JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


MAMA SALMA KIKWETE KATIKA MIKUTANO YA KAMPENI LINDI MJINI, NACHINGWEA NA LIWALE

Share This
  Mke wa Rais na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi,CCM, Mama Salma Kikwete akimnadi mgombea Urais kupitia CCM, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika katika uwanja wa Mpilipili huko Lindi Mjini tarehe 12.10.2015.
 Mgombea Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Mke wa Rais na Mjumbe wa NEC, Mama Salma Kikwete mara baada ya kumwombea kura kwa wananchi wa Manispaa ya Lindi kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye uwanja wa Mpilipili tarehe 12.10.2015. Aliyesimama kulia ni Mgombea Ubunge katika Jimbo la Mtama Ndugu Nape Nnauye.
Mke wa Rais na Mjumbe wa NEC Mama Salma Kikwete akiwa katika kijiji cha Ngunichile kilichoko katika Wilaya ya Nachingwea kwa ajili ya kuwanadi wagombea wa Chama Cha Mapinduzi kwenye Uchaguzi Mkuu utakaofanyika tarehe nchini tarehe 25.10.2015.  Katika mikutano hiyo Mama Salma alimnadi Dkt. John Magufuli kwenye urais na Ndugu Hassan Elias Masala kwenye Ubunge wa Jimbo la Nachingwea na Madiwani wote katika wilaya hiyo tarehe 13.10.2015.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad