JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


WANAFUNZI WAPIMWE MATUMIZI YA DAWA ZA KULEVYA WAKIWA SHULENI –WAZIRI ,UMMY MWALIMU.

Share This
Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii.
TATIZO la utumiaji wa dawa za kulevya kwa  vijana unaanzia  katika shule, hivyo kunahitaji kupimwa wanafunzi wakiwa shuleni katika kuweza kutokomeza tatizo la utumiaji wa dawa hizo.
Hayo ameyasema leo jijini Dar es Salaam Waziri Afya, Maendeleo ya Jamii jinsia na Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu wakati makabidhiano ya  Gari ya Kituo cha  Kuratibu  Matumizi ya Sumu lilitolewa na nchi ya Japan kwa ofisi ya  Mkemia Mkuu wa Serikali,  amesema kuwa tatizo la utumiaji wa dawa unaanzia shule hivyo ofisi mkemia mkuu wa serikali anaweza kupima wanafunzi kila baada ya muda na kuweza kugundua chanzo cha dawa hizo.
Amesema kuwa wanafunzi wakipimwa kila baada ya muda mkemia anaweza kujua na serika ikaweza kudhibiti juu ya matumizi ya dawa  za kulevya kutokea shuleni.
Waziri, Ummy amesema vijana wanaotumia dawa za kulevya  wengine walianzia katika shule na kuweza kuwafundisha wengine na kuwa ongezeko la watumiaji wa dawa za kulevya na kusababisha nchi kukosa nguvu kazi ya vijana kutokana na kuathirika dawa hizo.
Aidha amesema katika kazi data ya kuweka taarifa za vinasaba vitasaaidia kupunguza watoto wa mitaani kutokana wazazi watambuliwa na vinasaba mara baada ya kupima.
Ummy, amesema kuwa ofisi ya mkemi mkuu wa serikali ni ana kazi kubwa ya kutoa haki kwa kushirikiana na vyombo vingine ikiwemo majanga moto kwa kuweza kutambua watu baada ya kutokea,  vinasaba vya watoto ambao wanakuwa katika mgogoro na kubaini mhusika.
Nae Mtendaji wa Maabara wa Ofisi ya Mkemia Mkuu, Profesa Samwel Manyere amesema kuwa kupata gari hilo watafanya kazi kwa kiwango cha juu kutokana na jinsi walivyojipanga.
Aidha amesema kuwa wameweza kupata cheti cha utoaji huduma kwa kiwango cha Kimataifa (ISO) hivyo kitu chochote kikifanyika kinaendana na viwango hivyo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad