JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


MAKALA YA SHERIA: NJIA YA KISHERIA YA KUKUEPUSHA KUNUNUA ARDHI YENYE MGOGORO.

Share This
Na Bashir Yakub
Makala zilizopita  nilieleza   mambo au taarifa muhimu  zinazopaswa kuwa kwenye  mkataba wako  unapokuwa unanunua  nyumba/kiwanja. 
Nikasema  katika niliyosema  kuwa mkataba  lazima uoneshe  ukitokea mgogoro  utatatuliwa vipi,  ueleze kuwa  utapotokea mgogoro  muuzaji  lazima  awajibike kuhakikisha anakupa ushirikiano  mnunuzi  ili kumaliza  mgogoro huo na kuwa muuzaji  kama ana  mke  basi  mke wake ni lazima  aandaiiwe  nyaraka iitwayo  ridhaa ya mwanandoa ambayo  ni  tofauti  na mkataba  na  aisaini  pamoja na kuweka picha yake.  
Nilieleza  mengi  lakini hayo ni baadhi tu. Kwa wale ambao  hawakubahatika kuyasoma hayo basi  waandike neno "MAKALA  SHERIA"  kwenye google watapata makala  hizo. 
Leo  tena naeleza hatua  muhimu sana au ya lazima  na lazima haswaa  kwa mnunuzi wa kiwanja/nyumba  ambayo anatakiwa  apitie  kabla ya kufanya manunuzi.
Hatua hii kwa  jina la  kitaalam huitwa OFFICIAL  SEARCH  kwa lugha rahisi tu waweza kuiita  utafiti,upekuzi,  upembuzi au upelelezi rasmi  ambayo hufanywa na wanasheria. Mi napenda niite upelelezi. 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad