JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


Oryx Yagawia Watumishi wa Afya Kwimba Mitungi 167 ya Gesi

Share This
Na Mwandishi Wetu,Kwimba

WATUMISHI wa sekta ya afya katika Wilaya ya Kwimba wamepatiwa nishati safi ya kupikia ya mitungi mikubwa ya gesi ya Oryx na majiko yake pamoja na kupatiwa elimu ya matumizi sahihi na salama ya nishati hiyo.

Mitungi hiyo ya gesi ya Oryx kwa watumishi hao wa sekta ya afya Wilaya ya Kwimba Februari wamepatiwa jana Februari 28,2026 wakati wa uzinduzi wa jengo la kisasa la kuhudumia watoto wanaozaliwa kabla ya wakati (njiti) katika Wilaya hiyo na jengo hilo ya limejengwa kwa ufadhili wa Doris Mollel Foundation (DMF) kwa kushirikiana na Keep a Child Alive (KCA)

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Oryx Gas Tanzania Benoit Araman ,Meneja Mafunzo wa kampuni hiyo Peter Ndomba amesema wamegawa mitungi ya gesi kwa watumishi hao wa hospitali Wilaya ya Kwimba kama sehemu ya kuunga mkono jitihada hizo za kuhudumia watoto njiti lakini pia kuendelea kuhamasisha nishati safi ya kupikia nchini kwa kundi hilo muhimu.

“Oryx Gas Tanzania pamoja na Doris Mollel Foundation tayari tuna mkataba wa miaka minne katika kuunga mkono juhudi zake kwa mtoto njiti na leo tunatoa mitungi 167 kwa wafanyakazi wote wa idara ya afya hapa Kwimba

“Unajua kwanini tunafanya hivyo?Tunajua watu wa idara ya afya ndio wanakutana na wagonjwa kwa mara ya kwanza,wao ndio wasomi na ndio watalaam ambao wanaweza kuelekeza wagonjwa jinsi gani ya kujiepusha na madhara ya kuni na mkaa.

“Hivyo tumeona ni muhimu kundi hili kulisapoti na kupitia ubia wetu sisi na Dorris Mollel Foundation tutaendelea kufanyakazi ndani ya miaka minne ili kwa pamoja tujue tumefikia hatua gani kwa nchi nzima,”amesema Ndomba .

Kuhusu mafunzo ya matumizi sahihi na salama ya nishati ya kupikia ya gesi ,Ndomba amesema Oryx Gas lengo pia ni kuiwezesha kada hiyo ya sekta ya afya kuwa na uelewa mpana kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia ya gesi kisha wawe mabalozi kwa wananchi wengine wakiwemo wagonjwa.

“Tumeamua kutoa mafunzo haya kwasababu tunajua wananchi wanapopata matatizo ya kiafya wanakuja hospitali kwahiyo wale ndio wanakuwa watu wa kwanza kukutana na wananchi wenye matatizo.

Kwa upande wao watumishi wa sekta ya afya katika Wilaya hiyo wameishukuru kwa kupatiwa mitungi ya gesi pamoja na elimu ya matumizi sahihi na salama ya gesi ya kupikia kwani wanaamini watakuwa mabalozi waziri wa kuelezea faida za kutumia nishati hiyo ya kupikia ambayo ni salama kiafya.

Akizungumza baada ya kupatiwa mitungi hiyo Dk.Makore Maro ameishukuru kampuni hiyo kwa kuwapatia mitungi ya gesi ambayo kwao itakuwa na tija kubwa huku wakieleza kwa sasa kupitia majiko ya gesi waliyopatiwa watatumia muda mfupi kuandaa chakula na hivyo kuwa na muda mwingi wa kuhudumia wagonjwa.

Wakati huo huo Maria Sakimu ambaye ni Muuguzi na Msimamizi Wodi ya Wazazi katika Hospitali ya Wilaya ya Kwimba amesema wanashukuru kupatiwa nishati safi ya kupikia huku akieleza watakuwa mabalozi kwa wengine kuelezea umuhimu wa kutumia nishati safi ya kupikia ya badala ya kutumia nishati chafu ya kupikia ya kuni na mkaa .


















No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad