JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


MKUTANO WA NNE WA BARA LA AFRIKA KUJADILI MIPANGO ENDELEVU NA MAFUNZO KUANZA KUFANYIKA KESHO HOTELI YA GIRRAFE JIJINI DAR ES SALAAM

Share This
Na Dotto Mwaibale
MKUTANO wa Nne wa Bara la Afrika wa kujadili mipango endelevu  katika eno la mafunzo kwa vijana na wataalamu  wasiojiweza na ushirikji wao katika soko la ajira, unatarajiwa kuanza kufanyika kesho Hoteli ya Girrafe jijini Dar es Salaam.

Mkutano huo ambao utashirikisha nchi mbalimbali tisa unatarajiwa kuhudhuriwa na wageni 50 kutoka katika nchi hizo za Afrika.

Akizungumza na waaandishi wa habari kuhusu Dar es Salaam jana kuhusu mkutano huo, Meneja Mipango wa Ofisi ya Maendeleo  Don Bosco Tanzania, Rosemarytery  Njoki alisema, mkutano huo utatoa nafasi kwa Mtandao wa Don Bosco Afrika kuchunguza njia ambazo zitaleta ushirikiano mzuri kati ya sekta binafsi na umma ili kuleta maendeleo zaidi.

“Mkutano unatarajiwa kutafakari juu ya mipango inayoendelea katika eneo la mafunzo ya kijamii na wataalamu vijana wasiojiweza na ushiriki wao katika soko la ajira. Kama vile namna bora ya washirika wanaweza kufanya kazi na binafsi na ya umma sekta kuelekea maendeleo endelevu,” alisema Njoki.

Alisema mkutano huo pia utazungumzia masuala ya jinsia hasa kwa upande wa upatikanaji wa mafunzo ya ufundi stadi na kuwafanya wanawake kuwa sawa na wanaume kwa kufanya kazi sawa.

“Pia tunatafuta kubadilishana uzoefu na washirika weu wa Afrika ambao wote tunafanya kazi ili kuboresha elimu, masuala ya mafunzio ya ufundi stadi na kuwaunganisha vijana na masoko ya ajira ya dunia,” alisema.

Alisema kwa mara ya kwanza mkutano huo unafanyika nchini kuanzia leo hadi Septemba 25, utakuwa ni kwa ajili ya ushirikiano wa sekta binafsi na umma. Alisema mkutano huo pia utawakutanisha shirikisha watu mbalimbali ikiwemo taasisi za serikali na chuo cha VETA.

Kwa upande wake Meneja Mipango wa Don Bosco, Bram Reekmans alisema, mkutano huo pia utatumika kuangalia njia ambazo Don Bosco inaweza kutumia kushirikiana zaidi na sekta binafsi kama sehemu ya mipango endelevu.

Alisema majadiliano mengine yatakuwa yanahusu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi namna ya kushirikiana ili kuboresha elimu.

Ofisa Mwezeshaji Aira wa Don Bosco Tanzania, Oswald Manyerere alisema, lengo la mafunzo yanayotolewa na tasisi hiyo ni kuhakikisha wanawawezesha vijana wasiojiweza kupiga hatua na hatimaye kufikia malengo waliyojiwekea.

Alisema vijana wanaopitia katika chuo hicho wamekuwa wakitafutiwa kazi baada ya kufanya mafunzo yao, ambapo kwa kipindi cha mwaka jana vijana waliomaliza walikuwa ni 322 na hadi sasa waliopatiwa kazi ni 220 huku idadi kubwa ikiwa ya wasichana sawa na asilimia 86.

Alisema wanafunzi hao ni kutoka katika shule zilizochini ya Don Bosco, Dodoma, Iringa na  Oyterbay Dar es Salaam. 

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Maendeleo wa Don Bosco,Celestine Kharkongor alisema Don Boscow ilianza hapa nchini mwaka 1996.

Alisema tangu kuanzishwa kwa chuo cha Don Bosco kimeleta mabadiliko ya tabia kwa vijana pamoja na kuwakwamua kiuchumi.

Mwalimu wa Don Bosco, Hellen Jackson alisema mafunzo yanayotolewa na chuo cha Don Bosco yatasaidia kutoa ajira kwa vijana na kuondoa changamoto zilizopo sasa za ukosefu wa ajira hapa nchini.

Alisema wazazi wenye watoto wa kike ni fursa kwao kuwapeleka katika chuo hicho.
(Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com
 Mkurugenzi wa Maendeleo wa Don Bosco Tanzania ,Celestine Kharkongor (kulia), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Don Bosco Oyterbay jijini Dar es Salaam jana, kuhusu mkutano huo na shughuli zinazofanywa na Don Bosco hapa nchini.
 Meneja Mipango wa Ofisi ya Maendeleo  Don Bosco Tanzania, Rosemarytery  Njoki (kushoto), akizungumza katika mkutano huo. Kutoka kulia ni  Mkurugenzi wa Maendeleo wa Don Bosco Tanzania ,Celestine Kharkongor, Mratibu wa Don Bosco, Maika Denys na Meneja Mipango wa Don Bosco, Bram Reekmans.
 Meneja Mipango wa Don Bosco, Bram Reekmans (katikati), akizungumza kwenye mkutano huo.
 Mratibu wa Don Bosco, Maika Denys (kulia), akichangia jambo.


 Mwalimu wa Don Bosco, Hellen Jackson (kulia), akielezea mafanikio makubwa wanayopata wanafunzi katika shule hiyo.
Ofisa Mwezeshaji Aira wa Don Bosco Tanzania, Oswald Manyerere (kushoto), akielezea jinsi Don Bosco ilivyofanikiwa kuwatafutia ajira wanafunzi wao waliohitimu mafunzo mbalimbali.
Mkuu wa Idara ya Utafuta wa ajira na Ofisa Masoko, Don Bosco Dar es Salaam, Nyerembe Yunus Nyampiga (kushoto), akizungumza katika mkutano huo.

 Mmoja wa wanafunzi wa DonBosco akielezea mafanikio wanayopata shuleni hapo.
 Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.
 Wanafunzi na walimu wao wakiwa kwenye mkutano huo.
 Wanafunzi wakifuatilia kwa makini mkutano huo.
 Viongozi wa Don Bosco wakiwa meza kuu.
 Mkutano ukiendelea.
Wanahabari na Wanafunzi wakiwa kwenye mkutano huo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad