
KATIKA kuendeleza juhudi za kuimarisha usafi wa mazingira na afya ya jamii, Meridianbet imetoa msaada wa mapipa ya taka katika maeneo ya umma ndani ya Manispaa ya Kinondoni na maeneo mbalimbali ya wazi. Hatua hii inalenga kupunguza uchafuzi wa mazingira, na kuweka mazingira safi na salama kwa wafanyabiashara, wanunuzi na wananchi kwa ujumla.
Akizungumza wakati wa tukio hilo, Afisa Mawasiliano wa Meridianbet, Nancy Ingram aliwatambua wafanyakazi wa usafi kama nguzo muhimu ya afya ya jamii. “Hawa ni mashujaa wa afya ya jamii yetu. Kazi yao ni ngumu lakini ya muhimu sana. Kama Meridianbet, tunatambua mchango wao mkubwa na tumeona ni vyema kuonyesha kuthamini kazi yao kwa kuwapatia vifaa vya msingi vya kujikinga na mazingira hatarishi wanapokuwa kazini,” alisema.
Meridianbet haikuachi nyuma, kuna michezo mbalimbali ya kasino mtandaoni pamoja na mechi za kimataifa za kubashiri zenye odds bomba zinazokuongezea nafasi ya kuongeza kipato chako kila siku. Kujiunga ni rahisi, Tembelea meridianbet.co.tz au piga *149*10#.
Kwa upande wake, Mwakilishi kutoka Manispaa ya Kinondoni aliishukuru Meridianbet kwa msaada huo na kuuelezea kama mfano bora wa ushirikiano kati ya sekta binafsi na Serikali katika kuinua ustawi wa wafanyakazi wa ngazi ya chini huku akisisitiza umuhimu wa mshikamano katika kufanikisha maendeleo endelevu.
Zoezi hili ni sehemu ya mpango mpana wa uwajibikaji kwa jamii (CSR) wa Meridianbet, ambapo kampuni imekuwa mstari wa mbele kusaidia makundi mbalimbali kupitia misaada ya kijamii, sekta ya elimu, huduma za afya na ustawi wa vijana kupitia michezo.
Kwa kuendeleza shughuli kama hizi, Meridianbet inaendelea kuthibitisha kuwa si tu kinara katika burudani ya michezo ya kubahatisha, bali pia ni mshirika wa kweli wa maendeleo ya jamii. Uwekezaji katika usafi na afya ya mazingira ni hatua madhubuti kuelekea Tanzania safi, salama na yenye ustawi kwa wote.


No comments:
Post a Comment