JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


Mwenyekiti wa Wazazi CCM Morogoro Asaidia Waathirika wa Mafuriko Mlimba

Share This

 

Wanafunzi wa St Mary’s Ifakara wakimkabidhi msaada wa tani tano za chakula Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, Dunstan Kyoba uliotolewa na Mwenyekiti wa CCM Wazazi Mkoa wa Morogo (Kulia) Dkt. Rose Rwakatare.

Mwenyekiti wa Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dkt. Rose Rwakatale (aliyevaa nguo ya bluu) akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, Dunstan Kyoba msaada wa tani tano za vyakula kwa ajili ya waathirika wa mafuriko wa Jimbo la Mlimba mkoani.Hafla ya makabidhiano hayo imefanyika leo Aprili 22,2024 kwenye ofisi za Mkuu wa Wilaya.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Ifakara, Zahra Michuzi akiwa na wanafunzi wa shule ya St Mary’s mara baada ya kukabidhiwa msaada wa mchele kwa waathirika wa mafuriko Mlimba mkoani Morogoro leo Aprili 22,2024
Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, Dunstan Kyoba akiwa na wanafunzi wa shule ya msingi  St. Marys Mlrogoro baada ya kupokea msaada huo wa chakula kwa ajili ya waathirika wa mafuriko jimbo la Mlimba leo Aprili 22,2024.
Na Mwandishi Wetu
MWENYEKITI wa Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dkt. Rose Rwakatare ametoa msaada wa tani tano za mchele kwa waathirika wa mafuriko wa jimbo la Mlimba mkoani Morogoro.

Dkt. Rose amekabidhi msaada huo leo Aprili 22, 2024 kwa Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, Dunstan Kyoba katika hafla ambayo imefanyika ofisini kwake.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi msaada huo, Dkt. Rose amesema amezaliwa Mlimba hivyo ameguswa sana kuona wananchi wenzake wanaishi maisha ya shida....“Mimi ni mzaliwa wa Mlimba, kwa hiyo hapa ni nyumbani kwangu ndiyo maana nimeamua kuja kulia na wanaolia, tufarijiane wakati huu mgumu, sijaja bure nimekuja na mifuko 1,000 ya mchele angalau wapate chakula,” amesema

Aidha amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutuma ujumbe kupeleka msaada wa vitu mbalimbali na kuwaomba wadau mbalimbaali waendelee kupeleka msaada.

“Hata ukiwa na mfuko mmoja wa mchele, unga unakaaribishwa kuja kusaidia watanzania wenzako, sisi ni watanzania na tunajulikana dunia nzima kwa upendo,” amesema.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, Dunstan Kyoba amemshukuru Dkt. Rose Rwakatare kwa upendo aliouonyesha kwa wakazi wa Mlimba na kuwaomba wadau wengine kuiga mfano huo na kwenda kutoa misaada.

Amesema msaada huo umekuja wakati mwafaka kwani wananchi wa maeneo yaliyoathirika na mafuriko wanahitaji faraja na kushikwa mkono wakati huu.

“Napenda kutoa wito kwa viongozi wengine na wafanyabiashara waige mfano wa Dkt. Rwakatare waje kusaidia wananchi ambao wako kwenye wakati mgumu wakati huu,” amesema

Naye, Mohamed Msuya, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kilombero amempongeza Dkt. Rose kwa msaada alioutoa kwa wananchi hao na kusema kuwa msaada huo ni wa kuigwa na wa mfano kwa wananchi wa wilaya ya Kilombero bila kujali itikadi za kisiasa.

“Tumpongeze sana Dkt. Rose kwa kuwa na maono ya kuwasaidia wananchi wa Kilombero, kutoa ni moyo wala siyo utajiri kwasababu kuna watu wana vingi lakini hawana moyo wa kutoa,” amesema

“Nawaomba sana watanzania wote bila kujali itikadi kujitokeza kuwasaidia wananchi wa Jimbo la Mlimba waliopata shida ya mafuriko na tutampa ushirikiano wa kutosha yeyote atakayeleta msaada,” amesema

“Dkt Rose Rwakatare ni mfano wa kuigwa kwa wananchi wa Wilaya ya Kilombero, huyu ana moyo wa kipekee kwasababu kila linapotokea tatizo amekuwa msaada mkubwa kwenye Wilaya ya Kilombero,” amesema Msuya

Amesema kuna watu wanataka kutoa msaada lakini wanaogopa kutokana na sababu za kisiasa hivyo amewatoa hofu kwamba wajitokeze kusaidia kwani CCM na Serikali zitawalinda kwa kuwa siasa ni mpaka 2025.

“Kwa sasa hakuna siasa hapa tunaamini tuna madiwani na wabunge lakini tuko kwenye utendaji hatuko kwenye siasa kwa hiyo Dkt. Rose najua una marafiki huko mjini, wewe ni Mwenyekiti wa Wazazi CCM mkoa wa Morogoro, unawadau wengi tunajua unauwezo wa kuhamasisha wananchi wakaja kuleta misaada,” ameongeza

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad