jlogo

Karibuni Jamvini Wanajamii

topads

Post Top Ad

demo-image

UCHAGUZI MKUU WA CHAMUDATA WAFANA, LUIZER MBUTU AWEKA HISTORIA YA KUWA MWANAMKE WA KWANZA KUONGOZA CHAMA

Share This

Mwanamuziki Luizer Mbutu Nyoni ameweka historia usiku wa Jumatano Mei 11, mwaka huu kwa kuwa mwanamke wa kwanza nchi kushinda nafasi ya Mwenyekiti Chama cha Muziki wa Dansi Tanzania (CHAMUDATA) kufuatia uchaguzi mkuu uliofanyika ukumbi wa Dar Modern ulioko Magomeni Mikumi mtaa wa Ifunda jijini Dar es Salaam.

Luizer mwimbaji tegemeo na wa siku nyingi wa Twanga Pepeta, aliwashinda kwa mbali wapinzani wake Mwinjuma Muumini (Aliyeshika nafasi ya pili) na Said Kaunga.

Mwimbaji wa Sikinde, Abdallah Hemba akafanikiwa kushinda nafasi ya Makamu Mwenyekiti aliyokuwa akiipigania na mwanamuziki wa Tabora Jazz, Ramadhani Kitenge.

Katika nafasi ya Katibu Mkuu meneja wa Msondo Ngoma, Said Kibiriti alimbwaga Hassan Msumari aliyekuwa akitetea kiti chake.

Katibu Msaidizi wa Chamudata aliibuka wakili Msomi Baraka Elias Sulus ambaye alikuwa mgombea pekee na hivyo kura za ndio zikampitisha kwa kishindo, japo yeye mwenyewe hakuwepo ukumbini.

Nafasi sita za Wajumbe wa Kamati ya Utendaji zilizokuwa na mchuano mkali, zikaenda kwa Profesa Abuu Omar, Cecy Jeremiah Logome Mwasi Kitoko, Bernedict Berno Sanga, Said Mdoe, Gabriel Bakilana na Rhobi Chacha. Wagombea wengine Matei Joseph, Shomary Ally, Tabu Mambosasa, Andrew Mwampashi na Sholinda Mwezimpya kura hazikutosha.

Uchaguzi wa Chamudata ulifanyika kwa uwazi wa hali ya juu chini ya usimamizi wa Mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi, Kamanda Mstaafu Jamal Rwambo (SACP) na kufanya zoezi hilo likamilike bila malalamiko ya upande wowote.

Hiyo ilijidhihirisha pale wagombea walioshindwa wote walipojitokeza meza kuu na kutia Saini fomu za matokeo  na walipopewa nafasi ya kusema machache baada ya uchaguzi walikubali matokeo na kupongeza mchakato mzima wa uchaguzi huo ulivyofanyika.

SAFU MPYA YA UNGOZI WA CHAMUDATA NI HII HAPA:

MWENYEKITI
Luizer Morris Nyoni

MAKAMU MWENYEKITI
Abdallah Hamis Hemba

KATIBU MKUU
Said Nassoro Kibiriti

KATIBU MSAIDIZI
Baraka Elias Sulus (Advocate)

WAJUMBE (NAFASI SITA):
1. Abbu Omar Abubakar
2. Cecy Jeremiah Lugome
3. Said Abdillahi Mdoe
4. Bernedict Berno Sanga
5. Gabriel Byabato Bakilana
6. Rhobi Abubakari Chacha

Nafasi za Mweka Hazina na msaidizi wake  hazikujazwa kwa kuwa hakuna aliyejitokeza kugombea. Hivyo mwCHAMUDATA MPYA YAPATIKANA ...Luizer kidedea, Msumari aanguka

Luizer (Mbutu) Nyoni amefanikiwa kushinda nafasi ya Mwenyekiti Chama cha Muziki wa Dansi Tanzania (CHAMUDATA) kufuatia uchaguzi mkuu uliofanyika Jumatano jijini Dar es Salaam.

Katika uchaguzi huo wa Chamudata uliofanyika kwenye ukumbi wa Dar Modern ulioko Magomeni Mikumi, Luizer mwimbaji tegemeo wa Twanga Pepeta, aliwashinda kwa mbali wapinzani wake Mwinjuma Muumini (Aliyeshika nafasi ya pili) na Said Kaunga.

Mwimbaji wa Sikinde, Abdallah Hemba akafanikiwa kushinda nafasi ya Makamu Mwenyekiti aliyokuwa akiipigania na mwanamuziki wa Tabora Jazz, Ramadhani Kitenge.

Katika nafasi ya Katibu Mkuu wa Chamudata, meneja wa Msondo Ngoma, Said Kibiriti akambwaga Hassan Msumari aliyekuwa akitetea kiti chake.

Katibu Msaidizi wa Chamudata ni Wakili Msomi Baraka Elias Sulus ambaye alikuwa mgombea pekee na hivyo kura za ndio zikampitisha kwa kishindo.

Nafasi sita za Wajumbe wa Kamati ya Utendaji ambazo zilikuwa na mchuano mkali, zikaenda kwa Abuu Omar, Cecy Jeremiah Logome, Bernedict Berno Sanga, Said Mdoe, Gabriel Bakilana na Rhobi Chacha huku kura zikishindwa kutosha kwa Matei Joseph, Shomary Ally, Tabu Mambosasa, Andrew Mwampashi na Sholinda Mwezimpya.

Uchaguzi wa Chamudata ulifanyika kwa uwazi wa hali ya juu chini ya usimamizi wa Mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi, Kamanda Mstaafu Jamal Rwambo (SACP) na kufanya zoezi hilo likamilike bila malalamiko ya upande wowote.

Hiyo ilijidhihirisha pale wagombea walioshindwa walipopewa nafasi ya kusema machache baada ya uchaguzi ambapo wote walikubali matokeo na kupongeza mchakato wa uchaguzi huo ulivyofanyika.

SAFU MPYA YA UNGOZI WA CHAMUDATA NI HII HAPA:

MWENYEKITI
Luizer Morris Nyoni

MAKAMU MWENYEKITI
Abdallah Hamis Hemba

KATIBU MKUU
Said Nassoro Kibiriti

KATIBU MSAIDIZI
Baraka Elias Sulus (Advocate)

WAJUMBE (NAFASI SITA):
1. Abbu Omar Abubabar
2. Cecy Jeremiah Lugome
3. Said Abdillahi Mdoe
4. Bernedict Berno Sanga
5. Gabriel Byabato Bakilana
6. Rhobi Abubakari Chacha

Nafasi za Mweka Hazina na msaidizi wake hazikuweza kujazwa kwa kuwa hakuna aliyejitokeza kugombea. Hivyo Mwenyekiti wa uchaguzi akatangaza kwamba zitajazwa siku za usoni kwa kufuata muongozo wa katiba ya Chamudata.

 
Varda Arts walikuwepo
c2
Sehemu ya wajumbe
c3

Uchaguzi wa Chamudata ulifanyika kwa uwazi wa hali ya juu chini ya usimamizi wa Mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi, Kamanda Mstaafu Jamal Rwambo (SACP) 

c4

 Mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi, Kamanda Mstaafu Jamal Rwambo (SACP) akiwa meza kuu na wasimamizi 

c5
Kura zikihesabiwa
c6
Mwenyekiti akitoa maelekezo
c7
Uchaguzi wa Chamudata ulifanyika kwa uwazi wa hali ya juu chini ya usimamizi wa Mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi, Kamanda Mstaafu Jamal Rwambo (SACP) 
c8
Mwimbaji wa Sikinde, Abdallah Hemba akipokea kura za  nafasi ya Makamu Mwenyekiti aliyokuwa akiipigania na mwanamuziki wa Tabora Jazz, Ramadhani Kitenge.
c9
Katibu Mkuu wa Chamudata ambaye pia ni meneja wa Msondo Ngoma, Said Kibiriti (kulia) akaiwa Hassan Msumari aliyekuwa akitetea kiti chake.c10
Luizer Mbutu aliwashinda kwa mbali wapinzani wake Mwinjuma Muumini (Aliyeshika nafasi ya pili) na Said Kaunga.
c11
Luizer Mbutu akiwa Mwinjuma Muumini (kulia) na Said Kaunga.
c12

c13
Uchaguzi uliendeshwa kwa usimamizi makini wa Mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi, Kamanda Mstaafu Jamal Rwambo (SACP) 
c14
Wajumbe wa kamati ya Utendaji ya Basata toka kushoto: Abbu Omar Abubabar, Cecy Jeremiah Lugome, Bernedict Berno Sanga, Saidi Abdillahi Mdoe, Gabriel Byabato Bakilana, Rhobi Abubakari Chacha
c15
MAKAMU MWENYEKITI Abdallah Hamis Hemba
c16
Luizer Mbutu akipongezwa na Mwinjuma Muumini aliyeshika nafasi ya pili
c17
Katibu Mkuu Said Kibiriti
c18
Luizer Mbutu baada ya kutangazwa mshindi ambapo aliwashinda kwa mbali wapinzani wake Mwinjuma Muumini (Aliyeshika nafasi ya pili) na Said Kaunga.
c20
Luizer Mbutuakipongezwa na Said Kaunga aliyeshika nafasi ya tatu
c21
MWENYEKITI Luizer Morris Nyoni (kati),  MAKAMU MWENYEKITI
Abdallah Hamis Hemba (kushoto)  na KATIBU MKUU
Said Nassoro Kibiriti. Nyuma yao ni wajumbe wa kamati ya utendaji

c22
Kila aliyegombea aliitwa mbele kutia saini hati ya matokeo na kuyakubali

c23

c24

c25

c26

c27

c28

c29

c30

c31

c32

c33

c34

c35

c36

c37

c38
Mwakilishi wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) akiongea

c39

Mwakilishi wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo akiongea
c40

c41

c42

c43

c44

c45

c47

c48
Mwenyekiti wa Uchaguzi Kamanda wa Polisi Mstaafu Jamal Rwambow akihitimisha zoezi
c49
Dar Modern Taarab wakitumbuiza wajumbe baada ya uchaguzi
c50

 

Comment Using!!

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad