Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa kitengo cha Uhandisi wa Tanzania International Container Terminal Services Ltd (TICS) Cornelius Kwadijk, Mkurugenzi wa Maendeleo, Donald Talawa, Meneja rasilimali watu, Sadick Abdalla na Mwalimu mkuu wa shule ya sekondari ya Kurasini Florentine Assenga wakipanda miti katika shule hiyo jijini Dar es Salaam jana. Miche hiyo 250, mbolea na udongo wa kuistawisha imetolewa na TICS katika kampeni yake yenye kauli mbiu ya GO Green.
Waalimu wa shule ya sekondari ya Kurasini wakiwa na viongozi wa TICS kabla ya kuanza zoezi la kupanda miche 250 kwenye eneo la shule hiyo jijini Dar es Salaam jana. Miche hiyo, mbolea na udongo wa kuistawisha imetolewa na TICS katika kampeni yake yenye kauli mbiu ya GO Green.
Mfanyakazi wa TICS Slyvester Ntomba (kulia) akijumuika na wanafunzi wa shule ya sekondari ya Kurasini kupanda miche katika eneo la shule hiyo jijini Dar es Salaam jana. Miche hiyo 250, mbolea na udongo wa kuistawisha imetolewa na TICS katika kampeni yake yenye kauli mbiu ya GO Green.
Wanafunzi wa shule ya sekondari ya Kurasini
wakipanda miche katika eneo la shule hiyo jijini Dar es Salaam jana. Miche hiyo
250, mbolea na udongo wa kuistawisha imetolewa na TICS katika kampeni yake
yenye kauli mbiu ya GO Green.
No comments:
Post a Comment