JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


MKUU WA WILAYA YA RUANGWA MKOA WA LINDI,MARIAM MTINA ATOA MACHOZI WAKATI WA KUPOKEA MSAADA MASHINE TOKA VODACOM FOUNDATION

Share This
 Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa Mkoa wa Lindi,Mariam Mtina(wasita toka kushoto)akimsikiliza kwa umakini Muuguzi Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya hiyo, Omary Rajabu(kulia)alipokuwa akiwaelezea baadhi ya wafanyakazi wa Vodacom Tanzania,Wauguzi wa hospitali hiyo na wananchi jinsi mashine inayofyonza uchafu(Electrical Suction machine) kwa watoto waliozaliwa kabla ya wakati”Njiti” Zaidi ya shilingi Milioni 6/- zilitumika katika kunua vifaa hivyo na kutolewa msaada na Vodacom Foundation kupitia taasisi inayojishughulisha na watoto hao ya Doris Mollel. 
 Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa Mkoa wa Lindi,Mariam Mtina(wapili toka kushoto)pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Vodacom Tanzania, Wauguzi wa hospitali hiyo na wananchi wakimsikiliza Mganga Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa,Dkt Japhet Simeo(kushoto)akiwaelimisha jinsi mashine ya Oxygen inavyosaidia watoto waliozaliwa kabla ya wakati”Njiti” kupumua wakati wa hafla fupi ya makabidhiano ya msaada wa mashine hizo zilizogharimu zaidi ya shilingi milioni 6/- na kukabidhiwa na Vodacom Foundation kupitia taasisi inayojishughulisha na watoto hao ya Doris Mollel.
 Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa Mkoa wa Lindi,Mariam Mtina(katikati)akitoa shukurani kwa niaba ya wananchi wake kwa Meneja wa Vodacom Foundation,Sandra Oswald na Mwanzilishi wa taasisi ya Doris Mollel inayojishughulisha kusaidia watoto wanaozaliwa kabla ya wakati”Njiti”,Doris Mollel(kulia)kuhusiana na msaada wa mashine ya kupumulia na vifaa mbalimbali uliotolewa na Vodacom Foundation kupitia taasisi ya Doris Mollel vya kuwasaidia watoto hao wanaozaliwa katika wilaya hiyo.Vifaaa hivyo viligharimu zaidi ya shilingi milioni 6/-
 Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa Mkoa wa Lindi,Mariam Mtina(watatu toka kushoto)akipokea msaada wa mashine inayofyonza uchafu kwa watoto waliozaliwa kabla ya wakati”Njiti”kwa niaba ya wananchi wa wilaya hiyo toka kwa Meneja wa Vodacom Foundation, Sandra Oswald.Msaada huo uliotolewa na Vodacom Foundation kupitia taasisi ya Doris Mollel,Uliogharimu zaidi ya shilingi milioni 6/-
Baadhi ya wakazi wa Wilaya ya Ruangwa Mkoa wa Lindi,wakifurahia msaada wa mashine mbalimbali uliotolewa na Vodacom Foundation kupitia taasisi ya Doris Mollel inayojishughulisha kusaidia watoto wanaozaliwa kabla ya wakati”Njiti”Msaada huo ulikabidhiwa hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad