JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


DK. KIMEI AONGOZA HARAMBEE YA UJENZI WA KANISA LA KKKT USHARIKA WA SIHA MKOANI KILIMANJARO

Share This
  Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei akizungumza wakati wa ibada maalum iliyofanyika katika Kanisa la KKKT Usharika wa Siha Sango Mkoani Kilimanjaro. Ibada hiyo ilikwenda sambamba na harambee ya kuchangia ujenzi wa kanisa hilo ambapo zaidi ya shs Milioni 100 zilipatikana.
Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Kiijili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Cuthbert Temba akiongoza ibada.
 Waumini wa Kanisa hilo wakiwa katiba ibada.


  Katibu Mkuu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani, Goodfrey Nkini na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei wakiwa kanisani na Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB, Huduma Shirikishi, Esther Kitoka.
Mkurugenzi Benki ya CRDB tawi la Moshi, Francis Mollel (kulia) akipokea mbuzi kutoka kwa Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Siha Sango, Cuthbert Temba (wa pili kushoto) baada ya kununua mbuzi kwa shs 100,000 katika harambee ya  kuchangia ujenzi wa Kanisa la KKKT Usharika wa Siha Sango lililopo Mkoa wa Kilimanjaro. Wa pili kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei  akimkabidhi mbuzi Mchungaji Emmanuel Kileo baada ya wakati wa harambee ya kuchangia ujenzi wa Kanisa hilo. Kushoto ni Solomon Nkini.
 Katibu Mkuu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani, Goodfrey Nkini akipokea mbuzi baada ya kumnunua katika harambee ya ujenzi wa Kanisa la KKKT Usharika wa Siha.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad