JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


MAKALA YA SHERIA: USIFANYE MAKOSA, HUU NDIO UTARATIBU WA KUNUNUA NYUMBA ILIYOWEKWA REHANI/DHAMANA BENKI

Share This

Nimewahi kuandika mara kwa mara kuhusu utaratibu mzuri wa kumwezesha mtu kununua nyumba huku akiwa ameepuka mgogoro. Nilitahadharisha sana kuhusu migogoro ya ardhi ambayo sasa imekuwa janga la kitaifa hapa kwetu. Nakumbuka moja kati ya mambo niliyoeleza ni kuwa utaratibu wa manunuzi ya nyumba/viwanja unatofautiana.Nikasema kwamba tofauti zake zinatokana na ukweli kuwa kila nyumba ina mazingira yake. Hata hivyo sikusema utofauti wa mazingira hayo ila sasa naweza kueleza kwa ufupi utofauti wa mazingira ya kila nyumba unapokuwa katika taratibu za ununuzi.

1.UTOFAUTI WA KITAALAM KATIKA UNUNUZI NYUMBA.

Usikurupuke unapohitaji kununua ardhi. Unapaswa kujua kuwa nyumba na viwanja zina taratibu tofauti unapohitaji kununua. Ukikurupuka utalipia gharama ya kukurupuka kwako. Kutokana na hilo ni muhimu tujue kuwa kuna nyumba inayouzwa kwa utaratibu wa kawaida wa mmiliki mwenyewe kumuuzia mnunuzi. Hii mara nyingi huwa haina shida sana kwakuwa unahitaji tu kujiridhisha na baadhi ya mambo ya msingi kama kufanya upekuzi rasmi ( official search) katika mamlaka za ardhi n.k.

Pili kuna nyumba inayouzwa na wasimamizi wa mirathi. Hii uuzwaji wake hauko sawa na ile inayouzwa na mmiliki halisi. Hawa ni wasimamizi wa mirathi hivyo hata uuzaji wao si uuzaji kama wa mmliki halisi. Utofauti wao upo katika namna ya kuandika mkataba( sale agreement) na nyaraka ambazo wanapaswa kukuonesha wewe mnunuzi . Pia kuna ununuzi wa nyumba ya mkopo ambao sasa ndio mada ya leo. Ununuzi wa nyumba ya mkopo nao si ununuzi kama wa nyumba ya kawaida. Haufanani na nyumba ya kawaida na haufanani na wa nyumba ya mirathi. Unazo tarati bu zake tofauti kabisa na ununuzi mwingine.

Kusoma zaidi BOFYA HAPA

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad