JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


MGOMBEA WA CCM JIMBO LA KIGAMBONI AOMBA KURA KWA WANANCHI WA JIMBO HILO

Share This
Mgombea udiwani kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM, Kata ya Kibada, Jimbo la Kigamboni, Amini Sambo akijinadi kwenye eneo la kata hiyo, Dar es Salaam jana.
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi CCM, Phares Magesa, (kulia) akimnadi Mgombea udiwani wa chama hicho kata ya Kibada, Jimbo la Kigamboni, Amini Sambo eneo la Kibada, Dar es Salaam jana.

Na Mwandishi Wetu
KAULI mbalimbali za hamasa kuelekea uchaguzi mkuu zimeendelea kutawala majukwaani, huku jana Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM wilaya ya Temeke, Yahaya Sikunjema akiwavunja watu mbavu kwa vicheko na shangwe baada ya kuifananisha ccm na mama mjamzito mwenye sifa na uzoefu wa kuingia na kutoka salama siku zote kwenye chumba cha kujifungua yaani ‘leba’ huku upinzani ukiambulia.. ‘poole’

Akiwanadi kwa mbwembwe Mgombea urais kwa tiketi ya ccm, John Magufuli, Mbunge wa Jimbo la Kigamboni Dk Faustine Ndugulile na mgombea udiwani wa kata hiyo Amini Mzuri Sambo, eneo la Kibada Dar es Salaam jana, Sikunjema amesema historia ya CCM kuingia leba ya uchaguzi na kutoka salama inajidhihirisha wazi

Alisema kwa mara ya kwanza Tanu ilifanikiwa kutoka leba salama kwa kujifungua mtoto mzuri aliyeitwa Julius Kambarage Nyerere, baada ya hapo ikaingia leba tena na kujifungua jembe la nguvu Ally Hassan Mwinyi, ikaingia tena na kutoka salama na kipenzi chake Benjamin Mkapa, na kisha tukatoka tena salama kwa kumpata mtoto rangi ya chungwa Jakaya Kikwete

Huku akishangiliwa na mamia ya wananchi wa Kibada Sikunjema aliongeza kuwa katika kipindi chote hicho wapinzani kila wakitoka leba wamekuwa wakiambulia…poooole, “ hawana uzoefu hata kidogo na leba cha uchaguzi”

Aliongeza, “mtaniwia radhi akinamama kwa mfano huu..ila nataka nisisitize kuwa sote tunajua leba sio mahali pazuri, ukiingia kuna vitu vinne vinaweza kutokea..ama ukatoka salama, au ukapoteza mtoto au ukampoteza mama au ukapoteza vyote,..lakini ccm inajivunia kuwa na rekodi ya kutoka salama katika leba za chaguzi kwa vipindi vyote.”

Aidha, mwanasiasa huyo machachari aliyeongozana na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya chama hicho, Phares Magesa, kwa mwaliko wa mgombea udiwani wa kata hiyo Sambo, alihitimisha kwa kuomba kura za kutosha kwa wateule wa ccm kwa ngazi zote

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad