JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


TAMWA ZANZIBAR YAWANG'ARISHWA WAANDISHI CHIPUKIZI

Share This

 


Zanzibar: Najjat Omar.
CHAMA Cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania -Zanzibar – TAMWA-Z kimekutana na waandishi wa Habari chipukizi,wahariri,wamiliki wa vyombo vya Habari na wadau wa Habari kwa kuwatunuku na kuwatunza waandishi wa Habari 23 waliokuwa kwenye mradi wa Waandishi Chipukizi.

Mahafahali hayo yamefanyika katika Ukumbi wa Bima uliopo Maisara Mjini Magharib Unguja.

Khairat Haji ni Kaimu Afisa Programmu TAMWA -Zanzibar amesema katika hatua za kumarisha uongozi kwa wanawake ,mradi huu ambao hii ni awamu ya pili ambapo kwa awamu ya kwanza uliwafunza na kuwasimamia waandishi vijana 18 kwa 2022 .Huku mwaka 2023 waamdishi vijana 24 walipata fursa katika mradi huu wa Wamawake na Uongozi”Kupitia mradi huu ulikuwa unahitaji kazi 348 na hadi kufikia leo kazi hizo ni 347,huku magazeti 47 ,Makala za radio 117 huku Makala za mitandamo 187 ambazo zinakamilisha kazi 347” Amesema Khairat

Shifaa Said ni Jaji Kiongozi wa Tuzo za Waandishi wa Habari Chipukizi kwenye kuhariri kazi za waandishi hao 24 zilizofika kwao kazi hizo ambazo zimehaririwa kwa siku nne ,kazi hizo ambazo zilikuwa ni 175 kati ya hizo magazeti ni 15 za radio 85 na mitandao ya kijamii 75.Amesema “Vigezo muhimu vilivyozingatiwa kwenye kazi hizo ni Pamoja na weledi na umahiri katika sauti pamoja na sauti zizosikika huku upekee wa mada na kuangalia kuwafikia watu wenye mahitaji maalum” Amesema Shifaa Said.

Akiongeza kuwa “Mafanikio na ukuwaji wa wanufaika wa mradi huu kwa mwaka huu wameweza kuandika na kuchapisha Makala na vipindi vyema mabadiliko kwenye jamii” Amemaliza Shifaa Said.

Hawra Shamte ni Mjumbe wa Bodi ya Tamwa Zanzibar,amesema kuwa kuwepo kwa mahafali hii leo ambao wamepata nafasi ya kuwa kwenye huu kukubali kujifunza na kuandika masuala ya wanawake na hii ni “Dhahiri kuona kwamba majukumu yenu kwenye kuandika masuala ya wanawake na uongozi yametamalaki na ni hakika tuendelea kaundika na kuuhabarisha umma juu ya uwepo kwa habari hizi katika kuleta mabadiliko katika jamii hii ambayo inategemea kuwa na viongozi wanawake na wanaume.” Amesema Hawra.

Akiwa mmoja wa wanufaika kwa mradi huu Berema Suleiman Nassor ni mwandishi wa Zenji Fm pia ni mnufaika wa Mradi huu amesema kwenye uandishi wa Makala za wanawake na uongozi suala la upatikanaji wa data ni changamoto. Huku Nihifadhi Abdulla ambaye ni mwandishi wa Kati Fm amesema kuwa zamani alikuwa akiiandika Makala na Habari za kawaida ila sasa amebadilika “Sasa naandika habari zenye kuleta mabadiliko na usawa wa kijinsia kwanza sikuweza ila kwa sasa naona kwamba nimekuwa na naweza kupikwa vyema” Amemaliza.

Salma Said ni Mwandishi wa DW na Mhariri na amesema suala la kuona vijana wanakuwepo kwenye mradi huu ni kuonesha masuala ya uandishi wa Habari za viwango na wenye kuleta mabadiliko “Ikiwa haya yataendelea kuandikwa basi kutakuwepo na mabadiliko katika jamii kwenye uleta uwajibikaji ,kubadilishwa kwa sheria na haki kutendeka” Amesema Salma Said wakati akizungumza kwenye Mahafali hayo.

Issa Yussuf ni Mwandishi wa Gazeti la Daily News amesisitiza matumizi ya lugha ni muhimu sana kwenye uandishi wa Habari “Masuala ya lugha kwa usahihi na usanifu ni jambo ambalo litawafikisha mbali na kuwasaidia zaidi kwenye uandishi wa kujifunza na kusoma masuala ya mikataba na sheria mbali mbali.” Amesema Issa.

Akitoa Tuzo na kwa waandishi hao Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania -Zanzibar TAMWA -Zanzibar.Dkt Mzuri Issa amesema “Kuwa makala hizi kazi hizi zimeleta mabadiliko kwenye jamii kwa kuwashawishi wanawake kuingia kwenye siasa na kupata nguvu ya kusaidia kuvunja dhana potofu kwenye ya kuwa wanawake hawezi kuwa viongozi kuwa kwenye uongozi.” Amemaliza.

Mradi huu wa wanawake na Uongozi uliotekelezwa na TAMWA Zanzibar kwa kushirikiana na shirika la National Endowment for Democracy (NED) wa kuwawezesha waandishi wa habari vijana YMF kuandika habari za wanawake na uongozi umewashirikisha waandishi vijana ishirini na nne (24) kutoka Unguja na Pemba.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad