JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


KAMATI YA UCHAGUZI DRFA YAELEKEZA UCHAGUZI WA TEFA KUFANYIKA AGOSTI 23 MWAKA HUU

Share This
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI         
KAMATI 
ya uchaguzi DRFA inaelekeza kamati ya uchaguzi ya TEFA kufanya uchaguzi wa viongozi,jumapili tarehe 23/08/2015 katika ukumbi wa JKT kama ilivyopangwa kufanyika hapo awali.
Kamati pia inapenda  kuutarifu umma kuwa mchakato huu una Baraka zote kutoka TFF,hivyo uingiliaji wowote unakwenda kinyume na ibara ya 6(1)ya kanuni za uchaguzi za TFF 2013 na ibara za 52(6) na 56(6)(a) za katiba ya TFF ambazo zinaelekeza kuwa majukumu ya uchaguzi yapo chini ya kamati ya uchaguzi.
Itakumbukwa uchaguzi huo uliokuwa ufanyike jumapili ya tarehe 16,08,2015 uliahirishwa na kamati ya uchaguzi ya Tefa licha ya shirikisho la TFF kuagiza ufanyike,na hivyo mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi DRFA wakili Rashid Saadallah akaitaka kamati hiyo ya TEFA kumuandikia barua kueleza sababu ya kuahirisha uchaguzi huo.
baada ya kupitia sababu hizo,ndipo DRFA ikatoa majibu kwa kuelekeza uchaguzi huo sasa kufanyika jumapili hii.
KOZI YA MAKOCHA LESENI ‘C’ ILIYOANDALIWA NA  DRFA SASA YAIVA,WADAU WAOMBWA KULIPIA  ADA ZAO  MAPEMA.
kozi ya ukocha leseni C inatarajiwa kufanyika kuanza tarehe 28. 08. 2015,katika ukumbi wa TFF Uwanja wa Karume, ambapo washiriki wanakumbushwa kulipia ada zao za ushiriki ambayo ni shilingi  TZS 250,000.
Katika kzoi hiyo inategemewa kuwepo na madarasa mawili ya wanafunzi 30 kila darasa.
NB;NIMEAMBATANISHA NA MAJINA YA WASHIRIKI HAPO CHINI.
IMETOLEWA NA CHAMA CHA SOKA DAR ES SALAAM DRFA

Omary Katanga mkuu wa Habari na Mawasiliano DRFA

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad