Na Jane Edward, Arusha
Vilio,
nyuso za Huzuni, Majonzi na sura zilizokufa Matumaini ni mambo
yaliyotawala kwenye Nyuso za mamia ya Wakazi wa Mkoa wa Arusha
waliojitokeza kwa wingi kwenye Kliniki Maalum ya Mkuu wa Mkoa Mhe. Paul
Christian Makonda ya kusikiliza na kutatua changamoto mbalimbali za
Wananchi.
Mhe. Mkuu wa Mkoa amekuwa hapa kwenye viwanja vya Ofisi
yake Mkoani Arusha kuhakikisha kuwa Mawakili, watumishi wa idara
mbalimbali na taasisi zinazotoa misaada ya kisheria zinawajibika
kikamilifu kuwasikiliza na kutatua changamoto zote za Wananchi
waliojitokeza hapa.
Makonda ameahidi kusimamia kuhakikisha kila
mmoja anaridhika na maamuzi yatakayotolewa leo akiahidi pia kutoa msaada
wa mawakili kwa kesi zitakazokuwa na uhitaji wa kupelekwa mahakamani.
"Leo nataka niwaambie wananchi wa Arusha hizi siku tatu ni za kwao na
ninataka kila mwenye kero aje hapa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wasikilizwe na
wataalamu wangu hapa kwaajili ya utatuzi"Alisema
Haya hivyo zoezi hilo limeanza leo Mei 08,2024 na likitarajiwa kukamilika Mei 10, 2024.
Kliniki ya kusikiliza Wananchi yaanza Rasmi Mkoani Arusha.
Share This
Tags
# HABARI
Share This
Jiachie Blog
HABARI
Labels:
HABARI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Author Details
A Tanzanian blog operating since 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.
No comments:
Post a Comment