JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


KAMPUNI YA AIRTEL KUZINDUA MSIMU WA AIRTEL RISING STAR JUNI 26 JIJINI DAR ES SALAAM.

Share This
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
KAMPUNI  ya Simu ya Airtel imeweka mikakati ya kuinua soka la vijana kwa kuweka wazi hatua yao ya kuzindua msimu wa sita wa Airtel Rising Stars utakaofanyika Juni 26 mwaka huu huku akiwataka wadau kujitokeza ili kuweza kuinua soka la vijana.

Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel, Beatrice Singano amesema kuwa msimu huu wa sita utakuwa na mabadiliko makubwa sana kwani kwa sasa wanamikakati mikubwa ya kuinua soka la vijana hasa baada ya kuona timu ya vijana ya chini ya miaka 17 Serengeti Boys kufanya vizuri kwenye michezo waliyocheza ya kirafiki pamoja na mashindano ya AIFF yaliyofanyika nchini India na kufanikiwa kushika nafasi ya tatu.

Naye Kocha Mkuu wa  timu hiyo Bakari Shime amesema kuwa hiyo ni hatua nzuri sana kwa Kampuni ya Airtel kuendelea kusapoti michezo hususani kwa vijana kwani ni moja ya msingi mzuri wa kuinua michezo pamoja na kuwjenga wachezaji wakiwaangali wadogo

  Mkufunzi wa soka la vijana Nchini Kim Poulsen amewashikiri Airtel kwani katika mashindano hayo anaeweza kupata wachezaji wazuri ambao watawajenga na kuleta ushindani wa soka baaadae.
 Mkurugenzi wa Mawasiliano Airtel, Beatrice Singano akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani katika uzinduzi wa sita wa Airtel Rising Stars utakaofanyika Juni 26 mwaka huu pamoja na kuweka mikakati katika kusaidia kuinua soka la vijana Nchini na kuwataka makampuni kujitokeza kuwekeza soka la vijana.
Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17 Serengeti Boys akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani katika uzinduzi wa sita wa Airtel Rising Stars utakaofanyika Juni 26 mwaka huu huku akizungumzia maandalizi ya kikosi chake kueleka mchezo wao dhidi ya Timu ya Taifa ya Visiwa vya Shelisheli siku ya Jumapili  kuwania kufuzu kucheza Mataifa Afrika nchini Madagascar  2017.
 Mkufunzi wa soka la vijana nchini Mholanzi, Kim Poulsen akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani katika uzinduzi wa  Airtel Rising Stars msimu wa sita unaotarajiwa kufanyika Juni 26 mwaka huu.
Kikosi cha vijana chini ya miaka 17 Serengeti Boys wakiwa katika picha ya pamoja  Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel, Beatrice Singano  (katikati) na  Mkurugenzi wa soka la vijana  TFF, Ayoub Nyenzi katika uzinduzi Airtel Rising Stars msimu wa sita unaotarajiwa kufanyika Juni 26 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad