JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


SHIRIKA LA NDEGE LA ETIHAD LAPOKEA TUZO YA KIMATAIFA BAADA YA KUJIUNGA NA MPANGO WA KUPATA FEDHA.

Share This

MAKATABA wenya thamani ya dola za kimarekani milioni $700m uliosainiwa na washirika wa ndege ya Etihad kwa ajili ya upanuzi wa shirika hilo umetambuliwa na shirika lenye sifa duniani katika nyanja ya masuala ya kifedha na uchumi la “International Financing Review (IFR)” na hivyo kuitunuku shirika la ndege la Etihad na tuzo maalum. 

Mkataba huo wa miaka mitano ulitambulika kama dhamana kubwa kabisa ya mwaka iliyosainiwa kutoka barana ulaya, mashariki ya kati na Afrika, katika hafla iliyofanyika jijini London Januari 27

Mwezi Septemba , shirika la ndege la ndege la Etihad lilianza safari ya maonyesho, likiongozwa na mshauri mkuu, Goldman Sachs, katika bidi za kuongeza thamani ya hisa za Shirika hilo, kampuni yake tanzu ya huduma za viwanja vya ndege ya Etihad na washirika wengina wake watano wa huduma za angani – airberlin, Air Serbia, Air Seychelles, Alitalia na Jet Airways – wote wakiwa ndani ya shirika la ndege la Etihad.

Kupitia michango ya washirika wa ndege ya Etihad BV, kikundi kilifanikiwa kupata dola za kimarekani milioni 500, kiasi hicho kiliongezeka kwa kiasi cha dola za kimarekani milioni 200 ndani ya siku chache tu kufuatia kuongezeka kwa shauku kutoka jamii ya fedha ya kimataifa.

Ikiwa kama mkataba wakifedha wa kipekee katika sekta ya masuala ya anga, hii ni mara ya pili ndani ya wiki chache kwa shirika hili la ndege kutambulika na kupata tuzo kupitia mkataba wake huo. Washirika wa ndege la Etihad walipokea tuzo ya mkataba wa kifedha wa mwaka kutoka mashariki ya kati, katika hafla iliyofanyoka jijini London kupitia Makala ya Global Transport Finance ya nchini UK.

James Hogan, Rais na Afisa Mtendaji Mkuu wa shirika la Ndege la Etihad, alisema: “Uvumbuzi ndio msingi wa uendeshaji wa biashara zetu katika shirika hili. Tuzo hii kutoka “International Financing Review” inaonyesha dhahiri ni jinsi gani taasisi za kifedha zina uamini juu ya mafanikio yetu pamoja na mifumo yetu ya kibiashara katika kuunganisha biashara zetu zite tulizo wekeza” 

Akiongezea Bw Hogan, alisema: “Katika sekta ya biashara yenye ushindani mkubwa, siri ni kukuza uzalishaji pamoja na kuongeza ufanisi ili kukuza biashara. Kwa upande wa wahirika, kila mmoja wao ni kujikuza kibiashara. Ila kwa pamoja, nguvu inajumuishwa kwa pamoja. Mfumo huu wa uelewano ndio unatambua na kuidhinisha nguvu ya shirika zima. 

“Ningependa kumshukuru na kumpongeza afisa wetu mkuu wa masuala ya kifedha, Bw James Rigney, na timu yake nzima kwa juhudi zao za hali ya juu katika kuunda mfumo thabiti uliokuwa kivuto katika masoko ya ndani na nje ya nchi. Walifanya kazi kwa bidii sana kuleta shauku kubwa juu ya mifumo yetu ya kibiashara na tunayo furaha kuona bidi zao zikizaa matunda na kupata tuzo hizi, hasahasa wakati huu ambapo masoko mengi duniani yamejaa mashaka na wasiswasi juu ya kuwekeza fedha kutokana na changamoto za kiuchumi duniani”. 

Mkurugenzi mtendaji wa Goldman Sachs, Bw. Martin Weber, alisema: “ Tunafuraha kubwa kufanya kazi pamoja na washirika wa ndege ya Etihad katika kuwapatia dhamana hii kubwa na tunapongeza timu iliyohusika katika ushindi wa tuzo ya IFR. Mafanikio haya yanatokana na uongozi wa shirika la ndege la Etihad kukutana na wawekezaji mbalimbali dunia nzima, na hivyo kufanikisha kukamilisha mkataba huu. Hii pia ni ishara ya jinsi gani mfumo wao wa kibiashara ua nguvu ya kufurahisha masoko hata katika kipindi hichi kigumu cha masoko ya dunia” 

Safari za kuchangia fedha zilifanyyika Abu Dhabi, Dubai na London zikiwa zinasimamiwa na washauri wakuu Goldman Sachs, kampuni kutoka Abu Dhabi ya ADS Securities na Anoa Capital. Fedha zilizopatikana ziligawanywa katika Nyanja saba tofauti, ikiwa mchanganyiko wa matumizi ya mtaji na uwekezaji katika ndege, pamoja na kujazia fedha kulingana na mahitaji ya vitengo mbalimbali vya shirika hili la ndege ya Etihad. 

International Financing Review ndio chombo kinachoongoza duniani katika kutoa uchambuzi wa kina juu ya masoko, ikitoa ushauri na uchambuzi wa kina juu ya uwekezaji wa masuala ya kibenki kwa kauu wa benki duniani, pia hutoa habari juu ya masoko ya kibiashara kupitia Makala zake za kila wiki ma ripoti zao za kila siku mtandaoni

Uongozi wa shirika la ndege la Etihad ulisifiwa na IFR kwa kukamilisha na kufanikisha uchangishaji fedha, huku wakijenga uaminifu na kuungwa mkono na wawekezaji. 


Tukio hilo kubwa kabisa katika kalenda ya wawekezaji masoko wa dunia kila mwaka, litavutia wawekezaji wakubwa na wenye mafanikio zaidi ya 1,000 mwezi ujao jijini London ili kusherekea tuzo za IFA za kila mwaka.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad