JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


NHIF YAKABIDHI KADI ZA BIMA YA AFYA KWA WAVUVI LEO JIJINI DAR ES SALAAM

Share This
 Kaimu Mkurugenzi mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya  (NHIF) Bwana Michael Mhando akizungumza na wafanyabiashara   wa wasamaki katika Soko la  feri  hawapo pichani juu ya vikundi  vya    wajasiliamali wadogo na wakubwa  kujiunga na  Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
 Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya  (NHIF) Bwana Michael Mhando  akimkabidhi kadi ya uanachama ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya  (NHIF)  Mvuvi wa Samaki wa Soko Kuu la Feri Bwana Mohamed Ally Masoud mwishoni mwa wiki Jijini Dara es Salaam.
 Afisa Elimu kwa Umma wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya  (NHIF) Grace Michael akotowa eli kwa wavuvi  jinsi ya na kujiunga na mfuko huo
04.Mkurugenzi wa Mfuko wa Afya ya Jamii  Eugen Mikongoti akimffanulia jambo Mvuvi wa samko katika soko Kuu la samaki Fer leo jijini Dar es Salaam.

Maofisa wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) wakiendelea kueli misha leo jijini Dar es Salaam.
Picha na Emmanuel Massaka  ) 


MFUKO  wa Taifa wa Bima ya Afya  NHIF leo umekabidhi bima ya Afya kwa Wavi wadogowadogo (UWAWADA) wa mkoa wa Dar es Salaam,na Kaimu Mkurugenzi  wa mfuko huo,Michael Mhando .

Mhando amekabidhi Bima hizo leo kwenye soko kuu la kuuzia samaki Jijini Dar es Salaam maarufu ‘soko la feri’ ambapo awali ua kukabidhi bima hizo alisema kuwa anawapongeza wanachama wote wa uwawada waliojikusanya kwa vikundi vya watu kumi na kuhitaji siku ya leo kukabidhiwa Bima zao za NHIF kwa wanachama 10 waliojiunga na mfuko huo.

Alisema wanachama hao baada ya kukaa na kusikiliza huduma zinazotolewa na shirika hilo, namna ambavyo wamefanikiwa kufikia hatua hiyo ya kukabidhiwa bima zao kupitia mpango wa KIKOA ambao unawalenga hasa wajasiliamali wadogowadogo.

Aidha alisema kuwa vikundi husika kujiunga na mfuko huo ,hunufaika  na mafao ya matibabu sawa  na wanachama  wanaochangia kupitia mishahara yao ya kila mwezi.

Mhando alisisitiza kuwa lengo kubwa la mpango wa Mfuko wa Taifa wa Biama ya Afya ni kuyafikia makundi yote ya wajasiliamali wadogo na wakubwa ili kuwajumuisha katika mpango huo.

”Lengo letu kubwa la Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ni kuyafikia makundi yote ya wajasiliamali wadogo na wakubwa ili kuweza kuwajumuisha katika mpango huu”alisema Mhando.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad