JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


TPA yatekeleza maagizo ya Bodi ya TASAC Bandari ya Nyamisati

Share This
 
Mwenyekiti wa Bodi ya TASAC Nahodha Mussa Mandia akizungumza katika Bandari ya Nyamisati wakati  Bodi hiyo ilipofanya ziara Bandari hapo.
Mwenyekiti wa Bodi ya TASAC Nahodha Mussa Mandia akizungumza na Waandishi wa Habari wakati Bodi hiyo ilipofanya ziara katika Bandari ya Nyamisati wilayani Kibiti Mkoani Pwani kuangalia uendelezaji wa Bandari hiyo.
Mkurugenzi Mkuu wa TASAC Mohamed Salum alieleza kuhusiana na mipango ya mkakati katika Bandari ya Nyamisati katika kutoa huduma za Usafiri kwa Vyombo Vidogo vya Majini.
Meneja wa Bandari ya Nyamisati Issa Unemba akizungumza  na Waandishi wa Habari kuhusiana na utendaji wa Bandari hiyo pamoja na maboresho yaliyofanyika wakati Bodi ya TASAC ilipotembelea Bandari ya Nyamisati wilayani Kibiti mkoani Pwani.
Mkurugenzi Mkuu wa TASAC Mohamed Salum akiangalia chombo kidogo chenye vifaa vya uokozi (hakipo pichan)  katika Bandari ya Nyamisati.

*Mkurugenzi Mkuu TASAC asema zaidi ya Bilioni Mbili kununua boti za Uokozi

Na Chalila Kibuda ,Kibiti
BODI ya Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) imesema maagizo walioyatoa kwa Mamlaka ya Bandari (TPA)katika Bandari ya Nyamisati yametekelezwa kwa asilimia 95.

Akizungumza na Waandishi wa Habari baada ya ziara ya Bodi hiyo katika Bandari ya Nyamisati iliyopo wilayani Kibiti mkoani Pwani Mwenyekiti wa Bodi Nah.Mussa Mandia amesema kuwa TPA wametekeleza kwa asilimia 95 huku wakibakiza baadhi ya maeneo machache.

Mandia amesema kuwa katika ziara walioifanya katika Bandari ya Nyamisati 2022 ilikuwa ni kutaka maboresho ya Bandari ili iweze kujiendesha kibiashara kama moja ya Bandari ya mkakati.

"Tumeridhishwa na utekelezaji wa TPA kutekeleza na kuona Bandari ya Nyamisati inafanya kazi kutokana na kuwa wateja wa mizigo na abiria"amesema Nahodha Mandia.

Mandia amesema kuwa katika mahitaji ya Bandari hiyo inahudumia visiwa zaid ya 16 ambapo idadi abiria kati ya 120 hadi 300 kwa siku huku mizigo ikiwa mingi.

Mkurugenzi Mkuu wa TASAC Mohamed Salum amesema katika mkakati wa mwaka huu ni ununuzi wa boti za Uokoaji Sita zenye thamani ya zaidi ya Bilioni Mbili ambazo zitasambazwa katika vituo vya mikoa yenye bahari ya Hindi na maziwa makuu.

Amesema Vyombo vilivyopo katika Bandari ya Nyamisati vimesajiliwa na vinaa vifaa vya uokozi hivyo, mikakati iliyopo itafanya kuwa bora katika utoaji wa huduma.

Amesema mahitaji ya msingi ni mashine ya kupakia na kunyanyua mizigo 'Forklift' na miundombinu ya eneo la Bandari kusakafiwa Kitaalam kwa eneo la.kuhudumia mizigo.

Meneja wa Bandari ya Nyamisati Issa Unemba amesema kuwa Bandari ya Nyamisati itakwenda kuipita Bandari ya Bagamoyo kutokana na wahitaji wa mizigo kwenda katika nchi za Comoro na Madagascar.

Amesema kuwa utekelezaji kwa mizigo ya nje ya nchi kunatakiwa kuwepo kwa Afisa forodha kwani sehemu za maghala zipo za kutosha kwa vyakula na bidhaa zisizo za Chakula.

Mwenyekiti wa Bodi ya TASAC Nahodha Mussa Mandia akizungumza na Waandishi wa Habari wakati Bodi hiyo ilipofanya ziara katika Bandari ya Nyamisati wilayani Kibiti Mkoani Pwani kuangalia uendelezaji wa Bandari hiyo.

Mkurugenzi Mkuu wa TASAC Mohamed Salum akieleza kuhusiana na mipango ya mkakati katika Bandari ya Nyamisati katika kutoa huduma za Usafiri kwa Vyombo Vidogo vya Majini, amesema wataanzisha ofisi ya TASAC viwani Mafia.

Meneja wa Bandari ya Nyamisati Issa Unemba akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusiana na utendaji wa Bandari hiyo pamoja na maboresho yaliyofanyika wakati Bodi ya TASAC ilipotembelea Bandari ya Nyamisati wilayani Kibiti mkoani Pwani.

Mkurugenzi Mkuu wa TASAC Mohamed Salum akiangalia chombo kidogo chenye vifaa vya uokozi (hakipo pichani) katika Bandari ya Nyamisati.

Mwenyekiti wa Bodi ya TASAC Nahodha Mussa Mandia akizungumza katika Bandari ya Nyamisati wakati Bodi hiyo ilipofanya ziara Bandari hapo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad