JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


TICTS FAMILY DAY BONANZA ILIVYOFANYA JIJINI DAR

Share This
 Kamati ya Maandalizi ya Bonanza la Familia za Wafanyakazi wa Kampuni ya kuhudumia makontena Tanzania katika bandari ya Dar es salaam (TICTS), ikiwa katika picha ya pamoja wanati wa sherehe hiyo, iliyofanyika mwishoni mwa wiki katika Hoteli ya Kunduchi Beach, jijini Dar es salaam.

Katika Bonanza hilo, wafanyakazi wa kampuni hiyo pamoja na familia zao walishindana katika michezo mbali mbali, ikiwemo ya mpira wa miguu, kivuta kamba, kuogelea, kukimbia na magunia na mingineyo huku watoto walitoana jasho katika kulisakata dansi na kuogelea huku wengine wakiondoka na zawadi kemkem.

Akizunguma katika Bonanza hilo, Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni hiyo, Jared Zerbe alisema lengo kubwa la Siku hiyo ilikuwa ni kuwakutanisha wafanyakazi na familia zao ziweze kufurahi kwa pamoja na pia kusherehekea kuuaga mwaka na kujiandaa kuukaribisha mwaka mpya katika kazi zao.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya kuhudumia makontena Tanzania katika bandari ya Dar es salaam (TICTS), Jared Zebre (wa nne kulia) akikabidhi kikombe kwa wafanyakazi wa kampuni hiyo waliounda timu ya Mameneja baada ya kuibuka kidedea kwa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya timu ya wakanyakazi wa ngazi y chini, katika mchezo wa Bonanza la Familia za Wafanyakazi hao, lililofanyika kwenye ufukwe wa Hoteli ya Kunduchi, jijini Dar es salaam. wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa Maendeleo wa Kampuni ya TICTS, Donald Talawa na kushoto ni, Meneja Utekelezaji wa Kampuni hiyo, Patrick Kusiga.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya kuhudumia makontena Tanzania katika bandari ya Dar es salaam (TICTS), Jared Zebre (pili kushoto) akipikea tuzo maalum kutoka kwa viongozi wa Kamati ya Maandalizi ya Bonanza la Familia za Wafanyakazi wa Kampuni hiyo, lililofanyika kwenye ufukwe wa Hoteli ya Kunduchi, jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki.
Mkuu wa Kitengo cha Uendeshaji wa Kampuni ya kuhudumia makontena Tanzania katika bandari ya Dar es salaam (TICTS), Erik Sazs akijaribu kuuzuia mpira bila mafanikio katika mchezo wa Bonanza la Familia za Wafanyakazi wa Kampuni hiyo, lililofanyika kwenye ufukwe wa Hoteli ya Kunduchi, jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki.
Mkali wao akiondoka na mpira .
Mkuu wa Kitengo cha Uhandishi wa Kampuni ya kuhudumia makontena Tanzania katika bandari ya Dar es salaam (TICTS), Cornelis Kwadjik akijaribu kumkoka mmoja wa wachezaji wa timu ya Wafanyakazi wa Kampuni hiyo, katika bonanza la familia za wafanyakazi hao, lililofanyika kwenye ufukwe wa Hoteli ya Kunduchi, jijini Dar es salaam, mwishoni mwa wiki.
Mpira wa Wavu
Kuvuta kamba.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad