JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


TMDA YAJIVUNIA MAFANIKIO YAKE KATIKA KIPINDI CHA MIONGO MIWILI

Share This

 


Na Mwandishi Wetu

MAMLAKA ya Dawa na Vifaa Tiba ( TMDA) imesema imefanikiwa kwa kiasi kikubwa kufikia malengo yake kwa kuhakikisha jamii inalindwa afya zao na inakuwa salama kutokana matumizi ya dawa, vifaa tiba, vitendanishi na bidhaa nyinginezo zinazohusiana na afya.

Akizungumza leo wakati wa Kikao kazi cha Wahariri na Waandishi wa habari Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo Adan Fimbo amesema katika kipindi cha miongo miwili katika usimamizi wa bidhaa za dawa, vifaa tibana na vitendanishi wanajivunia mafanikio makubwa katika kutoa huduma.

Ametaja baadhi ya mafanikio yaliyokiwa katika kipindi cha miaka 20, ni kuanzishwa kwa Mamlaka ya udhibiti, Kukamilisha ujenzi wa upanuzi wa Maabara ya Dar es Salaam, Kubuni, kuanzisha na kutekeleza mradi wa Duka la Dawa Muhimu (DLDM / ADDO)

Pia kuzindua na kuanzisha Ofisi ya Kanda ya Ziwa, jijini Mwanza (sasa Kanda ya Ziwa Mashariki), kukamilisha ujenzi wa Ofisi ya Makao Makuu ya iliyokuwa Mamlaka ya Chakula na Dawa - TFDA (sasa Ofisi Ndogo ya Makao Makuu TMDA na Kanda ya Mashariki)

Ametaja mafanikio mengine ni kuzindua rasmi jengo la Ofisi ya Makao Makuu ya iliyokuwa Mamlaka ya Chakula na Dawa - TFDA (sasa Ofisi Ndogo ya Makao Makuu TMDA na Kanda ya Mashariki), kuanzisha, kukidhi na kutekeleza mifumo ya utendaji kazi ya kimataifa ya ISO 1901:2018

Pia kupata tuzo ya kuwa taasisi ya kwanza yenye mifumo bora ya utendaji kazi Serikalini (Best Managed Institution in Tanzania), Maabara ya TMDA kuwa na umahiri unaotambuliwa na Shirika la Afya Duniani (WHO Prequlified Laboratory) na Kituo cha umahiri wa usajili dawa barani Afrika

Ametaja pia Maabara ya mafunzo ya umahiri kwa Mamlaka za Udhibiti Dawa barani Afrika, Kuanzisha mifumo ya kielekroniki ya utoaji huduma kwa wateja,Kutoa huduma za udhibiti kwa njia ya kielektroniki (automation of regulatory services)

Fimbo ametaja kuimarika kwa makusanyo hivyo kuchangia asilimia 15 ya mapato yake katika gawio la Serikali na kuwa na ziada ya asilimia 70 kama inavyoekekezwa na Hazina

Mengine ni Kukamilisha ujenzi wa jengo la Ofisi ya TMDA Kanda ya Ziwa Mashariki Mwanza na kuanza kutumi, Kuanzisha mazingira wezeshi na rafiki ya ufanyaji biashar nchini kwa bidhaa zinazodhibitiwa na TMDA

Pia Kufikia Ngazi ya tatu ya Shirika la Afya Duniani - WHO(WHO Maturity L-3) kwa kuwa na mifumo bora ya udhibiti dawa barani Afrika hivyo kuwa taasisi ya kwanza ya udhibiti na kuifanya Tanzania kuwa nchi ya kwanza barani Afrika kufikia ngazi hiyo

Aidha Maabara ya TMDA kupata hadhi ya juu ya ngazi ya nne umahiri wa Shirika la Afya D\uniani, Kubadili jina kutoka TFDA kuwa TMDA, Kukamilisha ujenzi wa jengo la Ofisi ya TMDA Kanda ya Kati Dodoma na kuanza kutumika

Pia Mamlaka kupewa jukumu la udhibiti wa bidhaa za tumbaku,kuanzisha mfumo wa kufuatilia utoaji taarifa za madhara yatokanayo na matumizi ya dawa kwa njia ya simu

Mafanikio mengine ni Mamlaka kupata Hati safi kwa miaka 20 mfululizo kutokana na ukaguzi wa hesabu za taasisi kwa ukaguzi unaofanywa na ofisi ya CAG na kutimiza miaka 20 ya taasisi katika kulinda afya ya jamii kwa ufanisi.

Akifafanua pamoja na mafanikio tajwa, Mamlaka inaendelea kuboresha huduma zake kwa kuzingatia maoni ya wateja. mathalan, kwa Mujibu wa utafiti uuliofanywa na Shule ya Biashara ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (University of Dar es Salaam Business School) wa Desemba 2020 kuhusu wateja kuridhika na huduma zitolewazo na Mamlaka.

Amesema katika halmashauri 28 kwenye mikoa 14 ya Tanzania, ulibaini kuwa asilimia 47 tu ya wananchi ndiyo wanaifahamu TMDA. Ni dhahiri kwamba matokeo haya yanaakisi mabadiliko ya jina la taasisi yaliyofanyika mwaka 2019.

"Hata hivyo, Mamlaka inatambua mchango wa vyombo vya habari katika kuongeza uelewa wa wananchi kuifahamu Mamlaka.Kwa kuwa upo umuhimu mkubwa wa wadau wote wa TMDA kuifahamu Mamlaka na majukumu yake...

"Wahariri na Waandishi wa Habari wana wajibu mkubwa katika kuhakikisha kuwa Mamlaka inajulikana kwa jamii na Sheria tajwa inasimamiwa kiufanisi, TMDA imekuwa na utaratibu wa kukutana na wadau wake kwa lengo la kuwaelimisha juu ya kazi zake sanjari na majukumu ya kila mdau katika kutekeleza Sheria husika."

Kuhusu suala la uelimishaji jamii limepewa kipaumbele kikubwa na TMDA na ndiyo sababu tumewaita hapa Wahariri walioko mbele yako kwa lengo la kuwashirikisha mafanikio yaliyofikiwa na TMDA ili kujadiliana kwa pamoja namna ya kushirikiana zaidi katika kuhakikisha kuwa soko la Tanzania lina bidhaa zilizo bora, salama na fanisi ili kumlinda mlaji.

Amesema kimsingi, kazi hii sio rahisi na inahitaji ushirikiano wa karibu kati yetu sisi TMDA, waandishi wa habari na wananchi wote kwa ujumla wao.

Ameongeza ni matumaini yao kupitia tasnia ya habari, wataweza kuwafikia wananchi wengi zaidi na kuwapa elimu endelevu ili waweze kufanya maamuzi sahihi wakati wa kuchagua, kununua na kutumia bidhaa zinazodhibitiwa na TMDA kutoka katika soko.

Kuhusu Kikao kazi hicho amesema mada mbalimbali zimewasilishwa katika kikao hiki ambapo ni matarajio yao kuwa baada ya semina hiyo, washiriki waweze kuelewa vyema nini Mamalaka imetekeleza na katika kuhakikisha sheria na majukumu ya TMDA yanatekelezwa katika kulinda afya ya jamii.

Aidha, kupitia hoja zitakazoibuliwa baada ya mada husika kutolewa, tutaainisha kwa pamoja maeneo ya ushirikiano katika kuielimisha zaidi jamii kupitia vyombo vya habari kuhusu masuala yahusuyo udhibiti wa bidhaa za dawa vifaa tiba na vitendanishi kutokana na ukweli usimamizi wa Sheria hautakuwa na mafanikio kama hatutakuwepo na ushirikishwaji wa wadau wetu hususan vyombo vya habari.

"Ni imani yetu kuwa Wahariri na Waandishi hawa wakirudi kwenye maeneo yao ya kazi wataweza kueneza ujumbe watakaopata leo kwa watu wengi zaidi na hivyo kuwezesha jamii kupata elimu, kujilinda na kutumia dawa, vifaa tiba na vitendanishi vilivyosajiliwa au kupitishwa na TMDA."
Mkurugenzi Mkuu wa TMDA Adam Fimbo akizungumza wakati wa Kikao kazi cha Wahariri na Waandishi wa habari kilichofanyika jijini Dar es Salaam

Baadhi ya Wahariri wa Habari na watendaji wa TMDA wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, albert Chalamila alipokuwa akizungumza katika kikao kazi hicho.

Meneja Mawasiliano na Elimu kwa Umma, Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) Gaudencia Simwanza akitoa neno la ukaribisho kwa Wahariri wa Habari waliohudhuria katika kikao kazi hicho.

Baadhi ya Wahariri wa Habari na Watendaji wa TMDA katika kikao kazi hicho.

Picha ya Pamoja. Kaimu Meneja Huduma za Sheria wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA), Martha Malle, akitoa mada katika kikao kazi hicho kuhusu Sheria na Kanuni mbalimbali za udhibiti, za Mamlaka hiyo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad