Dar es Salaam July 6, 2009:
Kampuni ya simu za mkononi, Vodacom Tanzania, haijapandisha bei za vocha za muda wa maongezi kwa wateja wa jumla na hivyo bei sokoni haitakiwi kupanda.
Akizungumza Jijini mchana huu, Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano cha Vodacom Tanzania, Mwamvita Makamba alisema kilichotokea ni kwamba Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imebadilisha mfumo wa wa ukusanyaji wa kodi ya ongezeko la thamani (VAT) ambao umesababisha badiliko dogo katika gharama za usambazaji kwa wateja wa jumla.
Alisema mabadiliko hayo ya mfumo wa ukusanyaji wa kodi hayatakiwi kuleta mabadiliko katika bei ya uuzajiwa vocha sokoni.
Mwanvita alitoa ufafanuzi huo kufuatia hatua ya baadhi ya wauzaji wa rejareja wa vocha za muda wa maongezi kupandisha bei ya vocha hizo kwa kati ya shilingi 100 na 200, mathalani vocha ya Sh,1000 inauzwa kwa bei ya shilingi 1200, Sh.2000 inauzwa kwa Sh.2200. Sh.5000, inauzwa kwa Sh.5200 au zaidi.
“Kubadilika kwa mfumo wa ukusanyaji wa kodi ya ongezeko la thamani hakupaswi kubadilisha bei kwa wauzaji wa rejareja, natoa wito kwa wauzaji hao kuacha kupandisha bei ya vocha hizo kwani mabadiliko madogo ya kodi yaliyofanywa hayana madhara kwao,” alisema.
Mwanvita.
Alifafanua kwamba Vodacom hivi sasa inakutakana na wauzaji wa jumla wa vocha ili kuhakikisha kwamba bei za vocha zinabaki na thamani kama zinavyotakiwa sokoni, yaani vocha ya 1,000 inauzwa kwa 1,000 na si vinginevyo.
Baadhi ya wateja wa Vodacom wamekuwa wakilalamika kufuatia kupanda huko kwa bei kwa madai kwamba hakuna tangazo lolote la Vodacom lilowataarifu mabadiliko hayo ya bei na kwamba kupanda huko kunawaumiza.
Vodacom Tanzania ndiyo mtandao unaoongoza hapa Tanzania ukiwa na wateja zaidi ya milioni 6 na ukiwa umesambaa nchini nzima.
Imetolewa na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano
Mwamvita Makamba
Kwa niaba ya Vodacom Tan