Wakulima wa Korosho wa Kilwa Masoko wakiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa NSSF baada ya kumalizika kwa Semina.
Afisa Ushirika wa Vyama vya Wakulima (AMCOS) Bwana Vincent Mhengilolo akizungumza na Wenyeviti na Makatibu wa Vyama vya Ushirika wakati wa Semina iliyoandaliwa na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii(NSSF).
Mkulima wa Korosho wa Kilwa Masoko akiuliza swali ili kupata ufafanuzi kuhusu Mpango wa Hifadhi ya Jamii kwa Wakulima Mjini Kilwa Masoko.
SHIRIKA la Taifa la Hifadhi yaJamii(NSSF) limetoa Elimu kwa Wenyeviti na Makatibu wa Wakulima wa Korosho na Ufuta wa Wilaya ya Kilwa Mkoa wa Lindi kuhusu mpango wa Hifadhi ya Jamii kwa Wakulima, Mpango huo unamwezesha mkulima kupata mikopo mbalimbali ikiwemo mkopo wa vifaa vya kilimo pamoja na pembejeo za kilimo.
SHIRIKA la Taifa la Hifadhi yaJamii(NSSF) limetoa Elimu kwa Wenyeviti na Makatibu wa Wakulima wa Korosho na Ufuta wa Wilaya ya Kilwa Mkoa wa Lindi kuhusu mpango wa Hifadhi ya Jamii kwa Wakulima, Mpango huo unamwezesha mkulima kupata mikopo mbalimbali ikiwemo mkopo wa vifaa vya kilimo pamoja na pembejeo za kilimo.
Aidha
mpango huo unamwezesha mkulima na familia yake kufaidika na mafao
mbalimbali yatolewayo na NSSF yakiwemo mafao ya matibabu ambapo mkulima
atapata matibabu bure yeye na familia yake.
Afisa Mafao wa Shirika la Taifa la Hfadhi ya Jamii NSSF Bi Lydia Ignas akitoa ufafanuzi kuhuhu mafao mbalimbali yatolewayo na NSSF.
Meneja wa NSSF Mkoa wa Lindi Bi Nour Azin akizungumza na Wenyeviti na Makatibu wa Vyama vya Wakulima kuhusu mpango wa Hifadhi ya Jamii kwa Wakulima katika semina iliyofanyika Kilwa Masoko Mkoani Lindi.
Ofisa Mafao wa NSSF, Kabonwa Kandoro akiwaandikisha uanachama Wenyeviti na Makatibu wa vyama vya wakulima AMCOS baada ya semina iliyofanyika Kilwa Masoko mkoani Lindi.
No comments:
Post a Comment