JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


WAANGALIZI WA UCHAGUZI KUTOKA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI KUWASILI KESHO

Share This

EAST AFRICAN COMMUNITY



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

KUNDI la waangalizi wa uchaguzi Mkuu nchini Tanzania unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, mwaka huu kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki, wanatarajia kuwasili Dar es Salaam Jumapili, tarehe 18 October  2015 tayari kwa uangalizi wa uchaguzi kwa upande wa Tanzania Bara na Visiwani.

Kuwasili kwa kundi la Jumuiya ya Afrika Mashariki lenye takribani watu hamsini na tano, ni kuitikia mwaliko kutoka kwa Tume ya Uchaguzi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na pia kufuata Maazimio ya Baraza la Mawazili la Jumuiya ya Afrika Mashariki juu ya uangalizi wa uchaguzi kwa nchi Wanachama wa Jumuiya.

Kazi ya wasimamizi wa uchaguzi kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki itakuwa ni kuangalia kwa ujumla wake mazingira ya uchaguzi na kutathmini kwa kina mchakato wa uchaguzi nchini kote kabla, kipindi cha uchaguzi na baada ya siku ya uchaguzi.

Kundi la waangalizi wa uchaguzi kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki litaongozwa na aliyekuwa Makamu wa Rais wa Kenya, Mh. Awori Arthur Athansius Moody.

Kundi waangalizi wa uchaguzi kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki litatangaza uwepowake inchini Tanzania kwenye mkutano na Waandishi wa Habari utakaofanyika Jumatatu, tarehe 19, October 2015, saa mbili na dakika thelathini (8.30am) asubui, New Africa Hotel, Dar es Salaam.

·         NINI KITAFANYIKA- Kutoa taarifa ya kuwasili kwa waangalizi wa uchaguzi kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki


·         WAPI- New Africa Hotel, Dar es Salaam


·         LINI- Tarehe 19th October 2015 from 8.30 am -10.30am
  
Ndugu   Muandishi wa Habari, unaombwa kuthibitisha uwepo wako kwenye mkutano huu kupitia anuani zifutazo hapa chini;

Owora Richard Othieno,
Press and Protocol Coordinator
EAC Election Observer Mission
New Africa Hotel

Dar es Salaam, Tanzania
Tel: +255 784 835021; 



No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad