Bank Of Afrika imezindua huduma mpya ya kutuma na kupokea fedha kutoka mahali popote duniani kwa gharama naafuu.
Kwa mujibu wa Afisa masoko wa Benki hiyo, Daniel Sarungu
huduma hiyo itakuwa ikiwahudumia watu wote wenye akaunti kwenye benki
hiyo pamoja na wale wasio na akaunti, “Ni benki ambayo itawahudumia watu
wote wenye akaunti hapa kwentu na wasio na akaunti,”alisema.
Mkuu wa ICT wa benki hiyo, Willington Munyaga aliwataka
watanzania kuitumia huduma hiyo kwa madai kuwa ni njia salama na rahisi
na kwamba, itakuwa ikitolewa katika matawi yote 21 ya benki hiyo yaliyo
Dar es salaam nan je ya jiji la Dar es salaam.
Meneja wa huduma za kielectronic Editha Jumbe alisema kuwa,
wateja wa huduma hiyo watakuwa wakipokea ujumbe wa simu mara wanapotuma
fedha zao na wakati zinapotolewa na kuondoa gharama ya kupita simu au
kutuma email hasa kwa wateja wa ughaibuni ili kujua kama wamepatiwa
huduma hiyo.
No comments:
Post a Comment