JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


BENKI YA EXIM YAAHIDI KUSAPOTI ZAIDI MICHEZO VISIWANI ZANZIBAR

Share This
Meneja wa benki ya Exim Tanzania  tawi la Zanzibar Bw. Mwinyimkuu Ngalima akimkabidhi seti ya jezi mwakilishi kutoka timu ya soka yaa Kid Boys ya visiwani humo ikiwa ni sehemu ya udhamini wa mashindano yaliyolenga kuibua vipaji vya mchezo huo yaliyohitimishwa kwenye Uwanja wa Abeid Amani Karume, wilayani Mwanakwerekwe hivi karibuni.
Waziri wa Kazi na Huduma za jamii, Zanzibar  Mh.Ali Suleiman (mwenye suti ya kaki) akikabidhi kikombe cha ushindi kwa Nahodha wa timu ya soka ya Feza ambayo ilifanikiwa kuibuka mshindi kwenye mashindano yaliyolenga kuibua vipaji vya mchezo huo yaliyohitimishwa kwenye Uwanja wa Abeid Amani Karume, wilayani Mwanakwerekwe hivi karibuni. Wanaoshuhudia ni baadhi ya maofisa kutoka benki ya Exim Tanzania (wadhaamini) pamoja na waandaaji wa mashindano hayo.

Baadhi ya Maofisa kutoka benki ya Exim Tanzania, wakisalimiana na wachezaji wa timu ya soka ya Kid boys ya visiwani Zanzibar kabla ya kuanza kwa mchezo uliozikutanisha timu hiyo dhidi ya timu ya Feza ya visiwani humo pia kwenye mashindano yaliyolenga kuibua vipaji vya mchezo huo yaliyohitimishwa kwenye Uwanja wa Abeid Amani Karume, wilayani Mwanakwerekwe hivi karibuni. Timu ya Feza ilibuka na ushindi wa 1-0 dhidi ya Kid boys.

Zanzibar, Benki ya Exim Tanzania imeahidi kuunganisha nguvu zaidi na mamlaka za kimichezo visiwani Zanzibar katika kuhakikisha sekta ya michezo visiwani humo inakua zaidi.

Hatua hiyo ya benki ya Exim ilitangazwa na Meneja wa tawi la benki hiyo visiwani humo Bw.Mwinyimkuu Said Ngalima wakati wa kilele cha mashindano ya soka yaliyolenga kuibua vipaji vya mchezo huo yaliyohitimishwa kwenye Uwanja wa Abeid Amani Karume, wilayani Mwanakwerekwe kwa udhamini wa benki hiyo.

“ Kutokana na jitihada zinazoonyeshwa na mamlaka za michezo sambamba na Serikali tumeona na sisi pia tuna haja ya kuunga mkono jitihada hizi hasa katika kuibua vipaji ikiwa ni sehemu ya mpango wetu wa kushirikiana na jamii.’’ alisema Bw. Ngalima.

Benki hiyo ilikabidhi zawadi mbalimbali kwa washindi tofauti ikiwemo seti mbili za jezi kwa timu zilizoingia fainali, zawadi kwa mchezaji bora, goli kipa bora na muamuzi bora. Pia benki hiyo ilitoa zawadi kwa mchezaji aliyeonyesha kipaji zaidi.

Fainali hiyo ilivutia mashabiki wengi wakiwemo viongozi wa serikali wilayani humo na maeneo jirani wakiongozwa na Waziri wa Kazi na Huduma za jamii, Mh.Ali Suleiman ambapo hadi mwisho wa mchezo timu ya Feza iliibuka na ushindi wa goli 1-0 dhidi ya wapinzani wao timu ya Kid Boys.

Akizungumza mara tu baada ya kukabidhi zawadi kwa washindi Mh. Suleiman mbali na kuipongeza benki ya Exim kwa udhamini wa mchezo huo pia alitoa wito kwa mashirika na taasisi mbalimbali kujitokeza kwa wingi ili kusaidia sekta ya michezo visiwani humo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad