WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika utiaji saini mikataba 20 ya ukarabati na ujenzi wa miradi ya umwagiliaji baina ya Tume ya Taifa ya Umwagiliaji chini ya Wizara ya Kilimo na Wakandarasi jijini Dodoma hapo kesho.
Mikataba hiyo ni ya ujenzi na ukarabati wa Skimu 14
pamoja na miradi sita (6) ya usanifu wa kina na upembuzi yakinifu ili
kampuni zilizoshinda zabuni ziweze kuanza zoezi la utekelezaji wa miradi
hiyo kupitia mikataba husika.
Baadhi ya miradi hiyo ni pamoja
na skimu ya Itping iliyopo wilaya ya Njombe mkoani Njombe, Skimu ya
Mahiga iliyopo wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza, Skimu ya Msange iliyopo
Wilaya ya Singida mkoani Singida, Skimu za Ndungu na Kihurio zilizopo
Wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro, ujenzi wa Bwawa na Skimu ya Luiche
katika Wilaya ya Kigoma mkoani Kigoma.
Kwa upande wa usanifu wa
kina na upembuzi yakinifu katika Bwawa la Kalupale lililoko wilaya ya
Sikonge mkoani Tabora, upembuzi yakinifu katika Skimu ya Ifakara - Idete
iliyopo Wilaya ya Kilombero mkoani Morogoro, eneo lingine ni Pamoja na
Skimu ya Butonga – Nyamazuka, Igaka – Bundala na Isole Mkoani Mwanza.
No comments:
Post a Comment