JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


VIJANA NA WALEZI ZAIDI YA 1000 WAPATIWA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI ARUSHA

Share This

 Na Pamela Mollel,Arusha

Mafunzo ya ujasiriamali wa kuzalisha bidhaa mbalimbali yanayotolewa kwa vijana na walezi ikiwa ni hatua ya kuwezesha jamii kujitafutia kipato ili kumudu malezi ya watoto.

vijana na walezi hao ni zaidi ya 1000 Mkoani Arusha wamekusanywa kwa pamoja kwaajili ya kupatiwa mafunzo ya  ujuzi wa ujasiriamali kupitia shirika la viwanda vidogo vidogo SIDO kwa kushirikiana na taasisi ya SOS pamoja na  wadau wengine kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kiuchumi.

Meneja wa SIDO Mkoa wa Arusha Japhari Donge akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo hayo amesema mpango huo wa awamu ya kwanza imejumuisha vijana na walezi wapatao  300wakiwemo vijana wakiume na wakike  ambao wanapatiwa mafunzo ya kuzalisha bidhaa mbalimbali kwa matumizi ya kijamii .

Kwa upande wake  mgeni rasmi ambaye ni Katibu tawala msaidizi Mkoa wa Arusha, anayehusika na viwanda,uwekezaji na biashara frank Mbando amesisitiza vijana kutumia vyema fursa zinazotolewa ili waweze kukuza uchumi wao na uchumi wa taifa kwa kuzalisha bidhaa zenye ubora na zenye kukidhi maitaji ya kila siku .

“Vijana hii ni fursa itumie vizuri,ili muweze kujifunza aina mbalimbali ya ujasiriamali jambo hili litawezesha kukua kwa uchumi wetu”anasema Mbando

kwa upande wake mratibu wa uwezeshaji wa familia na vijana kutoka shirika la  SOS Mkoa wa Arusha Willson  Rando amesema maradi huo unafanya kazi ya malezi mbadala kwenye jamii ,kusaidia vijana kujikwamua kiuchumi pamoja na utoaji wa mafunzo ya ujasiriamali.

Ameongeza kuwa wao ni miongoni mwa waezeshaji wa mafunzo hayo kwa vijana yatakayowawezesha kujikita kufanya shughuli za ujasiriamali kwa lengo la kupata ajira na kujiongezea kipato.



 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad