JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


ALAF Yazindua Maonyesho ya Kazi

Share This

Mkurugenzi wa Taaluma wa Taasisi ya Teknorojia Dar es Salaam (DIT) Dk.
Kilaza Mwaikono akizingumza katika mkutano na wanafunzi wa Taasisi ya
Teknorojia Dar es Salaam (DIT) wakati wa maonyesho ya kazi
yajulikanayo Afaf (Career Fair), yaliofanyika katika ofisi za taasisi

hiyo jijini Dar es Salaam jana. 

Wanafuni wa Taasisi ya Teknorojia Dar es Salaam (DIT) wakiwa katika
mkutano wakati wa maonyesho ya kazi zinazozalishwa na kiwanda cha
mabati cha Alaf yajulikanayo Afaf (Career Fair), yaliofanyika katika
ofisi za taasisi hiyo jijini Dar es Salaam jana.











Mhandisi wa Kitengo cha mabati ya rangi wa kiwanda cha Alaf, Tumani
Minja, akizingumza katika mkutano na wanafunzi wa Taasisi ya
Teknorojia Dar es Salaam (DIT) wakati wa maonyesho ya kazi
yajulikanayo Afaf (Career Fair), yaliofanyika katika ofisi za taasisi
hiyo jijini Dar es Salaam jana.
Meneja rasilimali watu wa kiwanda cha mabati cha Alaf, Onjero Jumbe,
akizingumza katika mkutano na wanafunzi wa Taasisi ya Teknorojia Dar
es Salaam (DIT) wakati wa maonyesho ya kazi yajulikanayo Afaf (Career
Fair), yaliofanyika katika ofisi za taasisi hiyo jijini Dar es Salaam
jana.


ALAF Limited yazindua maonyesho ya kazi DIT
ALAF Limited, kampuni inayoongoza na inayoaminiwa kwa kuzalisha vifaa vya ujenzi Tanzania, Jumamosi ilizindua Maonyesho ya kazi kwenye Taasisi ya Teknolojia ya Dar es Salaam (DTI).

Meneja wa Rasilimali watu wa ALAF Bw. Jumbe Onjero alisema uzinduzi huo wenye dhamira ya ‘Kujenga Madaraja’ ulilenga kukuza vipaji vya vijana ili kupata mafanikio katika maisha yao.

Bw Onjero alisema: "Dhamira ya ‘Kujenga Madaraja’ inaonyesha moyo wetu wa dhati wa kuanzisha mahusiano imara na ya kudumu na wanafunzi wetu, wanaojiandaa kwa kazi na kwa mahitaji ya tasnia,” alisema.

Kulingana na Bw. Onjero alisema maonyesho ya taaluma ni fursa nzuri kwa watu binafsi kusikia masimulizi ya mafanikio ya ukuaji wa kazi, kuwa na mtandao wa mawasiliano na wanataaluma hao, na kujifunza zaidi kuhusu ujuzi unaohitajika ili watu waweze kufikia malengo ya kazi zao.

Alisema baada ya DIT, ALAF inaarajia kwenda katika taasisi mbalimbali za elimu ya juu, kama vile vyuo vikuu na vyuo vingine na shule za sekondari nchi nzima.
“Tukio la Jumamosi lilikuwa na hotuba kutoka nyanja mbalimbali, warsha shirikishi, na mijadala ya paneli, kipindi cha ‘maswali na majibu’ kilichoratibiwa vyema, kikiruhusu kushirikishana uzoefu binafsi wa washiriki.”

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Kaimu Mkurugenzi wa Taaluma wa DIT aliipongeza ALAF Limited kwa kuanzisha maonyesho ya taaluma, akisema ni njia nzuri ya kurudisha kwa jamii ukarimu.

"Hii itahakikisha wanafunzi wetu wanajiandaa vizuri kukabiliana na soko la ajira na wanajua matarajio ya jamii kwao watakaofika huko kwenye soko," alisema.

Alitoa wito kwa wanafunzi kutumia fursa ya maonyesho kwa sababu matukio kama haya ni ya nadra sana kwani pia inawapa wanafunzi fursa ya kifahamu ukweli kuhusu Soko la ajira.

Alisema kitendo cha kuwaleta wanafunzi waliopita DIT na sasa wameajiriwa na ALAF kimewatia moyo wanafunzi wanaotarajia kumaliza masomo Yao.

Mmoja wa wanafunzi hao wa zamani, Injinia Tumaini Minja, alisema Programu hii ya ALAF ilimfungulia fursa kwani aliajiriwa mwaka mmoja baada ya kufanya kama majaribio na baada ya miaka Saba sasa anasimamia kitengo cha mabati ya rangi.

"ALAF imeona umuhimu wa kuajiri vijana wa kitanzania Kwa maana hiyo wameweka nguvu kubwa katika career fair ili wapate watu sahihi," alisema.

Waziri wa Miundombinu na Teknolojia wa DIT, Kelvin Wilson ambaye ni mwanafunzi wa mwaka wa nne anayesomea uhandisi wa umeme, alisema zoezi hili ni la kuigwa kwani litahakikisha ALAF inapata mainjinia wa uhakika.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad