Mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete ametembelea ofisi
za Mamlaka ya majisafi na usafi wa mazingira Dar es salaam (DAWASA)
Mkoa kazi wa kihuduma Chalinze kwa lengo la kujenga ushirikiano zaidi na
kujua mipango iliyopo ya huduma ya maji kupitia miradi mbalimbali
inayoendelea kutekelezwa katika Mji wa Chalinze.
Ridhiwani
amebainisha kuwa lengo la ziara yake ni kuishukuru DAWASA kwa kuendelea
kutatua changamoto za Majisafi katika jimbo lake na pia kujua mipango
ya sasa na ya baadae ya upatikanaji wa Majisafi kwa wananchi wasiofikiwa
na huduma hiyo.
"DAWASA
ni wadau wakubwa katika kutoa huduma ya majisafi kwa wananchi wa jimbo
langu. Hivyo baada ya uchaguzi kuisha nimeona ni vizuri kuwatembelea na
kuwasikiliza mipango mbalimbali waliyo nayo na wanayoendelea kuitekeleza
katika mji wa Chalinze" alisema Ridhiwani
Ridhiwani
alitumia nafasi hiyo kuiomba DAWASA kuharakisha ukamilishaji wa mradi
wa Maji wa Mlandizi -Chalinze -Mboga pamoja na mradi wa maji Chalinze
awamu ya tatu kwa haraka zaidi ili wananchi waondokane na kero ya maji .
Kwa
upande wake, Meneja wa Dawasa Mkoa wa kihuduma Chalinze, Mhandisi
Honest Makoi, ameeleza kuwa huduma ya maji kwa mji wa Chalinze kwa sasa
ni nzuri na Mamlaka imepeleka huduma ya maji kwenye vitongoji sita
ambavyo havikuwa na huduma.
Amebainisha
kuwa kazi iliyofanyika kwenye vitongoji hivyo ni ujenzi wa viosk vya
kuchota maji 114 katika Vijiji na vitongoji Visakazi, Mwidu, Gwata,
changarikwa kwaruhombo na Kifuleta halmashauri ya Chalinze.
Kazi
tunayoendelea nayo kwa sasa ni kufanya marekebisho ya mtandao wa maji
tuweze kupeleka huduma ya maji katika Vijiji vya Tukamisasa, Kaloleni
na Lulenge. Kazi hiyo inaendelea na wananchi watapata huduma ya maji"
alisema Mhandisi Makoi
Ridhiwani
aliipongeza Dawasa kwa kazi kubwa na nzuri inayoendelea kufanyika na
kuahidi ushirikiano mkubwa baina yao ili dhamira ya kumtua mama ndoo ya
maji kichwani ifanikiwe.
Meneja wa Dawasa Mkoa wa kihuduma Chalinze, Mhandisi Honest Makoi akitoa maelezo kwa Mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete mara baada ya kutembelea ofisi za Mamlaka ya majisafi na usafi wa mazingira Dar es salaam (DAWASA) Mkoa kazi wa kihuduma Chalinze.
Wafanyakazi wa Mamlaka ya majisafi na usafi wa mazingira Dar es salaam (DAWASA) Mkoa kazi wa kihuduma Chalinze.
No comments:
Post a Comment