JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


GOJU RYU KARATE-DO JUNDOKAN SEMINA UINGEREZA IMEFANA SANA!!

Share This
 SenSei Rumadha Fundi, amesimama mbele ya bendera ya Tanzania.
 Wakicheza Kata ya kundi kwa pamoja "Shisochin Kata"
Wakuu matawi nchi shiriki.
Kundi la wawakilishi sita wa nchi za Ulaya.

 Gasshuku au semina ya Karate mtindo wa Okinawa Goju Ryu
Jundokan So Honbu, imefungwa Jumapili usiku na kufuatiwa kwa
 tafrija kubwa ya kuwaaga washiriki "Sayonara Party" wa kike
 na kiume, umri kuanzia miaka 13 had 70 toka nchi mbalimbali
 za Ulaya na Japan ikiwemo na Tanzania iliyowakilishwa na
 sensei Rumadha. Viongozi wa Karate wa nchi zilizoshiriki ni:
 sensei Rene Ramanitrandrasana 9 Dan  wa Ufaransa,
 Sensei Antoine, Ufaransa 5 Dan, Sensei Bob Honiball 8 Dan
 Uingereza, Sensei Tony  Green 8 Dan , Uingereza, Sensei
 Jenni 5 Dan, Uingereza,  Sensei Ilpo, Sweden, 7 Dan,
 Sensei Caideiro 5 Dan, Ureno, Sensei Dr. Freidrich Gsodam 9
 Dan, Austria.

 Hii ilikuwa ni semina kubwa ya kipekee kufanyika 
 Uingereza na wakuu wake wa tano kushiriki toka visiwa vya
 Okinawa; walio ongozwa na mwenyekiti wa sasa wa mtindo huo
 Sensei Yoshihiro Miyazato, Kancho.

 Mbinu na matumizi yake ya kujihami kutumia sanaa ya Karate
 pamoja na ubora wa kata zilifanyiwa mazoezi sana katika
 semina hiyo. Kuzingatia nidhamu na utamaduni wa jadi wa
 Karate na kuheshimu desturi zake halisi, viongelewa
 katika  mfumo huo wa Goju Ryu Karate. Kwa ujuml, semina
 hiyo iliwakutanisha  washiriki  wapatao  120,

 wakiwemo na watoto wa umri wa kuanzia miaka 13 had 17.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad