MWAKA WA WASOMI MISS UTALII TANZANIA 2009/2010

Saturday, November 7, 2009

Katika kile kinachoonekana kukubalika zaidi kwa wasomi zaidi, kiu ya Wasomi kujitoa Muhanga kwa kuutangaza Utalii na Utamaduni wa Mtanzania, wasomi wengi mwaka huu wamemejitokeza kushiriki katika mashindano ya Miss Utalii Tanzania, na kutwa mataji karibu yote katika ngazi mbalimbali za mikoa,Wilaya, na Kanda ambazo tayari zimekwisha fanya mashindano yake mwaka huu.



kama ilivyokuwa katika shindano la Miss Utalii temeke 2009, ambapo mrembo mwenye Digrii ya Uhasibu na Utawala wa Fedha Erica Allan, alipotwaa taji la Miss Utalii Temeke 2009/2010, jana Msomi mwingine mwenye shahada ya Sayansi ya Komputa, Shaymaa Ntetema aliweza kutwaa taji la miss Utalii Ilala 2009/2010 katika fainal iliyofanyika katika ukumbi wa Da' West Park Inn Tabata, Dar es Salaam.



Huku mwanafunzi wa Digrii ya Sayansi ya Jamii katika chuo Kikuu Shiriki cha Sayansi ya Jamii (Ustawi wa Jamii) Kijitonyama , Aghata Kilala aliweza kutwaa nafasi ya Pili akifutiwa na Sheila Bahamary , Mwanafunzi wa Shahada ya Juu ya Uhandishi wa Habari katika chuo cha DSJ. nafasi ya nne ilitwaliwa na Tausi Thomasi mwenye Elimu ya Kitato cha Sita huku nafasi ya tano na taji la kipaji likitwaliwa na Mwanafunzi wa Kozi za awali za Komputa, Jamida Abdu.ambapo katika shindano hilo warembo wote walipita kwa mavazi mbalimbali likiwemo la Asili ambalo pia walilitumia kama ngao ya Asili kwa kuchezea ngoma ya tamaduni za makabila ya Tanzania.



Aidha warembo waliweza kujibu maswali mbalimbali yanayohusiana na Utalii, Mila na Desturi, Vivutio vya Utalii na Hifadhi za Taifa za Utalii, Mikoa na Tamaduni mbalimbali, ikiwemo kuimba nyimbo za Tanzania. washiriki wengine walioingia katika kinyang'anyiro hicho ni pamoja na Tickey Lithon, Frola Nicholuas, Janneth Samson, Edna Endrew, Nezia Mangaka, ambapo shindano hilo lilipambwa na wanamuziki wengi wakiwapo bendi ya Extra Bongo chini yake ally Choki, Zia Musiki, Kundi la Muziki la Ngoma za Asili, Mfalme Bendi chini yake Costar Siboka, pamoja na wanamuziki wa Kizazi Kipya, Abubakary Msasu(Kiboot) ambaye hata hivyo alichelewa kuingia Ukumbini.



kwa mujibu wa Waandaaji wa mashindano hayo, sasa shindano ambalo linatazamiwa kufana kwa aina yake ni shindano la Miss Utalii Kinondoni, ambalo limesheheni wasomi wengi kutoka Vyuo Vikuu mbalimbali ikiwemo, chiuo Kikuu cha Dar es Salaam, Mzumbe, IFM, CBE, na Vingine Vingi Mgeni Rasmi katika Shindano hilo alikuwa Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mwantumu Mohamed, huku wadhamini wa shindano hilo Kampuni ya Mlonge by Makai Enterprises wakiweza kukabidhi zawadi kwa washindi zilizokabidhiwa na Afisa Utamaduni wilaya ya Ilala Shani Mohamed.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, November 07, 2009 | | Permalink | Maoni 0

HISTORIA FUPI YA MAREHEMU ALEX MUKAMA KUSSAGA




Kuzaliwa; Marehemu alizaliwa Julai 7, 1932 katika kijiji cha Bwasi Majita Musoma vijijini.

Masomo;


= Elimu ya Msingi alisoma Bukima Primary school kuanzia mwaka 1942 ambapo alihitimu darasa la nne. Mwaka 1946 alijiunga na Shule ya Mwisenge Middle school ambapo alisoma darasa la tano hadi la nane.



= Mwaka 1951 alijiunga na Chuo cha Ualimu Pasiansi Mwanza na kufuzu cheti cha Ualimu mwaka 1952.



= Mwishoni mwa mwaka 1952 baada ya kuhitimu cheti cha Ualimu alibakizwa hapo chuoni kama mkufunzi. Aliendelea kufundisha Pasiansi Teacher Training Centre hadi chuo kilipohamishiwa Butimba Teacher Training Centre-Mwanza. Alijiuzulu kazi ya ualimu mwaka 1959 na kujiunga na vyama vya Ushirika Ukerewe Growers Corperative Union.



= Mwaka 1961 aliacha kazi ya Ushirika na kuingia Serikali kuu ambapo alipelekwa Mzumbe Institute of administration kusomea utawala. Baada ya kumaliza masomo Mzumbe 1962 aliteuliwa kuwa Local Government Officer kule Njombe District-Southern Highlands Province wakati huo.



= Kwa juhudi na bidii aliyokuwa nayo kazini, mwaka 1964 alipandishwa cheo kuwa Regional Local Government Officer-Southern Highlands Province-Mbeya.

= Mwaka 1965 alihamishiwa Musoma na kuteuliwa kuwa Town Clerk wa mji wa Musoma.


= Mwaka 1967 alihamishiwa mjini Iringa kama Town Clerk, mji ambao ulikuwa mkubwa kuliko Musoma.



= Mwaka 1968 alipandishwa cheo na kuhamishiwa Mwanza kama Town Clerk ambako alifanya kazi hadi mwanzoni mwa mwaka 1973 ambapo alihamishiwa Mtwara Township.



= Akiwa Mtwara, marehemu alijiuzulu kazi za Serikali na kujiunga na Shirika la Bima la Taifa kama Meneja Utawala mwaka 1973 april. Akiwa Meneja utawala Bima, mwaka 1976 alikwenda Uingereza kuchukua mafunzo ya Utawala katika Chuo kikuu cha Manchester.Aliendelea kufanya kazi Bima na kupandishwa cheo kufikia ngazi ya Mkurugenzi wa Utawala Shirika la Bima hadi alipostaafu 1991.



Mzee Alex alishiriki katika uundwaji wa kampuni kubwa ya Media inayoitwa Clouds Entertainment. Kampuni hii ikihodhi baadhi ya makampuni yafuatayo; Clouds fm/choice fm/clouds tv ambapo mpaka kutokea kifo chake yeye akiwa ndiye Mwenyekiti.

Marehemu ameacha mke na watoto tisa, pamoja na wajukuu 11.

Mungu alitoa na Mungu ametwaa, jina la Bwana lihimidiwe
, Amen.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, November 07, 2009 | | Permalink | Maoni 0

hatimaye mzee alex mukama kusaga apumzishwa kwenye nyumba yake ya milele

Mtoto wa marehemu Mzee Alex Kusaga,Justine akisoma wasifu wa baba yake mchana huu mara baada ya mazishi kufanyika katika makaburi ya kinondoni jijini Dar
Mwenyekiti mtendaji wa Makampuni ya IPP na mwenyekiti wa wamiliki wa vyombo vya habari (MOAT) Bw. Reginard Mengi akiweka shada la maua kwenye kaburi la Mzee Kusaga kwa niaba ya vyombo vya habari.

Waziri Mkuu Mstaafu Jaji Joseph Warioba akiweka shada la maua katika kaburi.


Mjukuu wa marehemu,Alex akienda kuweka shada la maua kwenye kaburi la babu yake
Mtoto wa marehemu Mzee Alex Kusaga (jina lake limenitoka msaada tutani) akiweka shada la maua
Familia ya maremeu Alex Kusaga ikiweka mashada ya maua
Mtoto wa marehemu mzee Alex kusaga na Mkurugenzi wa Clouds Media Group,Joseph Kusaga na mkewe Juhyna Kusaga pamoja na mtoto wao wa kwanza Natalia, wakiweka shada la maua kwenye kaburi la mzazi wao mpendwa,Mzee Alex Kusaga ambaye alifariki hivi karibuni Pretoria,nchini Afrika ya Kusini alikokuwa akitibiwa ugonjwa wa Kansa.

Mke wa marehemu akiweka shada la mau kwenye kaburi la mpendwa wake leo mchana.
Meneja masoko wa kampuni ya simu ya mikononi ya TIGO,Bw.Massanja kwa niamba ya kampuni yake akiweka shada la maua kwenye kaburi la mzee Kusaga mchana huu
Mkurugenzi wa utafiti Clouds Media Group Ruge Mutahaba kwa niaba ya kampuni akiweka shada la maua.

Hapa ndipo alipopumzika Mzee Alex Mkama Kusaga kwa amani mchana wa leo katika makaburi ya kinondoni jijini Dar.Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi -AMEN

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, November 07, 2009 | | Permalink | Maoni 0

mazishi ya mzee alex kusaga mchana huu

Mkurugenzi wa utafiti Clouds Media Groug Ruge Mutahaba kwa niaba ya Clouds akiweka mchanga kwenye kaburi la marehemu Mzee Alex Kusaga mchana huu.
Mke wa marehemu Mzee Alex Kusaga akiweka mchanga

Mtoto wa Marehemu mzee Alex Kusaga,Justine kusaga akiweka mchanga kwenye kaburi la baba yake,mchana huu kwenye mazishi yaliyofanyika katika makaburi ya kinondoni jijini Dar


Mkurugenzi wa Clouds Media Group/Prime Time Promotions Joseph Kusaga akiwa ameambatana mkewe Johyana Kusaga wakiweka mchanga kwenye kaburi la baba yake.

Mungu ailaze roho ya Baba yetu,Babu yetu,ndugu yetu mpendwa Mzee Alex Kusaga mahali pema peponi-AMEN.
Mzee Alex Kusaga anakwenda kupumzishwa kwenye nyumba yake ya milele mchana huu.
Mwili wa marehemu Mzee Alex Kusaga ukipelekwa kwenye nyumba yake ya milele mara baada ya kuombewa mchana huu katika makaburi ya kinondoni jijini Dar
Baadhi ya wafanyakazi wa Clouds Media Group wakiwa wamebeba mashada kwa ajili ya kuweka kwenye nyumba ya milele ya Mzee K mchana huu.

Mwimbaji chipukizi mahiri kabisa katika anga ya muziki wa kiroho,Jesca akiimba kwa hisia mbele ya umati wa watu uliofika kwenye mazishi ya marehemu, Mzee Alex Kusaga leo mchana



Ndugu jamaaa na marafiki wakiwemo wafanyakazi wa Clouds Media Group wakiwa wamejikalia/kusanyika chini ya mti kabala ya mazishi kufanyika leo mchana kwenye makaburi ya Kinondoni jijini Dar


Sehemu ya familia ya marehemu,Mzee Alex Kusaga wakiwa wamekaa kwa pamoja katika hali ya majonzi leo mchana kwenye makaburi ya Kinondoni jijini Dar,kabla ya mazishi kufanyika


Sehemu ya familia ya marehemu,Mzee Alex Kusaga wakiwa wamekaa kwa pamoja katika hali ya majonzi leo mchana kwenye makaburi ya Kinondoni jijini Dar,kabla ya mazishi kufanyika



Baadhi ya ndugu,jamaa na marafiki wakiwa wamesimama kwa heshima wakati sala ya kumuombea marehemu ikisomwa.
Mwili wa marehemu ukishushwa na kuwekwa mahali kwa muda kwa ajili ya kupata sala ya pamoja kabla ya kumpeleka kwenye nyumba yake ya milele leo mchana.
Mke wa marehemu Mzee Alex Kusaga akishuka kwenye gari iliobeba mwili wa mumewe,leo jioni wakati ukiwasili katika makaburi ya kinondoni jijini dar kwa ajili ya mazishi.

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, November 07, 2009 | | Permalink | Maoni 0

marehemu mzee alex kusaga alivyoagwa kanisani

Mwili wa marehemu ukiingizwa kwenye gari tayari kuelekea makaburini kinondoni jijini Dar kwa mazishi leo mchana.
Mke wa marehu akitoka kanisani
Akina mama na maua yao ya upendo kwa marehemu

Mwili wa marehemu Alex Kusaga ukitolewa kanisani kwa ajili ya kwenda kuzikwa katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar
Mkurugenzi wa Clouds Media Gropu/Prime Time Promotions Joseph Kusaga pamoja na familia yake akitoa heshima za mwisho kwa baba yake mzee Alex Kusaga mchana huu katika kanisa la Azania Front,jijini Dar
Rais mstaafu wa awamu ya tatu ,Mh Benjamin Mkapa akitoa heshima za mwisho mbele ya mwili wa marehemu mzee Alex Kusaga mchana huu katika kanisa la Azania Front,jijini Dar.
Mama Anna Mkapa akitoa heshima za mwisho mbele ya mwili wa marehemu Mzee Alex Kusaga
Mke wa marehemu akitoa heshima za mwisho mchana huu ndani ya kanisa la Azania Front
watoto wa marehemu mzee Alex Kusaga wakitoa heshima za mwisho mchana huu kanisani
wakati wa sala,kulia ni Rais mstaafu wa awamu ya tatu,Mh William Benjamini Mkapa na mkewe Mama Anna MKapa
Rais mstaafu wa awamu ya tatu,Mh William Benjamini Mkapa na mkewe Mama Anna MKapa na Mke wa Marehemu wakisoma kitabu cha sala
Kanisa la Azania Front linavyoonekana kwa ndani huku sala ikiendelea
Familia ya marehemu,Mzeee Alex Kusaga wakiwa katika majonzi baada ya kuondokewa mpendwa wao,pichani wakisikiliza kwa makini sala iliyokuwa ikiendeshwa kwa ajili ya kumuombea marehu.

Ngugu wa marehemu Mzee Alex Kusaga wakiwa kanisani le mchana

Baadhi ya ndugu jamaa na marafiki wakiwa wametulia kwa makini wakifuatilia sala iliyokuwa ikiendeshwa kwa ajili ya kumuombea marehemu,Mzee Alex Kusaga.
Ndugu,jamaa na marafiki walifika kwa wingi kanisani kwa ajili kutoa heshima zao za mwisho kwa mpendwa wao Marehemu Alex Kusaga.
Baadhi ya wafanyakazi wa Clouds Fm/Tv wakiwa wametulia tulii wakifuatilia yaliyokuwa yanajiri ndani ya kanisa leo mchana.
Akina mama wakiwa katika nyuso za huzuni leo mchana nje ya kanisa la Azania Front baada ya kuondokewa mpendwa wao Mzee Alex Kusaga.
Mwili wa marehemu ukiwekwa kwa makini
Mwili wa marehemu Mzee Alex Kusaga ukiwasili kanisani leo mchana katika kanisa la Azania Fron,jijini Dar na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa watu.

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, November 07, 2009 | | Permalink | Maoni 3

Marehemu Alex kusaga alivyoagwa nyumbani kwake leo

Safani ya kuelekea kanisani kwa ajili ya kumuombea marehemu Alex Kusaga katika kanisa la Azania Front leo mchana
Akina mama nao wakielekea kwenye magari tayari kuelekea kanisani
Safari ya kanisani inaanza

Mwili wa marehemu Alex Kusaga tayari umewekwa ndani ya gari tayari kuelekea kanisani

Kamati ya msiba ambayo ni sehemu ya familia wakijipanga vyema namna ya kuweka utaratibu mzima wa usafiri kwa wageni mbalimbali kwa ajili ya kuelekea kanisani.
Mkurugenzi wa Clouds Media Group/Prime Time Promotions, Joseph Kusaga na ndugu wengine kwa ujumla akihakikisha kila kitu kinakwenda sawa hapo nyumbani
Sehemu wa familia ya Kusaga wakijiandaa kuondoka kuelekea kanisani mara baada ya kuuaga mwili

Ndugu wa karibu wa marehemu walibeba maua ya mpendwa wao,ambaye ka hakika ameacha pengo kubwa kwa familia na hata marafiki na watu wengine,ama hakika kazi ya mungu haina makosa.
Mwili wa marehemu ukiingizwa kwenye gari tayari kuelekea kanisani
mwili wa marehemu Alex Kusaga ukitolewa kwenye nyumba yake ya muda na kupelekwa kanisani na kisha kwenye nyumba yake ya milele
Mwili wa marehemu Alex Kusaga ukitolewa nje kwa ajili ya kupelekwa kanisani
Mke wa marehemu Alex Kusaga akimuaga mumewe kwa mara ya mwisho kabla ya mwili kupelekwa kanisani na kisha kwenye nyumba yake ya milele.
Mkurugenzi wa Clouds Media Group/Prime Time Promotions, Joseph Kusaga akitoa heshima za mwisho kwa baba yake
Mtoto wa Marehemu Alex Kusaga,Dada Sheba akitoa heshima zake za mwisho kwa baba yake mapema leo asubuhi
Ndugu wa karibu wa Marehemu mzee Alex Kusaga akilia kwa uchuku mara baada ya kumuaga kwa mara ya mwisho
Ndugu wa karibu na familia ya mzee Alex Kusaga wakimuaga
Mtangazaji wa Clouds Fm Ephrahim Kibonde akijaribu kuwaka sawa ratiba nzima ya kuanza kuuaga mwili wa marehemu mapema leo asubuhi nyumbani kwake marehemu.
Wageni,Ndugu na jamaa walifika mapema leo asubuhi kuuaga mwili wa marehemu Alex Kusaga nyumbani kwake.


Leo ndiyo ikuwa siku ya kuuaga mwili wa Mwenyekiti Mendaji wa kampuni ya Clouds Media Group,Marehemu Alex Mkama Kusaga,ambaye ameagwa leo asubuhi nyumbani kwake Mbezi Beach.Fuatilia mpangilio wa picha katika matukio mbalimbali yalikuwa yakijiri.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, November 07, 2009 | | Permalink | Maoni 2

kwa hali hii wasanii wetu wa filamu watafika kweli?

Friday, November 6, 2009


Pichani ni sehemu ndogo tu ya Cd feki zinazosambaa mitaani na kuuzwa,zenye filam kumi kwa moja amboa nyingi zimekamatwa Arusha,Mwanza na Dar es Salaam. Vile vile zimetapakaa mpaka Congo na Nchi jirani.Je? Wasanii tutafanikiwa kwa hali hii?Watanzani wenzangu kazi tunazofanya ni ngumu sana lakini wanaofaidika ni watu ambao hawatumii nguvu kubwa.Ombi letu kwa Watanzania wote mlio nje ya nchi na ndani ya nchi msinunue kazi zenye mfano wa makava haya.
Wanajamvini imefika mahali jamani tuwaonee huruma wasanii wetu wa filamu hapa bongo, kusema ukweli wamekuwa wakilalamika kila kukicha kuhusiana na uharamia wa kazi zao unaozidi kukithiri kila kukicha,wanawekeza muda wao mwingi,fedha zao na mambo chungu mzima lakini wanaokuja kufaidika ni mtu/watu baki kabisa ambaye kimsingi hakupaswa kufaidika,Jamii inatupasa kumka sasa kupambana na hii vita ingawa ni ngumu lakini angalau basi tuoneshe moyo wa kuwasaidia kwa namna moja ama nyingine,Vingnevyo wasanii wetu watakuwa masikini kila siku huku tukiwacheka na kuwauliza kwa nini hawaendelei,wakati majibu ya tatioz tunayo
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Friday, November 06, 2009 | | Permalink | Maoni 1

Hili ni Posta ya ujio wa album mpya ya mangwea inayoitwa NG'E 1982,


 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Friday, November 06, 2009 | | Permalink | Maoni 0

Kombe la Ligi Kuu Uingereza kushuhudiwa live dar,limetua leo

Mkurugenzi mtendaji wa Benki ya Barclays nchini Bw. Rashed Bade kulia na mwenyekiti wa Baraza la Michezo nchini BMT Kanali Idd Kipingu wakifunua kitambaa ili kuonesha kombe la Ligi kuu ya Uingereza (English Barcklays Premier Ligue Cup) mbele ya waandishi wa habari kwenye Hoteli ya New Africa jijini leo, kombe hilo litakimbizwa maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es salaam kwa siku mbili mfurulizo ili kuwapa fursa mashabiki mbalimbali wa timu za Uingereza waliopo nchini kuliona.
Mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Taifa(BMT)Kanali Mstaafu.Iddi Kipingu(kushoto) na Mmoja wa Walinzi wa Kombe la Ligi Kuu ya Uingereza,Keith Russel wakiwa wameshikilia kombe hilo baada ya kuwasili Uwanja wa ndege wa kimataifa wa mwalimu Julius Nyerere,mapema leo asubuhi kwa ziara maalum ya kuhamasisha michezo nchini..
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Friday, November 06, 2009 | | Permalink | Maoni 1

TAARIFA YA MWENYEKITI MTENDAJI WA IPP LTD.BW.REGINALD A.MENGI KWA VYOMBO VYA HABARI


Ndugu Waandishi wa habari,
Nimewaita hapa leo kuzungumza nanyi kwa lengo la kuweka rekodi sawa.
Kwa muda mrefu sasa nimekuwa nikituhumiwa na baadhi ya viongozi wa Chama Cha Mapinduzi(CCM)kwamba mimi si Mwanachama wa Chama hicho na kwamba sitoi misaada ya hali na mali kwa Chama Cha Mapinduzi.
Ndugu Wanahabari,
Kwa msemo wa kiingereza“Don’t argue with a fool because people may not know the difference between you and the fool”,wenye maana kwamba usibishane na mjinga kwa sababu watu wanaweza kushindwa kufahamu tofauti yako na huyo mjinga!
Hata hivyo wakati mwingine inakulazimu kujibu hoja unapomwona mtu anapotosha mambo kwa makusudi.
Kwanza,kuhusu kuropoka kwamba sitoi misaada kwa CCM, hilo ni jambo linalozushwa na watu binafsi na kwa malengo binafsi.Viongozi wakuu wa CCM ambao ni waadilifu na wanaosimamia ukweli wanajua undani wa jambo hili.
Pili,kuhusu uwanachama wangu wa CCM:
Napenda kuwaambia kwamba mimi ni Mwanachama wa CCM tangu tarehe 18 Aprili,1977 na kadi yangu ni Na.B124595, iliyotolewa na Tawi la Kisutu,Wilaya ya Ilala,Mkoa wa Dar es Salaam.
Hivyo basi madai yote kwamba mimi si mwanachama au nilijiunga na chama hivi majuzi kama inavyoelezwa na Mheshimiwa Waziri wa Utawala Bora Sophia Simba,Katibu wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam,Shaaban Kilumbe Ng’enda na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa DSM John Guninita ni uongo,uzushi na umbea wenye lengo la kudhoofisha juhudi za viongozi wa juu wa CCM na baadhi ya wanachama za kupiga ufisadi vita.
Mimi na wenzangu wengine tumekuwa mstari wa mbele kuhakikisha kwamba chama chetu kinaongozwa katika misingi yake ya asili ya kupiga vita rushwa na maovu mengine.Ndugu Wanahabari,Hawa wanaodai kuwa ndani ya CCM hakuna kiongozi msafi ni wazi kwamba wamedandia chama hiki hivi majuzi.
Ningetoa ushauri kuwa waondoke na watuachie chama chetu kwa kuwa hawafahamu msingi imara wa CCM.Mwisho napenda kumshauri Waziri Sophia Simba kwamba katika vita dhidi ya ufisadi ni vyema akanyamaza.Kwa sababu yeye si mwadilifu na hivyo hawezi kusimama kupinga vita ya ufisadi.
Aidha,ningemshauri kabla hajazungumza aombe ushauri kutoka taasisi za serikali kama vile usalama wa taifa badala ya kuropoka na kupotosha ukweli wa mambo.
Nawashukuru sana kwa kunisikiliza.
Reginald A. Mengi
MWENYEKITI MTENDAJI,
IPP LTD
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Friday, November 06, 2009 | | Permalink | Maoni 2

ratiba ya kuaga mwili wamarehemu alex mkama kusaga


 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Friday, November 06, 2009 | | Permalink | Maoni 0

daima tutakukumbuka


 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Friday, November 06, 2009 | | Permalink | Maoni 1

je umepoteza mzigo wako wowote?

JUZI WAKATI NIPO KWENYE DALADALA KUNA MTU ALINIPA MZIGO WAKE NIMSHIKIE KWA SABABU YEYE ALIKOSA KITU KWENYE DALADALA.KWA BAHATI MBAYA ALIPOFIKA MWISHO WA SAFARI YAKE ALITEREMKA NA KUSAHAU MZIGO WAKO.NAOMBA UWEKE UJUMBE HUU KWENYE BLOG YAKO ILI MHUSIKA ATAKAPOUSOMA AWASILIANE NA MIMI.
ILI KUJUA KAMA NDIYE MWENYE MZIGO MASWALI YAFUATAYO ITABIDI AYAJIBU.
KWA MAWASILIANO 077-313-1164·
MFUKO UNA RANGI GANI?·
JUU YA MFUKO KUMEANDIKWA MANENO GANI?·
NDANI YA MFUKO KUNA KITU GANI?·
JE ALIPANDA DALADALA LA KUELEKEA WAPI?·
ALIPANDIA DALADA WAPI?·
ALISHUKA KITUO GANI?·
ALIKUWA NA NANI KATIKA SAFARI YAKE
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Friday, November 06, 2009 | | Permalink | Maoni 0

Viatu kutokana na mkate!





Thamani yake kati ya pauni €12 hadi 22! http://wavuti.com/shoes-made-out-of-bread.html

Subi
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Friday, November 06, 2009 | | Permalink | Maoni 2

ni webu ya mawasiliano like hi5,myspace,facebook


mimi ni mtanzania ninaishi moscow kimasomo....nina webu ya mawasiliano like hi5,myspace,facebook yaani mtandao wa kuwasiliana.N
Naomba uniwekee hewani watu waione http://www.kislat.com/.kislat(Keep Insight Love All Times) nimtandao unaowakutanisha watu wote popote walipo duniani.(kislat is a social network website which connect you with the rest of the world,upload photos,video,forums,create and join groups,create post and videos,meet old and new friends!!!).
.Shukrani sana,God Bless You.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Friday, November 06, 2009 | | Permalink | Maoni 0

anatafutwa mkalimani

TANGAZO TANGAZO
NATAFUTA MKALIMANI WA KUTAFSIRI KUTOKA KIPOLAND KWEDA KISWAHILI NA AWE ANAJUA KINGEREZA.
KWA MAELEZO ZAIDI TUMA EMAIL KUPITIA,nganzo88@yahoo.no
SIMU +4747262181 .
Wako JB PROMOTIONS&JB HIPHOP WEAR-
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Friday, November 06, 2009 | | Permalink | Maoni 0

wadau habari ndiyo hiyo.!

Habari yako bwana michuzi junior,
Ninafurahika sana kusoma jarida lako kila jioni ninapotoka kwenye shughuli nzito ya kujenga taifa.Picha nzuri na maelezo yaliyotulia zinanifanya nifurahie sana blogu yako.Ninaomba unisaidie kutangaza kibiashara changu kidogo hiki mimi ni softwea injinia hapa newyork ninawapa watu softwea ya bure ya ofisini mwaka 2007 lakini haina ufunguo.
Mtu akihitaji ufunguo awasiliane na mimi zamron.1000@gmail.com na nitamchaji dola 15 tu na malipo yote ni kupitia paypal account.Kama mtu hataridhika nayo nitamrudishia fedha yake yote.Huu ni mwanzo tu nitaleta softwea zingine kama matlab,viso,maple na kadhalika.Click hiyo linki hapo chini na watu wanaweza kuanza kudownloadi wakati wowote.Hii itasaidia watu walionunua kompyuta mpya au wasioweza kununua softwea mpya ya bei ghali,na pia inawasaidia kupunguza muda.
Yaliyomo humo ni word,excel,publisher,powerpoint,onenote,access na nyingine nyingi.Naomba pia unisaidie kusambaza huu ujumbe kwa michuzi mkubwa pia na ninaweza nikakusaidia commission kidogo kama mambo yakiwa mazuri.
Kalumanzila
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Friday, November 06, 2009 | | Permalink | Maoni 0

VODACOM MISS TANZANIA MIRIAM GERALD AKABIDHIWA uwakilishi wake rasmi


Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC) Emmanuel Ole Naiko akimkabidhi bendera ya Taifa Vodacom Miss Tanzania Miriam Gerald, mrembo huyo anatarajiwa kuiwakilisha nchi kwenye shindano la dunia litakalofanyika tarehe 12 mwezi Disemba mwaka huu katika mji wa Sanddown nchini Afrika Kusini na ataondoka kesho (leo) kuelekea nchini humo ili kujiunga katika kambi ya Miss World pamoja na warembo wengine wanaowakilisha nchi zao.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Friday, November 06, 2009 | | Permalink | Maoni 0

Ally Choki ,Mack Dee kupamba Miss Utalii Ilala 2009 leo


Kivumbi cha kumpata mrembo wa Fainali za Miss Utalii Ilala 2009 ni tarehe 6/11/2009 Ijumaa katika ukumbi wa Da’ West Park Inn Tabata, ambapo jumla ya Warembo 12 watapanda katika jukwaa kuchuana kuwania taji kwa musimu wa 2009/2010.



Katika shindano hilo ambalo macho na masikio kwa wakazi wa Dar es Salaam limewatia wazimu kutokana na kutoelewa nani hataibua nderemo, Vifijo, na makelele kutokana na warembo wote kuwa katika hali ya Ushindani mkali ambapo kila mrembo amejigamba kuibuka na taji hilo kasha kubeba vifaa mbalimbali ikiwa ni pamoja na fedha thamani yake ikiwa ni milioni mbili .



Warembo hao walioanza kambi kwa takribani mwezi mmoja katika Ukumbi wa Da’ West Park Inn-Tabata, waliweza kujifunza masuala mbalimbali yanayohusiana na Utalii unaopatikana Tanzania ikiwemo Hifadhi za Utalii za Taifa, Vivutio vya Kitalii, pamoja na Maajabu ya Dunia yanayopatikana hapa Tanzania. Aidha katika shindano hilo, warembo hao wataonyesha Mavazi ya asili ya makabila mbalimbali ya Tanzania, watacheza ngoma kuonyesha utamaduni wa Mtanzania, Watavaa mavazi ya Kitanzania ya Kitalii, vazi la Ubunifu lililotengenezwa kwa maligafi za hapa Tanzania, pamoja na mengine mengi yanayohusiana na masuala ya Utamaduni wa Mtanzania.



Warembo wanaowania taji la Miss Utalii Ilala 2009 ni pamoja na ,Tickey Lighton,Neema King’aka, Edna Endrew, Frola Nicholaus, Sheila Baamary, Janeth Samson, Nezia Gabriel, Roselina Sekwao, Jamida Abdu, Aghata Kilala, Tabus Thomas, na Shaymin Ntemena. Zawadi mbalimbali zenye thamani ya shilingi milioni kumi zitatolewa kwa washindi na washiriki, ikiwa ni pamoja na Fedha, na vifaa mbalimbali vyenye thamani mbalimbali, zitalolewa kwa washindi ambapo mshindi wa kwanza kwa mujibu wa Waandaji wa shindano hilo ni thamani ya shilingi milioni 2, mshindi wa pili thamani ya million moja na laki mbili ,mshindi wa tatu thamani ya laki nane na , mshindi wa nne na tano, thamani ya laki tano na mshindi wa Kipaji (Talent) ni thamani ya laki saba na nusu na kifuta jasho kwa wote ni shilingi elfu thelathini na watapatiwa vifaa mbalimbali vyenye thamani ya shilingi laki moja kila mmoja.


Miss Utalii Ilala katika Msimu huu ilipata bahati ya Kuungwa Mkono kwa asilimia mia moja na Mkurugenzi wa Chicken Hut Tanzania ltd ya Mlimani City, Savannah Lounge- Paradise City Hotel iliyopo katika jingo la Benjamini Mkapa Tower-Posta Mpya, Chaga Bite iliyopo Kijitonyama, Kampala International University iliyopo Gongolamboto, pamoja na Ukumbi wa Da’ West Park Inn- Tabata.



Wadhamini wengine waliojitokeza kuunga mkono ni wadau wa Shindano la Miss Utalii ikilinganishwa na miaka ya nyuma, ambapo baadhi ya watu mbalimbali wamejitokeza kusaidia ikiwa ni pamoja na Kampuni ya Ulinzi na Usafirishaji ya Aurora, Kampuni ya Usafirishaji ya Mamaa Sakinma Trans, Mashujaa Pub, Kampuni ya Uongozaji Watalii na Usafirishaji Watalii ya Aucland Tours & Safari, Hotel ya Kisasa ya Grand Villa Hotel iliyopo Kijitonyama, Gym Ya kisasa ya Fitness Centre ya Chang’ombe (Oil Com), Saloon ya Kisasa ya Dage Saloon iliyopo Sinza, Kampuni ya Vifaa vya Umeme ya Vam General Suplay, Kampuni inayojishughulisha na Mti wa Maajabu Ya Mlonge(Mlonge by Makai Enterprises) na Wabunge wa jiji la Dar es Salaam Burudani mbalimbali zitapatikana katika kupamba Onyesho hilo ikiwa ni pamoja na Kundin la Muziki la Extra Bongo chini ya Ally Choki, Zia Musica,kundi la ngoma za asili Mfalme Bendi chini ya Costa Siboka zamani Mr Ginnes, na makundi mbalimbali ya muziki wa ngoma za asili, mwanamuziki wa kizazi kipya mtanzania anayeishi nchini afrika kusini Abubakari Ally (Kiboot) ambapo wote mnakaribishwa Da’ West Park Inn Tabata.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Friday, November 06, 2009 | | Permalink | Maoni 1

kwa Wadau waTeknolojia

Wadau wote,
Sasa tunatengeneza software za computer kwa mahitaji yako utakavyo kama vile Hospital and Phamacy Management System, Payroll, Point of Sales Management System Including Stock system, Micro Finance(SACCOS) Management System, Schools Management System, software ya Internet cafe management,Dry Cleaner Management System, Bar stock and Management, .Tunatoa Huduma Tanzania nzimaFor more details contact: pcresourcesltd@gmail.com
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Friday, November 06, 2009 | | Permalink | Maoni 0

tamasha la fiesta one love lasogezwa mbele.

Thursday, November 5, 2009

Tamasha la Fiesta One Love 2009 lililotarajiwa kufanyika jumamosi hii,Novemba 7 katika uwanja wa posta,kijitonyama jijini Dar,limeaihirishwa na kusogezwa mbele.


Akizungumza mratibu mkuu wa tamasha hilo Bw.Ruge Mutahaba amesema kuwa tamasha hilo limeaihirishwa hadi Novemba 21,mabadiliko hayo yanatokana na wahusika wakuu wakiwemo wafanyakazi wa Clouds Media Group/Prime Time Promotions (ambao kwa kiasi kikubwa ndiyo waandaji wa tamasha hilo) kuondokewa (kufariki) kwa Mwenyekiti wao Mzee Alex Mkama Kusaga juzi jioni nchini Afrika ya Kusini alikopelekwa kwa ajili ya matibabu.


Mutahaba amesema ratiba ya wasanii wambao walipaswa kushiriki kwenye tamasha hilo la Kitaifa iko pale pale wala haijabadilika,na kwamba msanii ambaye alitajwa angewatumbuiza wakazi wa Dar kutoka chini Marekani kwenye tamasha hilo,Buster Rhymes na wenzake naye ratiba yake iko pale pale,kwamba atakamua vilivyo siku hiyo. .
Aidha kwa taarifa za msiba wa Mzee K. inaelezwa kuwa mwili wake utawasili leo jioni na msiba upo nyumbani kwake Mbezi Beach karibu na Girrafe Hotel,kuhusu ratiba za mazishi na mambo mengine tutaendelea kufahamishana zaidi.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, November 05, 2009 | | Permalink | Maoni 1

Tanzanight show


Habari?
Naomba kuwakumbusha kuhusu show ya Tanzanight hapa Finland.Show ya kwanza ipo kesho tarehe 6.11. @ Korjaamo, Helsinki na kesho kutwa 7.11. @ Klubi, Tampere.


Jukwaani wanapanda Sanaa Sana, Dudu Baya, Benjamin wa Mambo Jambo na Andrew Ashimba pamoja na wanamuziki toka Finland.Kwa maelezo zaidi tembelea viungo hivi
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, November 05, 2009 | | Permalink | Maoni 0

yousuo n'dour ,Angelique Kidjo kukamua jukwaa moja novemba 15 dar




Wasanii nyota wa muziki barani Afrika,Angelique Kidjo kutoka Benin na Yossou N'Dour wa Senegal, wanatarajia kufanya onesho lao moja jijini Dar litakalofanyika katika viwanja vya Karimjee,Novemba 15 mwaka huu.


Wasanii hao ambao watatua hapa bongo kwa mwaliko mkubwa wa kampuni ya simu ya Zain Tanzania,Meneja masoko wa kampuni hiyo Costantine Magavila alisema kuwa onesho hilo ni maalumu kwa wakazi wa Dar,pamoja na watumiaji wa mtandao wa Zain.Magavila alisema kuwa wasanii hao watakuwa jukwaani kuanzia saa moja usiku hadi saa sita usiku na wanatarajia kuwasili nchini Novemba 13 mwaka huu tayari kwa onesho hilo.


Magavila alibainisha kuwa onesho hilo litatoa nafasi kwa watumiaji wa huduma ya ZAP,kupata punguzo la bei kuwashuhudia wasanii hao ambapo watakaonunua tiketi kwa huduma hiyo watalipia sh 20,000/= badala ya sh. 25,000/= kama watu wa kawaida.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, November 05, 2009 | | Permalink | Maoni 0

uonevu india

Habari, pole na kazi muheshimiwa. naomba unitundikie duku duku langu hapo chini.thank you in advance
ALIENS, FAR AWAY FROM HOME
The incident which occurred in Mysore City, India, on 31st October 2009,leading to the arrest of 1 Kenyan and 9 Tanzanian students has raised a lot of concern among foreign students, in particular Africans here in Mysore and India at large. Most of what has been said in the media is not true nor is all of it untrue, the truth lies somewhere in between. All in all the damage has been done, that can not be changed. As far as the truth about exactly what happened that morning, it is yet to be determined by the Court of law.
In the meantime, we should realize that we have been stigmatized. Not by this particular incident only, but by many other incidences which have occurred prior, by the mistakes made by those who were here before us and even those who are in other foreign lands. Currently, once a mishap occurs concerning an African and an Indian, immediately, with no questions asked, it is presumed that the African is at fault.
It is true that some of us have broken the laws once or twice, but am sure there are more law abiders than law breakers among us but since Indians have it in their heads that an “African is bound to break the law,” we are the ones who have to suffer. And not only the ones at faults that suffer, but all of us have to face the consequences, something which is not fair at all. If we meet with an accident then it is concluded that the African was drunk or negligent, without a doubt.
Unfortunately one of us met with an accident few weeks back and a pedestrian died on the spot. The headings in the local newspapers read “a foreigner kills an Indian”. As if it was an intentional murder case or that this has never happened before involving Indians only. You forget that road accidents do happen, whether you are red or black or white or yellow.
Recently, one male and two female Tanzanians were beaten up by Indians in a restaurant just because the Indians who were there demanded to be served first before the “Negroes” who were there before those Indians, simply because it is “their India” and that they were the ones paying the taxes, hence it was their right.
Our friends were brutally injured and fortunately one of the Indians involved was in the same college as one the Tanzanian victims. To our astonishment, the lectures kept begging us to exclude this particular Indian from the case as it would bring a bad reputation to her and her family simply because it was a “she”.
They completely forgot the fact that another foreign student, from that same college, who had equal rights, had to be suspended them at the expense of an Indian girl who was worried more about her reputation. This particular incident was not seen in any of the newspapers despite the complaint being filled at the police nor did the principal make a big fuss out of it.
In the current event, because the accused were Africans, and because we are ever the lawbreakers and not the victims, the media had a field day with this one. We all know why this is so. The locals have been putting the blame on our cultural values, that once we are here we should adjust with the local customs. We are in the 21st century, due to globalization and improved infrastructure the world has become one big village and people from different parts of the world are crossing borders, coming together and interacting in various fields.
In such occasions cultural clashes are bound to happen so if it is cultural adjustments, then it should be a give and take policy, the locals need to adjust too. Locals should be aware that there are foreigners here too and an environment need to be created to make us feel comfortable since their Government made it possible for us to be here. If they did not want us here, they should not have granted us visas.
Not only that, but also because there are fellow Indians back in our home countries, and we have made it a point to make sure they are not harassed or discriminated in any way. We understand that “majority rule” prevails but just because we are the minority, we should not be forced to loose our individuality, put down our customs and values, forget about our practices and adopt yours just like that, it would be denial of our basic “right to freedom.” Law is a universal common knowledge and we are aware of it therefore we cant be defending any cultural practices which might be offensive to the indigenous people or which might lead to breaking the laws of this particular land. All we are asking is for the right to live with human dignity.
Until today, Indians still refer to us as “Negroes”, despite world wide rejection against the use of this particular term as it is regarded offensive. They are aware of the implications of the word and at times they just use it so as to annoy and provoke us and see how we would react. You might come across 6year olds calling out “Negro” with a big smile on their faces, just to see how you react. It is obvious that they are being taught but their elders, and this shows the level of ignorance and racism among most of them.
We often see in the newspapers and televisions Indian from different parts of the world protesting about racism against them. From Shilpa Shetty’s incident in England few years back to the recent protests in Australia. Are you aware of the racism happening in your own country? For a country practicing “untouchability”, you need not look so far to realize there is racism against your own kind, let alone racism against other nationalities. Incase you are not aware, there are many Indians back in our home country.
Most of whom have been given ample opportunities and have succeeded and prospered a lot. Crackers are not allowed in our country but with due respect to Indian culture, they are allowed to fire crackers on “Diwali!”, this shows the respect we have for your culture and how far we are willing to go to make sure that you people are comfortable in our country. Few months back, I was on a plane back home for the holidays. I was sitting next to an Indian woman carrying a 3months old baby girl. She addressed me in “Swahili”, asking me where I was from.
I told her I was a Tanzanian and she told me she was Kenyan and that she is so excited going back HOME to Kenya after giving birth to her beautiful baby girl in India. This was only her second time in India in 35 years since she was born in Kenya. I was not surprised by all this because back at home many of them even get angry when you refer to them as Indians, they want to be called Tanzanians, proudly, with full of joy on their faces and hearts. You should see the look on their faces once we tell them that we are going to India for studies.
They ask, “why India?” and we often wonder “could it be that bad?” Never have I heard of or read in the newspapers a racist act against an Indian back in our country. Last month I had entered in one of the bookstores here in Mysore, they do offer membership cards but unfortunately for me that day I was denied of one. When I asked the reason behind this, the clerk replied “we do not offer these cards to your kind.” I asked “when you say my kind, you mean foreigners?” He said “no, Africans!” God forbid, if this were how you are being treated back in our home countries.
To make matters even worse, our guardians on this foreign land, the Tanzanian High Commission in New Delhi, are not doing anything to make things any better. Unfortunately, I was not lucky enough to visit the High Commission nor did I have any personal matter which required an assistance from there, as of this I feel very fortunate. But the experience of those who have been there and those who have required assistance from our High Commission has not been very good, it has been disappointments only.
For the 4 years I have been here, I haven’t come across any Tanzanian who has spoken positively about our High Commission. It might sound odd, but it is the truth. I had to experience it first hand during these several months when I got the opportunity to be the Chairperson of Tanzanian Students Association in Mysore.
To mention a few incidences : a Tanzanian had met with an accident and injured a middle aged Indian woman. The Indian family demanded a big sum of money as compensation. It was obvious that the exorbitant amount of money was demanded simply because the driver was a Tanzanian, a “Negro.” The driver and the parents back at home tried to seek assistance from the Embassy but nothing has been done till today. It has been more than 2 years now, after extorting a lot from us, the case had to be taken to the court of law where it is still going on to date. No assistance has been granted from there.
Another student had problems with his Visa and needed to go back home, he was stranded here for 1 whole year but the High Commission responded as it always does “ we can not help you on that.” So he had to seek assistance from the Indian High Commission in Dar es salaam, and that is when he was able to leave. The other Tanzanian who had met with an accident and a pedestrian died on the spot.
He was later arrested and convicted. The Commission was asked for assistance but it did not provide any, it responded with “what was he doing on the road at that time!” We engaged a lawyer and posted bail on our own without a helping hand from the Commissioner. The three Tanzanians who were beaten up by Indians in a restaurant, after the complaint being filled, we expected the Commission to put pressure and fight for the rights of the victimized students but rather it responded with “what were they doing there in the first place? If they could have been inside their houses, none of this would have happened.”
With the very recent incident, I was constantly being asked for a report, as to what we have accomplished so far in helping our friends. We engaged a lawyer by ourselves, as we always do, we came up with the bail money of 50,000 Indian Rupees {nearly 2 million Tshs}, we managed to raise that amount on our own, through contributions. Mind you, the bail money was needed immediately or else the 9 Tanzanians would have remained in prison till today.
The Embassy responded with, “the matter is already in the Court, there is nothing much we can do. Just keep us posted with a written report!” And without shame, we hear them in the media claiming that they have helped us and that they are working with us through out this whole time. Very untrue. These have been the common responses I have been receiving from our guardians in New Delhi. It makes us wonder, what are they doing for us.. In 4 years, an official from the High Commission has visited Mysore only ONCE.
And this could not have been possible if it was not for the son of the current Vice President of Tanzania who was studying here at the time. We usually hear from our neighbors in Bangalore that an official is has come from the High Commission for an event or just to come and check on things. We have sent invitations to the Commission several times for various events such as Graduations, but they always reply saying they are caught up with work hence can not make it here. This is not the case with Bangalore.
Mysore and Bangalore is only 2 hours away but these people never make it to Mysore. It is alleged that this is so because most of the students in Bangalore are under Government sponsorship, does this mean others who are under private sponsorship need not be assisted in any way by the High Commission? A year ago, the son of one of the most top officials was studying in Bangalore, everyone here knows what kind of a character he was but yet the Commission made constant visits to Bangalore to clear up whatever mess he had made.
But for the Tanzanians in Mysore, it takes only 1 incident to be blacklisted. If this is so, if the Commission is at the disposal of only the selected few, then it should be disclosed so that us, the sons and daughters of the common laymen, and of the farmers, should look for other means of assistance or other guardians who will look out for our interests. As if it is not enough being discriminated by the locals, our own kind is doing just that.
Due to the lack of assistance from the High Commission, Indians take advantage of us because they know there is no one near to help us since we have left our parents back home and we have come here all alone. We have no choice than to keep aside our differences and look out for each other because we are all we have got in this foreign land, far way from home. A friend of mine once said “The only mistake we have made is for being BLACK.”

BY MWINGA B MUNGWE

MYSORE
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, November 05, 2009 | | Permalink | Maoni 10

Karibu MSHALE ndani ya Jukwaa la Bongo Fleva!”

Wednesday, November 4, 2009

“Wapenzi Wa Muziki kaeni Mkao Wa Kula, MSHALE msanii mpya anakuja kuwashika na Single yake Makini iiitwayo NIWE NAWE, Karibuni. Pini Hili Limerekodiwa Pale Fish Crab ,chini ya Producer Mahiri, LAMAR. Ndani Ya Single Hii Mshale Amemshirikisha Rapper Maarufu katika Tasnia ya Muziki wa Bongo Fleva, ambaye Jina Lake Limehifadhiwa Kwanza Mpaka Single hii Itakapoenda Redioni mapema wiki ijayo. Karibu MSHALE ndani ya Jukwaa la Bongo Fleva!”
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Wednesday, November 04, 2009 | | Permalink | Maoni 4

mwili wa marehemu mzee alex kusaga kuwasili kesho

Baadhi ya viongozi wa juu wa Clouds Media Group, Kulia ni Mzee Gille pamoja na Mzee Changamike wakiwasili leo jioni nyumbani kwa marehemu Alex Kusaga,kwa ajili ya kuwapa pole wafiwa Mbezi Beach jijini Dar.
Kikao cha kamati ya msiba kikijadili jambo leo jioni nyumbani kwa marehemu Mzee Alex Kusaga,Mbezi beach jijini Dar.


Baadhi ya wafanyakazi wa Clouds Media Group wakiwa msibani leo jioni
Mazungumzo ya hapa na pale yakiendelea kuhakikisha taratibu mbalimbali za msiba zinakwenda sawa
Wageni na majirani wakiwa nyumbani kwa marehemu Alex Kusaga aliyefariki jana jioni nchini Afrika ya kusini alikokwenda kutibiwa,Kwa taarifa zilizopatikana ni kwamba mwili wa marehemu utawasili kesho nyumbani kwake Mbezi Beach,na baadae taratibu nyingine za mazishi zitafuata
Pichani ni baadhi ya wafanyakazi wa Clouds Media Group wakiwa nyumbani kwa marehemu Alex Kusaga,Mbezi Beach jijini Dar leo jioni walipokwenda kuwapa pole wafiwa.

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Wednesday, November 04, 2009 | | Permalink | Maoni 0

MILIONI KUMI YA ZAWADI MISS UTALII ILALA 2009 WAREMBO WAPAGAWA DA’ WEST PARK INN-TABATA.


Kivumbi cha kumpata mrembo wa Fainali za Miss Utalii Ilala 2009 ni tarehe 6/11/2009 Ijumaa katika ukumbi wa Da’ West Park Inn Tabata, ambapo jumla ya Warembo 12 watapanda katika jukwaa kuchuana kuwania taji kwa msimu wa 2009/2010.



Katika shindano hilo ambalo macho na masikio kwa wakazi wa Dar es Salaam limewatia wazimu kutokana na kutoelewa nani hataibua nderemo, Vifijo, na makelele kutokana na warembo wote kuwa katika hali ya Ushindani mkali ambapo kila mrembo amejigamba kuibuka na taji hilo kasha kubeba vifaa mbalimbali ikiwa ni pamoja na fedha thamani yake ikiwa ni milioni mbili .

Warembo hao walioanza kambi kwa takribani mwezi mmoja katika Ukumbi wa Da’ West Park Inn-Tabata, waliweza kujifunza masuala mbalimbali yanayohusiana na Utalii unaopatikana Tanzania ikiwemo Hifadhi za Utalii za Taifa, Vivutio vya Kitalii, pamoja na Maajabu ya Dunia yanayopatikana hapa Tanzania.


Aidha katika shindano hilo, warembo hao wataonyesha Mavazi ya asili ya makabila mbalimbali ya Tanzania, watacheza ngoma kuonyesha utamaduni wa Mtanzania, Watavaa mavazi ya Kitanzania ya Kitalii, vazi la Ubunifu lililotengenezwa kwa maligafi za hapa Tanzania, pamoja na mengine mengi yanayohusiana na masuala ya Utamaduni wa Mtanzania.


Warembo wanaowania taji la Miss Utalii Ilala 2009 ni pamoja na ,Tickey Lighton,Neema King’aka, Edna Endrew, Frola Nicholaus, Sheila Baamary, Janeth Samson, Nezia Gabriel, Roselina Sekwao, Jamida Abdu, Aghata Kilala, Tabus Thomas, na Shaymin Ntemena. Zawadi mbalimbali zenye thamani ya shilingi milioni kumi zitatolewa kwa washindi na washiriki, ikiwa ni pamoja na Fedha, na vifaa mbalimbali vyenye thamani mbalimbali, zitalolewa kwa washindi ambapo mshindi wa kwanza kwa mujibu wa Waandaji wa shindano hilo ni thamani ya shilingi milioni 2, mshindi wa pili thamani ya million moja na laki mbili ,mshindi wa tatu thamani ya laki nane na , mshindi wa nne na tano, thamani ya laki tano na mshindi wa Kipaji (Talent) ni thamani ya laki saba na nusu na kifuta jasho kwa wote ni shilingi elfu thelathini na watapatiwa vifaa mbalimbali vyenye thamani ya shilingi laki moja kila mmoja.



Miss Utalii Ilala katika Msimu huu ilipata bahati ya Kuungwa Mkono kwa asilimia mia moja na Mkurugenzi wa Chicken Hut Tanzania ltd ya Mlimani City, Savannah Lounge- Paradise City Hotel iliyopo katika jingo la Benjamini Mkapa Tower-Posta Mpya, Chaga Bite iliyopo Kijitonyama, Kampala International University iliyopo Gongolamboto, pamoja na Ukumbi wa Da’ West Park Inn- Tabata.



Wadhamini wengine waliojitokeza kuunga mkono ni wadau wa Shindano la Miss Utalii ikilinganishwa na miaka ya nyuma, ambapo baadhi ya watu mbalimbali wamejitokeza kusaidia ikiwa ni pamoja na Kampuni ya Ulinzi na Usafirishaji ya Aurora, Kampuni ya Usafirishaji ya Mamaa Sakinma Trans, Mashujaa Pub, Kampuni ya Uongozaji Watalii na Usafirishaji Watalii ya Aucland Tours & Safari, Hotel ya Kisasa ya Grand Villa Hotel iliyopo Kijitonyama, Gym Ya kisasa ya Fitness Centre ya Chang’ombe (Oil Com), Saloon ya Kisasa ya Dage Saloon iliyopo Sinza.


Wengineo ni pamoja na Kampuni ya Vifaa vya Umeme ya Vam General Suplay, Kampuni inayojishughulisha na Mti wa Maajabu Ya Mlonge(Mlonge by Makai Enterprises) na Wabunge wa jiji la Dar es Salaam Burudani mbalimbali zitapatikana katika kupamba Onyesho hilo ikiwa ni pamoja na Kundi la Muziki la Extra Bongo chini ya Ally Choki, Zia Musica,kundi la ngoma za asili Mfalme Bendi chini ya Costa Siboka zamani Mr Ginnes, na makundi mbalimbali ya muziki wa ngoma za asili, mwanamuziki wa kizazi kipya mtanzania anayeishi nchini afrika kusini Abubakari Ally (Kiboot) ambapo wote mnakaribishwa Da’ West Park Inn Tabata.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Wednesday, November 04, 2009 | | Permalink | Maoni 0

MTANDAO WA KISASA WA KUUZA MAGArI WAANZISHWA NCHINI


Mtandao huu hauna gharama kutumia,mtu yoyote mwenye gari lake na anataka kuliuza,anatakiwa kujisajili bila gharama yoyote,na baada ya hapo utaweza kutuma tangazo lako,kama kuna ugumu wowote wa kutumia mtandao huu basi usisite kuwasiliana na wahusika na kuwaeleza shida yako.Sisi tumeamua kuwatumikia Watanzania kwa namna hii. gonga hapa kuingia.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Wednesday, November 04, 2009 | | Permalink | Maoni 4

OBAMA MTOTO GLOBUNI


Mkuu heshima yako,kwa heshima na taadhima naomba uwajulishe wadau kuhusu hii.


Habari Wadau, Napenda kuwatambulisha kwenu Obama mtoto amekuja na blogu yake ambayo itakuwa ikiwahabarisha mambo yote huko ughaibuni.Na pia hata pia kwa habri zinazotokea kule nyumbani (Tanzania). inakwenda kwa jina
http://www.obamamtoto.blogspot.com/


Natumai kupata ushirikiano tosha toka kila kona.Ntanguliza shukrani zangu za dhati kwa wadu wooote!ahsante!haji boston

(Obama mtoto)
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Wednesday, November 04, 2009 | | Permalink | Maoni 11

MWENYEKITI MTENDAJI WA CLOUDS MEDIA GROUP AFARIKI DUNIA




Mwenyekiti mtendaji wa Clouds Media Group,Bw Alex Kusaga ambaye ni baba yake mzazi na Joseph Kusaga, amefariki leo alasiri (jana) Pretoria ,nchini Afrika ya Kusini ambako alipelekwa kwa ajili ya matibabu.


Kwa taarifa zilizopatika ni kwamba msiba upo nyumbani kwake Mbezi-Beach karibu na Giraffe Hotel.



Aidha kwa taarifa zaidi tutaendelea kufahamishana kadiri ya zitakavyokuwa zinatujia.


MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI-AMEN
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Wednesday, November 04, 2009 | | Permalink | Maoni 3

Mitshubishi Pajero inauzwa

Tuesday, November 3, 2009







Model: Mitshubishi Pajero IO
Year of Make : 1999
Size of engine : 1800 cc
Transimission: Automatic
Gari ipo katika hali nzuri
Wasiliana na 0733 660669
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, November 03, 2009 | | Permalink | Maoni 0

wenyewe tumeishaizoea bongo yetu.!



Ukitaka vitoweo a.k.a samaki wabichi basi kula chochoro la msasani bonde la mpunga, basi unakutana na mambo hayo safi kabisa.
Ukipita chohoro ya msasani unakuja kutokea huku tanesco-mikocheni unaendelea zako,lakini huku nako kunakuwa na nyororo ile mbaya,lakini lilikuwa bado halijachanganya sana


Tumelikimbia nyororo tunakumbana na kilami chetu cha ushkaji na vumbi kiani maeneo ya huku msasani.
Vijana wa kazi wakichimba mifereji kwa ajili ya kuweka mabomba ya maji safi maeneo ya msasani leo jioni,wengine wanayaita maji ya mchina sijui kwanini.

Daah.! Wenyewe tunakomaa na bongo yetu,tufanyeje sasa,hii ni jioni ya leo barabara ya Ally-Hassan Mwinyi.Wengine kama vipi unaingia vichochoro vingine kuepuka hii adha ya foleni ya kufuata barabara moja kwa moja.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, November 03, 2009 | | Permalink | Maoni 2

vikwangua anga vyazidi kuinogesha dar

Kikwangua anga Kingine hiki kipo msasani maeneo ya bonde la Mpunga kikifanyiwa finishing
Kikwangua anga kingine hiki kinapanda taratibu kama kionekanavyo leo jioni,kipo mbele ya shule ya sekondari ya Tambaza.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, November 03, 2009 | | Permalink | Maoni 1

mtaa wa msimbazi leo jioni


 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, November 03, 2009 | | Permalink | Maoni 0

vodacom miss tanzania akabidhiwa ndinga yake rasmi leo

Vodacom Miss Tanzania Miriam Gerald akiwa amesimama mbele ya gari lake aina ya Suzuki Vitara Grand mara baada ya kukabidhiwa mchana huu kwenye duka la Vodashop mtaa wa Ohio.
Miriam Gerald akihojiwa na mwandishi wa habari wa TBC1 Evance Mhando mara baada ya kukabidhiwa gari lake mchana huu.


Meneja mkuu wa Makampuni ya Shivacom Parthiban C. wa pili kutoka kulia na Meneja wa udhamini na mawasiliano wa Vodacom Tanzania George Rwehumbiza wakimkabidhi funguo za Gari aina ya Suzuki Grand Vitara Vodacom Miss Tanzania Miriam Gerald katika duka la kampuni hiyo lililopo mtaa wa Ohio jijini Dar mapema leo, Gari hilo jipya lenye thamani ya shilingi milioni 53 litamsaidia mrembo huyo katika kazi zake mbalimbali za kijamii .

Miriam Gerald kutoka Mwanza,alijishindia zawadi hiyo ya gari katika shindano lililofanyika septemba 2 mwaka huu jijini Dar na anatarajiwa kuiwakilisha nchi kwenye shindano la dunia litakalofanyika nchini Afrika Kusini hivi karibuni, anayeshuhudia tukio hilo kushoto ni mkurugenzi wa kamati ya Miss Tanzania Hashim Lundenga.Picha kwa hisani ya Full Shangwe.
Pamoja na kuzawadiwa mchuma wake,Miriam ataagwa keshokutwa kwenye kituo cha Uwekezaji,TIC kwa ajili ya safari yake ya jijin London Uingrereza na baadaye Afrika Kusini.
Miriam anatarajia kuondoka nchini ijumaa amabapo atashiriki mkutano wa siku tatu wa Kimataifa wa biashara ambao utaanza Novemba 9 hadi 11 nchini humo.
akizungumza hivi karibuni jijini Dar,Mwenyekiti wa kamati ya Miss Tanzania, Hashim Lundenga alisema kuwa wanatarajia mrembo huyo atakwenda kuipeperusha vema bendera ya Tanzania.
Lundenga alisema kuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo atakuwa Mkurugenzi wa TIC,Emmanuel Ole Naiko.
Mashindano ya MIss World 2009,yamepangwa kufanyika desemba 12,Sandton Convention Center,mjini Johannesburg.
Mashindano yataanzia London,ambako warembo watawasili Novemba 7,na Novemba 10,watakwenda Dubai,Falme za kiarabu,ambako wataunganisha ndege Novemba 15 kwenda Johannesburg.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, November 03, 2009 | | Permalink | Maoni 0

NATIONAL BUSINESS DIRECTOY


Na mwandishi wetu, Kigali, Rwanda

KAMPUNI ya New Habari (2006) Limited inatarajia kupanua wigo wa kitabuchake cha orodha za simu kwa wafanyabiashara na taasisi mbalimbali kwakuzihusisha nchi za Rwanda na Burundi.

Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano, Udhamini na Matukio wa New Habari (2006)Limited, Petter Mwendapole alisema jana kutoka mjini Kigali Rwanda kwamba lengo la kuzingiiza nchi hizo kupanua wigo wa biashara kwa nchi hizochanga katika Jumuiya ya Afrika Mashariki.

“Tunadhani kuna nafasi ya kukuza biashara kwa nchi hizi mbili ambazozinategemea mambo mengi kutoka Tanzania. Directory hii itasaidiawafanyabiashara wa Tanzania kufahamika Burundi na Rwanda na vile vile wanchi hizo kufahamika Tanzania,” alisema.

Mwendapole altoa kauli hiyo wakati akimkabidhi moja ya Directory za mwakahuu Waziri wa Afrika Mashariki wa Rwanda, Monique Mukuruliza.Katika mkutano uliofanyika ofisini kwa waziri mjini Kigali, WaziriMukuruliza alieleza kufurahishwa kwake na kitabu na kueleza kuwa Rwandainafurahia kujiunga Jumuiya hiyo kwani inauhakika wa kufaidika na mambombalimbali.


“Nchi yetu bado ni changa lakini inapotokea kuna kitu kinawezakuutunganisha pamoja tutakiunga mkono kwa nguvu zetu zote,” alisema.Tayari kampuni mbili zimeonyesha nia ya kusimamia directory hiyo nchini hapa.Directory hiyo ambayo inapatikana katika ofisi zote za ubalozi wa Tanzaniaduniani sasa itakuwa na sehemu ambazo ina anuani za Burundi na Rwanda.Kesho Directory inatarajiwa pia kutambulishwa nchini Burundi.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, November 03, 2009 | | Permalink | Maoni 0

Ailinda's fashion collection at SFW


Swahili Fashion Week 2009 starts on 4th November through 6th November, 2009


I'm happy to inform you that our Tanzanian fashion guru, Ailinda Sawe is featuring in this year's Swahili Fashion Week. Ailinda will be showcasing on the 1st night of the show.Ailinda has over the past 30 years asserted herself as a formidable force behind the Tanzania fashion industry, designing for the home market and being ever so loyal to the culture that feed her with inspiration and spiritual strength.



Ailinda Sawe’s collection is more about a cultural dialogue and connections between different worlds.The dialogue is about where we as Africans come from and where we’re headed to in terms of fashion and ways of dress; it’s a dialogue about what our rich traditional heritage can offer like, for example, the richness of traditional cuts and embellishments.Ailinda also tries to create a connection between the past and the present, African tradition and modernity, tribal costumes and contemporary haute couture.


Her extensive research in tribal costumes and ways of dress coupled with her background as a graduate of the prestigious Mancester Polytechnic Institute in the UK, lends powerful tools to her design work.She tries to explore possibilities with a variety of fabrics without losing site of utility; at the same time accommodating the exoticism of some elements of Swahili culture like the use of the kanga fabric and the baibui.


This year Ailinda celebrates more than three decades of her quest and commitment in those areas, a time in which she established a household brand (Afrika Sana) and a loyal Tanzanian market for her creations.Let's come together and pay homage to our cultural heritage and this icon of culture!


KARIBUNI SANA!

(Tickets are available at various outlets @ TZS20,000)

Mwafrika Merinyo.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, November 03, 2009 | | Permalink | Maoni 0

mtindo wa maisha yako ni uamuzi wako


Kaka michuzi habari, natumai u mzima nasi tupo tunapambana kama kawaida


Lleo ninamchapo mmoja wa mambo ya physical pia ni fundisho kua " mtindo wa maisha yako ni uamuzi wako kwa kuishi kutokana na uhalisia sio nani atakuonaje"
kwa huko kwetu ni ngumu na nia adimu sana kuona mwanamke anajimwaga na baiskeli hasa wale wenye hali ya kati au wenye uwezo ni ndoto kwa Dar es salaam ila kwa mikoani utawaona wengi ila ni wale wasio na uwezo hii ni tofauti sana na huku baiskeli ni kitu cha kawaida tena hutumika kama njia ya mazoezi na sio fedhea kama ilivyo huko nyumbani.


Nyumbani baiskeli ni maarufu sana mwanza na shinyanga. Kunamama huyu ni miaka 50 au zaidi nimekutana nae zaidi ya mara 5 ila nilishindwa jinsi yakumpiga picha ingeniletea matatizo kumpiga picha bila idhini yake siku moja nimeamka asubuhi kama zali tu nachungulia chini nje ya jengo naloishi namuona kapaki anazungumza na dada mmoja basi pale pale nikammulika je mama wa miaka 50 kwetu anaweza endesha baiskeli na akajivunia bila kujistukia?


pia kuna mama mmoja ni bonge balaa ila anakimbiza baiskeli ajabu namvizia nae nitampata tu then picha nitaimuvuzisha ktk blog yetu ya Jiachie. Kaka nawatakia fiesta njema bila shaka itakua bomba balaa full one love big up.


Malik williams


Venice Italy
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, November 03, 2009 | | Permalink | Maoni 1

TOYOTA SPRINTER TRUENO FOR SALE!







Model: Toyota Sprinter Trueno
Year: 1999Engine
size: 1600cc,very economical!
Transmission: Automatic
Mileage: 91,000
KMFuel: Petrol
Descriptions:Anti-Lock Brakes / Driver Airbag / Passenger Airbag / Power Windows / A/C: front / Power Steering / Remote Keyless Entry / Tilt Wheel / AM/FM Radio / AM/FM Stereo / CD player / Alloy Wheels / Power Mirrors.
Gari ipo katika hali nzuri sana kama inavyoonekana kwenye picha, imelipiwa kodi zote.
Bei: 7 Million (maelewano yapo)
Wasiliana nami simu no: 0713 466579 / 0655 888757
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, November 03, 2009 | | Permalink | Maoni 2
Idadi ya watu