JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


MDAU ATOA SHUKRANI KWA MICHANGO YA MATIBABU

Share This
SHUKRANI
Habari Ndugu zetu Watanzania mlio ndani na nje ya nchi nawasalimu.

Natumaini wote mko salama.
Kwa niaba ya Dada yetu Ndugu yetu Mtanzania Mwenzetu AMINA ALLY JUMA na Familia yake yote kwa ujumla, Leo tunarudi kwenu kwa SHUKRANI ZA DHATI kwa Moyo kwa kujitolea kwenu kwa hali na Mali na Sala zenu.

Tangu Mwezi uliopita tulikuja kwenu kwa ajili ya kuomba msaada kwa ajili ya Dada yetu AMINA anayesumbuliwa na maradhi ya Saratani ya Damu (ACUTE AMELOID LEUKEMIA) Ambaye kwa sasa yuko nchini India akiendelea na Matibabu.

Napenda Kuwashukuru sana Wadau wote walioweza kuusambaza ujumbe, hasa kwa njia ya mitandao (Social Media) kwani mchango wenu umekuwa mkubwa mno na uliozaa matunda mema. 

Tumefanikiwa kupata kiasi ($7500.00) ambacho kilitakiwa kwaajili ya kutimiza malengo ya dada Yetu AMINA kwa matibabu yake, TUNAWASHUKURU WOTE WALIOJITOLEA KWA HALI MALI NA SALA ZENU MWENYEZI MUNGU AZIDI KUWABARIKI NA TUENDELEE NA USHIRIKIANO HUU.

Pia tunatanguliza shukrani zetu za dhati kwa, MICHUZI BLOG, WANAWAKE LIVE, SMILEY KIDS EVENTS, ZAMARADI MKETEMA, JOKATE MWEGELO, 8020 FASHION BLOG, SARAH RAQEY, DINA MARIOS, ITV na wengine wote kwa njia moja tuliweza kujitoa kwa nia njema katika kuwajibika, TUNASEMA ASANTENI SANA SANA NA MUNGU AWABARIKI.

KUANZIA LEO HII 20/11/2015 TUNASITISHA MICHANGO HII NA TUKIMSHUKURU SANA MUNGU KWA WEMA WAKE WOTE.

Tunawashukuru sana kwa Michango yenu yote, kwa ushirikiano tumetimiza lengo, na sasa tumemkabidhi Mungu mwenyezi muumba wetu atende miujiza yake kwa Dada yetu AMINA na ndugu zetu wote walioadhirika na ugonjwa huu tuzidi Kuombeana Kupendana na Kushirikiana.

PS: KUTAKUWA NA DUA YA SHUKRANI NYUMBANI KWA AMINA MIKOCHENI B’ WARIOBA, TAASISI STREET, SIKU YA IJUMAA 27/11/2015 KWA WALE WATAKAOWEZA KUFIKA KARIBUNI SANA.

ASANTENI SANA KAZI NJEMA NA MUNGU AWABARIKI ……AMEN

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad