Bandari ya Mtwara imeendelea kupokea Meli zaidi zinazoleta makasha matupu ambapo tarehe 27 Oktoba 2024 Meli ya MV LAKONIA ya Kampuni ya SINOTASHIP (COSCO) ilitia nanga Bandarini hapo kwa ajili ya kupakua shehena ya makasha matupu 300 na inatarajiwa kupakia shehena ya makasha 175 ya korosho za msimu wa mwaka 2024/2025.
Meli hii ni ya pili kuletwa na Kampuni ya SINOTASHIP baada ya MV CONTSHIP DAY kutia nanga tarehe 1 Oktoba 2024 ikiwa na makasha matupu 240.
Meli hii inafanya jumla ya Meli zilizowasili katika Bandari ya Mtwara kufikia nane (8) ambapo inafanya idadi ya makasha matupu yaliyowasili hadi sasa kufikia 3,999 tayari kwa kuanza kuhudumia shehena ya korosho kwenda nchi za nje.
Aidha, Meli ya MV LAKONIA itakuwa ya kwanza kwa msimu huu kuanza kusafirisha korosho ghafi kwenda nchi za nje ambapo itasafirisha korosho hizo kwenda nchini Vietnam.
Kampuni ya SINOTASHIP imeahidi kuendelea kuleta Meli nyingine ikiwemo MV AREOPOLIS inayotarajiwa kutia nanga mwanzoni mwa mwezi Novemba ikiwa na makasha matupu 300.
BANDARI YA MTWARA YAENDELEA KUPOKEA MELI ZAIDI ZINAZOLETA MAKASHA MATUPU
Share This
Tags
# HABARI
Share This
Jiachie Blog
HABARI
Labels:
HABARI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Author Details
A Tanzanian blog operating since 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.
No comments:
Post a Comment