Kamati
ya Maandalizi ya Bonanza la Familia za Wafanyakazi wa Kampuni ya
kuhudumia makontena Tanzania katika bandari ya Dar es salaam (TICTS),
ikiwa katika picha ya pamoja wanati wa sherehe hiyo, iliyofanyika
mwishoni mwa wiki katika Hoteli ya Kunduchi Beach, jijini Dar es salaam.
Katika
Bonanza hilo, wafanyakazi wa kampuni hiyo pamoja na familia zao
walishindana katika michezo mbali mbali, ikiwemo ya mpira wa miguu,
kivuta kamba, kuogelea, kukimbia na magunia na mingineyo huku watoto
walitoana jasho katika kulisakata dansi na kuogelea huku wengine
wakiondoka na zawadi kemkem.
Akizunguma
katika Bonanza hilo, Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni hiyo, Jared Zerbe
alisema lengo kubwa la Siku hiyo ilikuwa ni kuwakutanisha wafanyakazi na
familia zao ziweze kufurahi kwa pamoja na pia kusherehekea kuuaga mwaka
na kujiandaa kuukaribisha mwaka mpya katika kazi zao.
Afisa
Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya kuhudumia makontena Tanzania katika bandari
ya Dar es salaam (TICTS), Jared Zebre (wa nne kulia) akikabidhi kikombe
kwa wafanyakazi wa kampuni hiyo waliounda timu ya Mameneja baada ya
kuibuka kidedea kwa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya timu ya wakanyakazi wa
ngazi y chini, katika mchezo wa Bonanza la Familia za Wafanyakazi hao,
lililofanyika kwenye ufukwe wa Hoteli ya Kunduchi, jijini Dar es salaam.
wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa Maendeleo wa Kampuni ya TICTS, Donald
Talawa na kushoto ni, Meneja Utekelezaji wa Kampuni hiyo, Patrick
Kusiga.
Afisa
Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya kuhudumia makontena Tanzania katika bandari
ya Dar es salaam (TICTS), Jared Zebre (pili kushoto) akipikea tuzo
maalum kutoka kwa viongozi wa Kamati ya Maandalizi ya Bonanza la Familia
za Wafanyakazi wa Kampuni hiyo, lililofanyika kwenye ufukwe wa Hoteli
ya Kunduchi, jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki.
Mkuu
wa Kitengo cha Uendeshaji wa Kampuni ya kuhudumia makontena Tanzania
katika bandari ya Dar es salaam (TICTS), Erik Sazs akijaribu kuuzuia
mpira bila mafanikio katika mchezo wa Bonanza la Familia za Wafanyakazi
wa Kampuni hiyo, lililofanyika kwenye ufukwe wa Hoteli ya Kunduchi,
jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki.
Mkali wao akiondoka na mpira .
Mkuu
wa Kitengo cha Uhandishi wa Kampuni ya kuhudumia makontena Tanzania
katika bandari ya Dar es salaam (TICTS), Cornelis Kwadjik akijaribu
kumkoka mmoja wa wachezaji wa timu ya Wafanyakazi wa Kampuni hiyo,
katika bonanza la familia za wafanyakazi hao, lililofanyika kwenye
ufukwe wa Hoteli ya Kunduchi, jijini Dar es salaam, mwishoni mwa wiki.
Mpira wa Wavu
Kuvuta kamba.
No comments:
Post a Comment