Standard Chartered imefanikiwa kupanga ufadhili wa pamoja unaozidi dola za Marekani bilioni 2.33 kusaidia mradi mkubwa wa maendeleo ya reli katika Afrika Mashariki. Fedha hizo zitatumika na Yapi Merkezi kwa ajili ya ujenzi wa Kipande cha 3 na Kipande cha 4 (takribani kilomita 430) za Reli ya Kisasa ya Standard Gauge (“SGR”) nchini Tanzania, inayounganisha Makutupora na Isaka.
Kipande cha 5 cha SGR, kinachounganisha Isaka na Mwanza (takribani kilomita 249), kinajengwa na China Civil Engineering Construction Corporation. Mradi wa reli ya SGR (Vipande vya 1 hadi 5) unaounganisha Dar es Salaam na Mwanza ni miongoni mwa miradi mikubwa zaidi ya miundombinu katika historia ya nchi.
Ufadhili wa SGR kwa vipande vya 3 na 4 unajumuisha dola za Marekani bilioni 1.32 kutoka kwa Export Credit Agencies (ECA) uliosainiwa mwaka 2025 na 2026, pamoja na dola milioni 462 za ufadhili wa muda mrefu kutoka benki za kibiashara na taasisi za fedha za maendeleo, uliosainiwa mwaka 2023.
Standard Chartered ilifanya kazi kama Mratibu Mkuu wa Kimataifa, Bookrunner, Mpangaji Mkuu aliyeteuliwa, Wakala wa Mfuko na Mkopesha kwa Wizara ya Fedha ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Vifurushi vya ECA vinajumuisha msaada kutoka EKN (Uswidi), KUKE (Poland) na SACE (Italia) kama ECAs zinazoongoza, pamoja na bima ya ziada kutoka ECAs nyingine mbili.
Ufadhili wa SGR kwa Kipande cha 5 unajumuisha dola milioni 559 kutoka Sinosure (Wakala wa Mikopo ya Mauzo ya Nje wa China), uliotolewa mwaka 2025. Standard Chartered pia ilifanya kazi kama Mratibu Mkuu wa Kimataifa, Bookrunner, Mpangaji Mkuu aliyeteuliwa, Wakala wa Mfuko na Mkopesha kwa Wizara ya Fedha ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Muamala huu unaonesha ushirikiano thabiti na uratibu mzuri kati ya taasisi mbalimbali za ECA katika kusaidia miradi muhimu ya kimkakati ya miundombinu yenye kuleta manufaa halisi kwa uchumi na jamii za eneo husika.
Ujenzi na uboreshaji wa SGR utaunganisha bandari ya Dar es Salaam na magharibi mwa Tanzania pamoja na nchi jirani, ukitoa njia ya usafiri inayotegemewa kwa abiria na mizigo. SGR itachochea maendeleo ya kiuchumi katika maeneo ya ndani ya Tanzania na kutoa fursa za ajira kwa wananchi wa maeneo hayo. Serikali ya Tanzania inaunga mkono maendeleo ya SGR kupitia Shirika la Reli Tanzania (TRC).
Ufadhili huu unaimarisha dhamira ya Standard Chartered ya kuisaidia Serikali ya Tanzania kufikia malengo yake ya ukuaji, ukijenga juu ya ufadhili wa dola bilioni 1.46 ulioongozwa na ECA uliopangwa na Standard Chartered kwa Vipande vya 1 na 2 vya SGR, uliosainiwa mwaka 2020.
Ciro Aquino, Mkuu wa Task Force Africa, SACE, alisema:“SACE inafurahia kuunga mkono Vipande vya 3 na 4 vya Reli ya Standard Gauge (SGR), kufuatia msaada wake kwa Vipande vya 1 na 2 vya mradi huo nchini Tanzania. Mafanikio haya yanaakisi dhamira madhubuti ya SACE ya kuimarisha na kukuza mnyororo wa ugavi wa Italia, na kuyaweka makampuni ya Italia kama washirika muhimu katika kuimarisha uunganishaji na ukuaji wa uchumi barani Afrika, ambayo ni malengo makuu ya Mpango wa Mattei.”
Ã…ke Nordlander, Mkurugenzi Mkuu wa EKN, alitoa maoni “EKN ilikuwa sehemu ya SGR Vipande vya 1 na 2, mradi ambao tayari unatoa mbadala salama na wenye ufanisi zaidi kuliko usafiri wa barabara, na sasa pia ni sehemu ya Vipande vya 3 na 4. Tunajivunia EKN kusaidia mauzo ya nje ya Uswisi yanayochangia maendeleo haya muhimu.”
Janusz WÅ‚adyczak, Mkurugenzi Mtendaji wa KUKE, alisema “KUKE ilikuwa na dhamira kubwa kushiriki katika mradi huu wa kimkakati nchini Tanzania. Uwekezaji huu unaonesha umuhimu mkubwa wa ushirikiano wa kimataifa na kutumia uwezo wa taasisi za kifedha kutoka nchi mbalimbali ili kuleta athari chanya kubwa na yenye maana katika maisha ya watu barani Afrika.”
Herman Kasekende, Mkurugenzi Mtendaji na Mkuu wa Huduma za Wateja wa Standard Chartered Tanzania, alisema “Tumejizatiti kusaidia kufadhili utekelezaji wa miundombinu mikubwa ili kuunga mkono ukuaji endelevu barani Afrika, na tunafurahia kuona mradi huu wa reli ukiiweka Tanzania kama kitovu kikuu cha usafirishaji na usambazaji, huku ukichochea biashara ya kikanda na kuzalisha ajira.
Standard Chartered, kwa kushirikiana na washirika wetu, tunajivunia kutumia mtandao wetu wa kipekee na uwezo wetu kusaidia fursa za uwekezaji wa kimataifa nchini Tanzania.”
.jpeg)

Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Natu El-maamry Mwamba na Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered, Bw. Herman Kasekende, wakibadilishana Mkataba wa kugharamia ukamilishaji wa Reli ya Kisasa (Standard Gauge -SGR), kipande cha tatu (loti 3) na cha nne (loti 4) kutoka Makutupora ya mkoani Singida hadi Isaka, yenye thamani ya takriban dola za Marekani bilioni 1.277, katika hafla iliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kambarage, Treasury Square, jijini Dodoma.


Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Natu El-maamry Mwamba na Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered, Bw. Herman Kasekende, wakisaini Mkataba wa kugharamia ukamilishaji wa Reli ya Kisasa (Standard Gauge -SGR), kipande cha tatu (loti 3) na cha nne (loti 4) kutoka Makutupora ya mkoani Singida hadi Isaka, yenye thamani ya takriban dola za Marekani bilioni 1.277, katika hafla iliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kambarage, Treasury Square, jijini Dodoma.
Ufadhili wa SGR kwa vipande vya 3 na 4 unajumuisha dola za Marekani bilioni 1.32 kutoka kwa Export Credit Agencies (ECA) uliosainiwa mwaka 2025 na 2026, pamoja na dola milioni 462 za ufadhili wa muda mrefu kutoka benki za kibiashara na taasisi za fedha za maendeleo, uliosainiwa mwaka 2023.
Standard Chartered ilifanya kazi kama Mratibu Mkuu wa Kimataifa, Bookrunner, Mpangaji Mkuu aliyeteuliwa, Wakala wa Mfuko na Mkopesha kwa Wizara ya Fedha ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Vifurushi vya ECA vinajumuisha msaada kutoka EKN (Uswidi), KUKE (Poland) na SACE (Italia) kama ECAs zinazoongoza, pamoja na bima ya ziada kutoka ECAs nyingine mbili.
Ufadhili wa SGR kwa Kipande cha 5 unajumuisha dola milioni 559 kutoka Sinosure (Wakala wa Mikopo ya Mauzo ya Nje wa China), uliotolewa mwaka 2025. Standard Chartered pia ilifanya kazi kama Mratibu Mkuu wa Kimataifa, Bookrunner, Mpangaji Mkuu aliyeteuliwa, Wakala wa Mfuko na Mkopesha kwa Wizara ya Fedha ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Muamala huu unaonesha ushirikiano thabiti na uratibu mzuri kati ya taasisi mbalimbali za ECA katika kusaidia miradi muhimu ya kimkakati ya miundombinu yenye kuleta manufaa halisi kwa uchumi na jamii za eneo husika.
Ujenzi na uboreshaji wa SGR utaunganisha bandari ya Dar es Salaam na magharibi mwa Tanzania pamoja na nchi jirani, ukitoa njia ya usafiri inayotegemewa kwa abiria na mizigo. SGR itachochea maendeleo ya kiuchumi katika maeneo ya ndani ya Tanzania na kutoa fursa za ajira kwa wananchi wa maeneo hayo. Serikali ya Tanzania inaunga mkono maendeleo ya SGR kupitia Shirika la Reli Tanzania (TRC).
Ufadhili huu unaimarisha dhamira ya Standard Chartered ya kuisaidia Serikali ya Tanzania kufikia malengo yake ya ukuaji, ukijenga juu ya ufadhili wa dola bilioni 1.46 ulioongozwa na ECA uliopangwa na Standard Chartered kwa Vipande vya 1 na 2 vya SGR, uliosainiwa mwaka 2020.
Ciro Aquino, Mkuu wa Task Force Africa, SACE, alisema:“SACE inafurahia kuunga mkono Vipande vya 3 na 4 vya Reli ya Standard Gauge (SGR), kufuatia msaada wake kwa Vipande vya 1 na 2 vya mradi huo nchini Tanzania. Mafanikio haya yanaakisi dhamira madhubuti ya SACE ya kuimarisha na kukuza mnyororo wa ugavi wa Italia, na kuyaweka makampuni ya Italia kama washirika muhimu katika kuimarisha uunganishaji na ukuaji wa uchumi barani Afrika, ambayo ni malengo makuu ya Mpango wa Mattei.”
Ã…ke Nordlander, Mkurugenzi Mkuu wa EKN, alitoa maoni “EKN ilikuwa sehemu ya SGR Vipande vya 1 na 2, mradi ambao tayari unatoa mbadala salama na wenye ufanisi zaidi kuliko usafiri wa barabara, na sasa pia ni sehemu ya Vipande vya 3 na 4. Tunajivunia EKN kusaidia mauzo ya nje ya Uswisi yanayochangia maendeleo haya muhimu.”
Janusz WÅ‚adyczak, Mkurugenzi Mtendaji wa KUKE, alisema “KUKE ilikuwa na dhamira kubwa kushiriki katika mradi huu wa kimkakati nchini Tanzania. Uwekezaji huu unaonesha umuhimu mkubwa wa ushirikiano wa kimataifa na kutumia uwezo wa taasisi za kifedha kutoka nchi mbalimbali ili kuleta athari chanya kubwa na yenye maana katika maisha ya watu barani Afrika.”
Herman Kasekende, Mkurugenzi Mtendaji na Mkuu wa Huduma za Wateja wa Standard Chartered Tanzania, alisema “Tumejizatiti kusaidia kufadhili utekelezaji wa miundombinu mikubwa ili kuunga mkono ukuaji endelevu barani Afrika, na tunafurahia kuona mradi huu wa reli ukiiweka Tanzania kama kitovu kikuu cha usafirishaji na usambazaji, huku ukichochea biashara ya kikanda na kuzalisha ajira.
Standard Chartered, kwa kushirikiana na washirika wetu, tunajivunia kutumia mtandao wetu wa kipekee na uwezo wetu kusaidia fursa za uwekezaji wa kimataifa nchini Tanzania.”
.jpeg)

Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Natu El-maamry Mwamba na Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered, Bw. Herman Kasekende, wakibadilishana Mkataba wa kugharamia ukamilishaji wa Reli ya Kisasa (Standard Gauge -SGR), kipande cha tatu (loti 3) na cha nne (loti 4) kutoka Makutupora ya mkoani Singida hadi Isaka, yenye thamani ya takriban dola za Marekani bilioni 1.277, katika hafla iliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kambarage, Treasury Square, jijini Dodoma.


Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Natu El-maamry Mwamba na Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered, Bw. Herman Kasekende, wakisaini Mkataba wa kugharamia ukamilishaji wa Reli ya Kisasa (Standard Gauge -SGR), kipande cha tatu (loti 3) na cha nne (loti 4) kutoka Makutupora ya mkoani Singida hadi Isaka, yenye thamani ya takriban dola za Marekani bilioni 1.277, katika hafla iliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kambarage, Treasury Square, jijini Dodoma.


No comments:
Post a Comment