JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


DC ATOA WIKI MBILI WANAFUNZI WAENDE SHULE

Share This
Na Woinde Shizza 
Mkuu wa Wilaya ya SimanjiroMkoani Manyara, Mahmoud Kambona ameagizawanafunzi wote waliofaulu kujiunga nashule za sekondari wilayani  humo wawe wamewasili kwenye shule zao na kuanzamasomo baada ya wiki mbili.

Kambona alitoa agizo hilo juzialipokuwa anakagua shule ya Sekondari Msitu wa Tembo na kuzungumza na watendajiwa vijiji, kata, madiwani na maofisa Tarafa, kuhusiana na wanafunzi waliofaulukujiunga na masomo ya sekondari. Alisema wanafunzi wote waliofaulukujiunga na Sekondari wanatakiwa wafike kwenye shule zao baada ya muda wa wikimbili kwa ajili ya masomo na endapo wasipotekeleza hilo atawachukulia hatuakali viongozi wa eneo husika.


 “Nitawachukulia hatua
kali viongoziwote wakiwemo madiwani, maofisa tarafa, watendaji wa
kata, vijiji na wenyevitiwa vijiji wa sehemu husika ambao wanafunzi wote waliofaulu watakuwa hawajafikashuleni,” alisema Kambona.

Pia,
aliwaagiza wakuu wa shule zasekondari za wilaya hiyo kuwaelekeza
wazazi na walezi wa watoto ambao wamefaulukujiunga na shule zao, juu ya majukumu yao na majukumu ya serikali kuhusiana naelimu bure.Baadhi
ya wazazi wa wanafunziwaliofaulu Joseph Odoyo na Mustafa Seif walisema
dhana ya elimu bure ya RaisJohn Magufuli bado hawajaielewa kwani iliondolewa ni ada pekee ila chakula na mahitajimengine
wanachangia.

“Ada ya sh20,000 ndiyo pekee iliyofutwaila tunachangia huduma nyingine za mpishi sh.15,000 kuni sh15,000 kusaga na
kukoboash15,000 kulima shamba la shule sh.15,000 na viungo sh10,000 kwa muhula mmoja,”alisema Odoyo. Alisema pia wazazi wanatakiwa
kuchangiakilo 80 za mahindi, kilo 35 za maharage, kilo tano za sukari,
kilo 12 za mchelena lita tano za mafuta ya kula kwa muhula mmoja ila sh5,000 ya muhuri wa nemboya shule imetolewa.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad