KUMI YA “TANZANIA FILM CRITICS ASSOCIATION”-TFCA

Tanzania Film Critics Association ni mradi ulio chini ya Image Profession wenye kuhusisha kundi la wanachama wa hiyari kwa malengo ya kuleta changamoto za kimaendeleo katika Tasnia ya Filamu ikiwa pamoja na  kuchambua,kukosoa,kushauri na kusaidia maswala mazima yahusuyo Filamu na wahusika wa Filamu hapa Tanzania.

Pamoja na kufanya shughuli zake kwa kutumia mitandao ya kijamii ,kundi pia litakuwa na shughuli zitakazofanyika katika mazingira mbali mbali ya kawaida ikiwa pamoja na kuwa na mabaraza yatakayohusisha wataalamu mbalimbali wa Tasnia ya Filamu.

Waliopendekezwa watakaoungana na wajumbe watatu kutoka Image Profession(IP)kuingia katika kamati ya watu kumi itakayosimamia na kuratibu utendaji wa Tanzania Film Critics Association,katika kipindi cha miezi sita mpaka mwaka.

Wafuatao ni wajumbe  saba  na idadi ya mapendekezo waliyoyapata kutoka katika mchakato wa kupendekeza uliofanyika kwenye kundi hili kwenye mtandao wa kijamii wa Facebook.
1.   John Kitime                                      (47)
2.   Goddy Semwaiko                     (37)
3.   Bishop Hiluka                         (36)
4.   Apilike Gordon                        (33)
5.   Rashid Faraji                           (31)
6.   Rashid Adam                           (25)
7.   Richard Mloka                         (24)

Mkutano wa kwanza wa wajumbe wakamati utakuwa siku ya Jumamosi ya Tarehe 11.02.2012 ,tunatoa shukrani kwa kila mmoja aliyeshiriki katika mchakato mzima wa kundi na wale wote wanaochukuwa muda wao kutoa mada mbalimbali kuchangia na hata kusoma yale yanayoandikwa kwenye kundi..
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, February 04, 2012 | | Permalink | Maoni 0

MAFUNDI WACHAKARIKA KUSHONA SARE 400 ZA VIJANA WA GWARIDE MAALUM KITAFA LA MIAKA 35 YA CCM

Friday, February 3, 2012
MAFUNDI 20 waliopewa kazi wa kushona sare zitakazovalishwa na Vijana wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) wakati wa gwaride maalum siku ya kilele ya miaka 35 ya CCM wakiwa kazini jana kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza ambako sherehe za maadhimimisho hayo kitaifa zitafanyika Jumapili hii. Jumla ya vijana 400 kutoka wilaya zote za mkoa wa Mwanza watashiriki gwaride hilo.
Uwanja wa CCM Kirumba zitakakofanyika kitaifa sherehe za kilele cha maadhimisho ya miaka 35 ya CCM, Jumapili hii, Februari 5, 2012, ukiwa umepambwa maneno ya kumkaribisha Mwenyekiti wa Chama, Rais Jakaya Kikwete ambaye atakuwa mgeni rasmi kwenye sherehe hizo.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Friday, February 03, 2012 | | Permalink | Maoni 0

baada ya ukimya wa miaka 7,mr nice aibuka na single yake mpya.

 

Sikiliza kwa makini wimbo mpya wa Mr Nice uitwao Tabia gani.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Friday, February 03, 2012 | | Permalink | Maoni 2

rais kikwete ahudhuria hafla ya siku ya Sheria jijini dar leo.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiuhutubia katika Siku ya Sheria Tanzania jijini Dar es salaam leo January 3, 2012
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiangalia kalenda aliyozawadiwa na Jaji Mkuu Mh. Mohamed Chande Othman baada ya kuhutubia katika Siku ya Sheria Tanzania  jijini Dar es salaam leo January 3, 2012.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwasili katika viwanja vya Mahakama kuu jijini Dar es salaam leo January 3, 2012 na kupokewa na Jaji Mkuu Mh. Mohamed Chande Othman nyuma yake, Spika Anne Makinda (anayepeana nae mikono, na viongozi wa juu wa Mahakama kabla ya kuhutubia katika Siku ya Sheria  Tanzania jijini Dar es salaam leo January 3, 2012.PICHA NA IKULU.

============  ======== ========= 

SALAMU ZA MHE. JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, KWENYE SIKU YA SHERIA TAREHE 03 FEBRUARI, 2012
 
Mheshimiwa Jaji Mkuu;
Mheshimiwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;

Mheshimiwa Jaji Mkuu wa Zanzibar;
Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria;
Mheshimiwa Jaji Kiongozi na Majaji wa Mahakama Kuu;
Mheshimiwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali;
Rais wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika;
Mahakimu na Watumishi Wengine wa Mahakama;
Wageni Waalikwa; Mabibi na Mabwana:

Nakushukuru sana Mheshimiwa Jaji Mkuu kwa kunialika kuja
kujumuika nanyi katika siku hii adhimu ya kuadhimisha Siku ya Sheria kwa mwaka 2012. Nakushuru pia kwa kunipa nafasi ya kutoa salamu kwa hadhara hii ya mabingwa wa sheria na watoaji haki. 

Lazima nikiri kuwa baada ya kusikiliza nasaha maridhawa zilizotolewa katika hotuba yako nzuri na nyinginezo za walionitangulia mimi sintokuwa na mengi ya kusema. Hakika tumepata darasa la kutosha. Hivyo, nitasema
machache.

Niruhusuni nianze kwa kutakiana heri ya Mwaka Mpya.
Naungana na viongozi wa dini waliotuombea dua hapa leo hii
kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuumaliza mwaka uliopita salama na tunamuomba atujaalie neema na baraka tele mwaka huu wa 2012.

Tumuombe atujaalie ndoto zetu zitimie na tunayopanga yafanikiwe. Mheshimiwa Jaji Mkuu;

Nakupongeza sana wewe binafsi kwa kazi yako nzuri uifanyayo ya kusimamia na kuuongoza mhimili wa Mahakama. Wahenga walisema ‘nyota njema huonekana asubuhi’. Katika kipindi kifupi ulichokuwa
Jaji Mkuu umeonyesha kuwa wewe ni kiongozi mahiri na mtetezi

shupavu wa maslahi ya mhimili wa Mahakama na haki za raia. Aidha,umekuwa daraja imara kati ya mihimili yetu mitatu ya dola yaani Serikali, Bunge na Mahakama. Kupitia kwako, mafanikio mengi yamepatikana na heshima na taswira ya Mahakama katika jamii inazidi kuboreka. Nakushukuru sana.
Nawapongeza, pia, Majaji wa Rufaa, Majaji wa Mahakama Kuu, Mahakimu pamoja na watumishi wengine wote wa Mahakama. 

Kwa kweli wamefanya kazi kubwa na nzuri pamoja na kuwepo changamoto mbalimbali. Mimi na wenzangu Serikalini pamoja na wananchi walio wengi tunatambua na kuthamini mchango wenu muhimu katika utoaji wa haki.

Jitihada zenu ndizo zimewezesha Mahakama kupata
mafanikio ambayo tunayazungumzia leo. Mimi naamini kuwa
mwelekeo wetu wa siku za usoni unaleta matumaini makubwa.

Ujumbe wa Mwaka
Mheshimiwa Jaji Mkuu;

Nawapongeza sana kwa mada nzuri ya maadhimisho ya Siku
ya Sheria mwaka huu inayosema “Adhabu Mbadala Katika Kesi za Jinai na Faida zake katika jamii”. Kwa hakika huu ni ujumbe ambao umekuja wakati muafaka kabisa.
Jambo hili ni muhimu sana. 

Read more »
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Friday, February 03, 2012 | | Permalink | Maoni 1

kumekucha mambo ya malavi davi,kaa mkao wa kula.

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Friday, February 03, 2012 | | Permalink | Maoni 0

rais kikwete akutana na viongozi wa NGO ikulu jijini dar leo.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipokea mapendekezo ya Baraza la Taifa la NGOs Ikulu jijini Dar es salaam leo January 3, 2012 kuzungumzia mchakato wa Katiba.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikutana na viongozi wa Baraza la Taifa la NGOs Ikulu jijini Dar es salaam leo January 3, 2012 kuzungumzia mchakato wa Katiba. Picha na IKULU.

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Friday, February 03, 2012 | | Permalink | Maoni 1
Idadi ya watu