JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


MFUKO WA BIMA YA AFYA (NHIF) KIGOMA WAWAKUMBUKA WAZEE LEO KATIKA SIKU YAO.

Share This
Baadhi ya wafanyakazi wa mfuko wa bima ya afya NHIF kigoma wakikabidhi msaada wa vyakula kwa uongozi wa kituo cha Silabu cha kulelea wazee wasiojiweza ikiwa leo ni siku ya maadhimisho ya siku ya wazee duniani.
 Meneja wa Mfuko wa bima NHIF  ya kigoma akisalimiana na wazee wanaotunzwa katika kambi ya Silabu kata ya kibirizi
Baadhi ya wazee wasiojiweza wanaoishi na kutunzwa katika kambi ya kulea wazee ya Silabu kata ya Kibirizi Mkoani hapa.

 Na Editha Karlo.Kigoma
MFUKO wa Bima ya afya (NHIF)wametoa msaada wa  vyakula kwa wazee wasiojiweza uliopo katika kituo cha silabu kata ya kibirizi mjini hapa.

Akiongea baada ya kukabidhi msaada huo wa chakula Meneja wa Mkoa wa mfuko huo Elius Odhiambo alisema kuwa mfuko unatumbua umuhimu na mchango wa wazee kwa jamii.

"Sisi kama mfuko wa bima ya afya tuna thamini sana na kutambua mchango wenu wazee kwa jamii kwani kila mmoja wetu ni mzee mtarajiwa"alisema odhiambo

Alisema wamekabidhi msaada wa chakula wenye thamani ya shilingi milioni moja na elfu sitini,vyakula walivyotoa ni mchele kilo 100,sukari kilo 100,unga wa ugali kilo 100,maharage kilo 100 na mafuta ya kupikia kilo 20

Meneja huyo alisema wataendelea kusaidiana na kuwasaidia wazee hao kila inapobidi.

Naye mkuu wa kituo hicho cha kutunzia wazee Juma Ndikamukana wasiojiweza aliushukuru mfuko wa bima ya afya kwa msaada wao huo na kuwakumbuka wazee katika siku yao leo.

Alisema kituo hicho kina jumla ya wazee 51 wasiojiweza wanaotunzwa wanaotoka maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Kigoma

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad