Mkuu wa Mikakati na Bidhaa za Wateja Binafsi wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Heristraton Genesis (wa pili kushoto), akizungumza, wakati wa hafla ya kukabidhi gari jipya kabisa aina ya Subaru Forester 2024 kwa mshindi wa kwanza wa kampeni inayoendelea ya Tumia na Ushinde 'Spend & Win' Bw. Rashidi Saidi (wa tatu kutoka kulia), katika hafla iliyofanyika Dar es Salaam leo. Kampeni hii inalenga kuwahamasisha Watanzania kufanya miamala ya kibenki kwa njia za kidijitali, kama vile kadi za ATM na kadi za mkopo, zinazotoa usalama, urahisi, na upatikanaji wa huduma mbalimbali za kibenki.
Mshindi wa Droo ya Kwanza ya Kampeni ya Tumia na Ushinde 'Spend & Win', ya Benki ya Absa Tanzania, Bw. Rashid Nassoro, akipozi kwa picha ndani ya gari lake aina ya Subaru Forester 2024 lenye thamani ya zaidi ya shs milioni 40 jijini Dar es Salaam leo baada ya kukabidhiwa rasmi.


No comments:
Post a Comment