JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


TAASISI YA MOYO YA JAKAYA KIKWETE YAZINDULIWA LEO DAR ES SALAAM

Share This
Waziri wa Afya Dokta Seif Rashid
Na: Neema  Mwangomo, MHN                                              04  Sept  2015
 
Rais JAKAYA  KIKWETE leo amezindua Taasisi ya Moyo ambayo itajulikana kwa jina la  Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete ( The Jakaya  Kikwete Cardiac Institute ) ambayo itatoa mafunzo ya Ubingwa wa juu katika fani ya Upasuaji wa Moyo , Usingizi na Tiba ya Moyo kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili( MUHAS).

            Akizindua Taasisi hiyo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam kwa niaba ya Rais JAYAKA KIKWETE , Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dokta   SEIF  RASHID amesema taasisi hiyo  imeleta ahueni  kwa wagonjwa  wa moyo nchini ambapo kati ya Januari hadi Agosti mwaka huu imehudumia wagonjwa wa nje 14, 257 ,wagonjwa waliolazwa ni 912 na imefanya upasuaji kwa wagonjwa 148.

            Kati ya wagonjwa waliofanyiwa upasuaji ,wagonjwa watano tu ndio waliofariki Dunia ambao ni Asilimia 3. 4 , kiwango ambacho ni kidogo kuliko wastani uliokisiwa na wataalam wa asilimia 13.


            Akifafanua amesema huduma zilizotolewa na taasisi hiyo  zimeokoa kiasi cha Shilingi 1, 915,440,000  iwapo wagonjwa hao  wangepelekwa kutibiwa nje ya nchi.

            Akielezea kuhusu hali ya magonjwa yasiyo na maambukizi amesema magonjwa hayo hujumuisha magonjwa ya Moyo , Kisukari na Saratani na kwamba takwimu za Shirika la Afya Duniani ( WHO) zinaonesha kuwa takribani watu Milioni 17 hupoteza maisha kila mwaka Duniani ambayo ni sawa na asilimia 60 ya vifo vyote vinavyotokea.

            Hata hivyo amesema sababu kuu ya maradhi ya moyo nchini Tanzania kama ilivyo katika nchi nyingine za Afrika zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara ni mbili , moja ni homa ya Rumatiki  pamojaa  na magonjwa ya moyo ya kurithi au kuzaliwa nayo  .
           
Inaendelea
Kwa upande wake Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii , Dokta SEIF RASHID amesema , huduma za upasuaji wa moyo katika Hopsitali ya Taifa Muhimbili ilianza Mei 21 , 2008 na mpaka sasa huduma zinazopatikana ni za upasuaji wa moyo , matibabu ya moyo , vipimo vya moyo na uchunguzi wa mishipa na shinikizo.

            Kwa mujibu wa Dokta SEIF RASHID kutoka mwaka 2008  mpaka mwaka 2015  wagonjwa 600 wamefanyiwa upasuaji wa Moyo na hadi kufikia Agosti mwaka huu Taasisi imeweza kufanya upasuaji kwa wagonjwa wa moyo 145 idadi hii inajumuisha wagonjwa waliofanyiwa upasuaji  mkubwa wa moyo na waliozibwa matundu ya moyo bila upasuaji.

            Naye Mwenyekiti wa Bodi Hospitali ya Taifa Muhimbili  Profesa JOSEPH KUZILWA  amesema taasisi hiyo ni ya kisasa , yenye vifaa vya hali ya juu vinavyotumia teknolojia ya kisasa katika uchunguzi na tiba ya magonjwa ya moyo.

            Akielezea mafanikio Profesa KUZILWA amesema kwa kushirikia na Madaktari bingwa kutoka nchi rafiki ,kituo kimefanya upasuaji wa moyo kwa wagonjwa 148 , kimechunguza mishipa ya moyo kwa kutumia kifaa maalum kwa wagonjwa 160 , kimewawekea Stents wagonjwa 9 na kuwawekea vifaa vya mapigo ya moyo wagonjwa 13.

            Jengo hilo lenye thamani ya Shilingi Bilioni 16. 6 limejengwa na Serikali ya China ambapo  serikali ya Tanzania imenunua vifaa vyenye thamani ya Shilingi Bilioni

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad