JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


MIAKA 61 YA UHURU NA ONGEZEKO LA WATANZANIA MILIONI 61

Share This


Mkuu wa wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani Nickson Simon (kushoto), Katibu Tawala wa Wilaya hiyo Mwanana Msumi (katikati) na Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Kisarawe(kulia) wakiwa wameshika keki kama ishara ya kuadhimisha miaka 61 ya Uhuru wa nchi yetu.Keki hiyo ilikatwa na kulishwa viongozi mbalimbali pamoja wananchi walioshiriki kwenye Mdahalo ulioandaliwa na Mkuu wa Wilaya kwa ajili ya kujadili masuala mbalimbali.


Kamanda wa Polisi Wilaya ya Kisarawe Eva Stesheni(kushoto) akiweka vijiti kwenye vipande vya keki.Katikati ni Mkuu wa wilaya hiyo Simon Nickson akitoa maelezo kuhusu keki hiyo na kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Kisarawe Zuberi Kizwezwe.

Mkuu wa wilaya ya Kisarawe Nickson Simon(kushoto) akimlisha keki Katibu Tawala wa wilaya hiyo Mwanana Msumi(kulia) kama ishara ya kusherehekea na kuadhimisha miaka 61 ya Uhuru wa Tanganyika.Tukio hilo la kukata keki limefanyika baada ya kumalizika kwa mdahalo ulioandaliwa na Mkuu wa wilaya hiyo kwa ajili ya kujadili masuala mbalimbali wakati wakiadhimisha siku hiyo.

Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Nickson Simon(kushoto) akimlisha keki Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya hiyo Zeuberi Kizwezwe.Kisarawe imeadhimisha siku ya Uhuru kwa kufanya shughuli mbalimbali za kijamii kuanzia Desemba 1 na leo Desemba 9 wamehitimisha kwa kufanya mdahalo ngazi ya wilaya.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani Zuberi Kizwezwe akizungumza wakati wa Mdahalo uliondaliwa na Mkuu wa Wilaya hiyo kwa ajili ya kujadili masuala mbalimbali ya kiutamaduni wakati Taifa likiadhimisha miaka 61 ya uhuru wake

Ofisa Ustawi wa Jamii katika Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani Mwandili Rangi akitoa ufafanuzi kuhusu hali ya mahusiano ya kwenye ndoa ndani ya Wilaua hiyo wakati wa mada ya kuzungumzia mahusiano na unyanyasaji wa kijinsia.Wengine kwenye picha hiyo ni Mkuu wa wilaya hiyo Nickson Simon(katikati) na Kamanda wa Polisi Eva Stesheni (kulia).


Baadhi ya washiriki wa mdahalo uliondaliwa na Mkuu wa wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani Simon Nickson ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha miaka 61 ya Uhuru wan chi yetu ambapo kwenye mdahalo mada mbalimbali zilijadiliwa.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad