Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Golden Fleet LTD na Golden Coach LTD Bw. Mohamed Raza Dewji (kulia) akimkabidhi Afisa Uuguzi wa Idara ya Uuguzi na Ubora wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Bi. Mariana Makanda msaada wa vitanda thelasini na magodoro thelasini, katikati ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Umma na Huduma kwa Wateja wa hospitali hiyo Bw. Aminiel Eligaesha.
Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Golden Fleet LTD na Golden Coach LTD Bw. Mohamed Raza Dewji (kulia) akieleza kwa waandishi wa habari jinsi alivyoguswa na tatizo la wagonjwa kulala chini mara baada ya Rais John Magufuli alipotembea hospitali hiyo.
Daktari akimpatia huduma mgonjwa kwa kutumia mashine ya MRI ambayo ilikuwa mbovu kwa muda mrefu ila imetengamaa mara baada ya Rais John Magufuli kufanya ziara katika Hospitali ya Taifa Muhimbili na kuagiza matengenezo ya haraka yafanyike.
Madaktari wakifuatilia kwa makini jinsi mashine ya MRI inavyofanyakazi mapema hii leo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Picha zote na Eliphace Marwa - MAELEZO.
No comments:
Post a Comment