JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


TANZAONE: MMEA WA ‘LOZERA’ HAUFAI KWA MATUMIZI YA BINADAMU

Share This
  Tabibu Gonzaga Marwa akiangalia baadhi ya mkopo ya Dawa jijini Dar es Salaam leo

TAASISI isiyo ya Kiserikali ya Tanzaone Herbal Clinic chini ya mradi wake wa ‘Tanzaone’ hatimaye imethibitisha pasipo shaka kuwa mmea ujulikanao kama Lozera na bidhaa zitokanazo na mmea huo hazifai kwa matumizi ya binadamu na wanyama.

Akizungumza na waandishi wa habari, sanjari na kuonyesha majibu ya vipimo vya kitaalamu kutoka Wakala wa Maabara ya Ofisi ya Mkemia Mkuu wa serikali kupitia utafiti uliofanywa chini ya mradi huo, Mratibu wa mradi.

 Tabibu Gonzaga Marwa, amesema  matokeo ya uchunguzi wa sampuli za mmea huo yameonesha una ukuvi yaani ‘fangasi’ aina ya Aspergillus ambao hutoa sumu ya Aflatoxin ambayo huweza kusababisha saratani ya maini.

Aidha, Tabibu Marwa ameiomba serikali kupitia Wizara ya Afya, na Mamlaka ya Chakula na Dawa TFDA, kuhakikisha wanachukua hatua za haraka kunusuru afya za walaji, sambamba na kushauri wadau wa tiba asili nchini kufanya utafiti wa kina wa dawa za mitishamba na bidhaa zake kabla ya kumfikia mlaji.

Hati ya uchunguzi ya Mradi huo, namba 241/2013, uliopewa jina la ‘Tanzaone Red Tea Juice’ na kudumu kwa miaka mitatu 2010/2013, kwa kushirikisha watuamiaji wakubwa wa Lozera zaidi ya 250 nchini kote, ilichunguzwa, kuidhinishwa na kuthibitishwa na Mkemia Mkuu wa Serikali

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad