JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


IDARA YA UHAMIAJI YAFANYA MABADILIKO KWA WAFANYAKAZI 200 KATIKA VITUO VYA KAZI.

Share This

Kaimu Kamishina wa Fedha na Utawala, Abbas Irovya akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo.

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
IDARA ya Uhamiaji imefanya mabadiliko ya wafanyakazi katika vituo vya kazi ikiwa ni kuongeza ufanisi wa kazi wa idara hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Kaimu Kamishina wa Fedha na Utawala, Abbas Irovya amesema mabadiliko hayo ni kuongeza ufanisi kazi na tija.

Mabadiliko hayo ni DCI.Faustine Nyaki Mkoa wa Iringa anahamia Mkoa Mwanza, na aliyekuwa Mwanza,DCI.Remigius Ibrahim Pesambilia anahamia kwenda kwa Mfwadhi wa Ofisi ya uhamiaji uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere , DCI.Rose Mhagama (Njombe) amehamia Mtwara,DCI.Chale,s Habe (Geita) anahamia Njombe.



Amesema kuwa mabadiliko hayo kwa wafanyakazi katika idara hiyo ni 200 ambapo inatokana agizo la Waziri mwenye dhamana hiyo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad