Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Cambridge cha Uingereza, wameaanzisha utafiti wa vinasaba unaolenga kuboresha matibabu ya saratani ya tezi kwa watoto nchini Tanzania na ukanda wa Afrika.
Akieleza kuhusu utafiti huo, Dkt. Advera Ngaiza, Bingwa wa Uchunguzi wa Magonjwa ya Saratani amesema mradi huo utahusisha uchukuaji wa sampuli za vinasaba na tishu kutoka kwa watoto wenye saratani ya tezi nchini Tanzania.
Amesema sampuli hizo zitachakatwa katika Maabara Kuu ya MNH, huku uchunguzi wa kina wa kisayansi ukifanyika ili kuelewa kwa nini matibabu ya sasa hayatoi matokeo mazuri kwa watoto wa Kiafrika.
"Lengo letu ni kugundua dawa salama, sahihi na yenye ufanisi mkubwa zaidi itakayosaidia kutibu saratani ya tezi kwa watoto katika ukanda wa Afrika."
Hatua hii inakuja baada ya kubainika kuwa mifumo mingi ya sasa ya matibabu haitoi matokeo yanayotarajiwa kwa watoto wa ukanda huu wa afrika ikilinganishwa na maeneo mengine duniani.








No comments:
Post a Comment