JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


READ INTERNATIONAL KUJENGA MAKTABA ZA SEKONDARI NYINGI ZAIDI NCHINI

Share This
  Muasisi wa Shirika lisilo la kiserikali la READ International, Rob Wilson (katikati) akizungumza katikasherehe za miaka 10 ya shirika hilo jijini Dar es Salaam. Wengine ni baadhi ya wanachama wa shirika hilo la kujitolea nchini Tanzania. READ International inatimiza miaka 10 tokea kuanzishwa ikisihirikiana na Realising Education for Development pamoja na wahisani wengine imeweza kusaidia ujenzi wa maktaba 72 na kutoa vitabu zaidi ya milioni 1.4 nchini kote.
 Mjumbe wa Bodi ya READ International, Faraja Kotta Nyalandu (kulia), mwanzilishi wa READ, Tom Wilson (wa pili kushoto) pamoja na baadhi ya wanafunzi wa shule ya sekondari Makumbusho ya jijini Dar es Salaam wakikata keki kusherehekea miaka 10 ya shirika hilo.
  Muasisi wa Shirika lisilo la kiserikali la READ International, Rob Wilson (kulia) akizungumza na baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari Makumbusho alipotembelea maktaba ya shule hiyo iliyowezeshwa kwa ufadhili wa shirika hilo kwa kushirikiana na Realising Education for Developmentpamoja na wahisani  wengine. READ International inatimiza miaka 10 tokea kuanzishwa huku ikisaidia ujenzi wa maktaba 72 na kutoa vitabu zaidi ya milioni 1.4 nchini kote. Wengine pichani ni baadhi ya walimu wa shule hiyo.
 Mmoja wa wanachama wa kujitolea wa READ, Amani Alphonce Shayo akizungumza katika hafla hiyo jinsi mpango wa ukarabati wa maktaba ulivyoleta manufaa kwa wanafunzi wa kitanzania.  
  Mwenyekiti wa Bodi ya READ International, Hatima Karimjee akizungumza katika sherehe za miaka 10 ya shirika hilo.
 Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya inayojishughulisha na uchimbaji wa madini ya MANTRA, Frederick Kibodya akizungumza kuhusu ufadhili wao katika katika kuisaidia READ International kwa ushirikiano na Realising Education for Development katika kukabiliana na tatizo la uhaba wa nyenzo za elimu katika shule za sekondari nchini.
Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari Makumbusho ya jijini Dar es Salaam wakijisomea katika maktaba iliyowezeshwa na Shirika la READ International kwa kushirikiana na Realising Education for Development. READ International imetimiza miaka 10 tokea kuanzishwa ikisaidia ujenzi wa maktaba 72 na kutoa vitabu zaidi ya milioni 1.4 nchini kote.  
ILI kukabiliana na tatizo la miundombinu katika sekta ya elimu nchini inayozikabili shule nyingi sa sekondari,  Shirika lisilo la Kiserikali la READ International kwa kushirikiana na mpango wa Realising Education for Development limetangaza mpango wa kujenga zaidi ya maktaba 500 katika kipindi cha miaka 10 ijayo ili kuinua kiwango cha elimu nchini.

Akizungumza wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 10 tokea kuanzishwa kwa shirika hilo, Muasisi wake Rob Wilson alisema jijini Dar es Salaam juzi kuwa kupitia michango ya wafadhili wao pamoja na Realising Education for Development  wanaweza kujenga japo maktaba 50 kwa kila mwaka.

 “Katika kipindi cha miaka 10 tumefanikiwa kusidia vitabu milioni 1.4 na kujenga maktaba takrabani 72. Kwa msaada wa wadau wa elimu tumefika hapa, sasa tunakusudia kufanya vizuri zaidi katika miaka 10 ijayo,” alisema bwana Wilson.

.
Muasisi huyo alisema wanajivunia mchango wanaoupata kutoka kampuni mbalimbali na kuzitaja baadhi kama Bakhresa, Simba Cement, Wentworth, Mantra, Atlas Copco, na Songas na kusema ni matumaini taasisi nyingine kwa kuona mafanikio waliyoyapata watajitokeza na kuwaunga mkono.

“Ikiwa ni sehemu ya Mpango wa Ukarabati wa Maktaba wa READ kwa kushirikiana  na Realising Education for Development  na  wanachama wa shirika hili wa kujitolea hugeuza vyumba visivyotumika katika mashule na kuwa maktaba nzuri na kisha kuziwezesha kwa nyenzo muhimu kama vitabu, meza, viti na makabati,” aliongeza muasisi huyo.
  
Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa READ International nchini, Montse Pejuan  alisema licha ya ujenzi huo wa maktaba lakini pia wamesaidia kufundisha wakutubi na  kusaidia shule kufundisha walimu wao wa maktaba.

“Tunafanya bidii kujenga mpango mzuri utakaowawezesha wanafunzi kupenda kujisomea na hivyo kuwawezesha kufaulu vizuri masomo yao,” alisema.

Kwa upande wake msemaji wa Kampuni ya Simba Cement Bi.Mtanga Noor alisema kampuni yao imetumia takribani shs milioni 48 kusaidia ujenzi wa maktaba tatu jijini Dar es Salaam na kutoa wito kwa makampuni mengine kuisaidia juhudi za READ ili kuleta mabadiliko katika ubora wa elimu nchini.
  
Mbali ya Simba Cement wadhamini wengine ni Hogan Lovells, MeTL Group, Wizara ya Elimu na Mazunzo ya Ufundi, Radar Education Ltd, KPMG, IMMMA Advocates, Nabaki Afrika, Oyster bay Group, Learning InSync, MANTRA, Wentworth Foundation, Bakhresa Group, Songas, na BG Tanzania.

Wengine ni pamoja na Karimjee Jivanjee Foundation, Better World Books,  Veolia,  klabu za Rotary za Oysterbay na Bahari, Bakhresa Group, Hogan Lovells,  Corona, Atlas Copco,  Aidan Publishing na APENET. 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad