JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


VIONGOZI MASHABIKI WA TIMU ZA SIMBA NA YANGA WATOA BURUDANI ARUSHA

Share This

 


Na Eleuteri Mangi, Arusha
TIMU ya Viongozi wa vilabu vinavyoshiriki michuano ya Mei Mosi Taifa 2024 ambao ni mashabiki wa vilabu vya Simba na Yanga wametoa burudani kwa wakazi wa jiji la arusha katika mchezo wa mpira wa miguu na netiboli kuthibitisha umwamba wa vilabu vyao wanavyoshabikia hapa nchini.

Akizungumzia michezo hiyo iliyofanyika Aprili 26, 2024 katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Arusha, Katibu wa Kamati ya Michezo ya Mei Mosi Taifa Bw. Alex Temba amesema kuwa wanamichezo hao ambao ni viongozi mashabiki wa timu ya Simba katika mpira wa miguu wameibuka kidedea kwa kuwafunga viongozi mashabiki wa Yanga kwa magoli 2 - 0 wakati kwa upande wa netibili viongozi wa timu ya Yanga wameibuka kidedea.

“Kwa kweli mechi ilikuwa nzuri imefurahisha, unaona mashabiki na wananchi wa jiji la Arusha walivyojitokeza kwa wingi, hizi timu zetu mbili zina mkusanyiko mkubwa sana wa watu. Tunawakaribisha wananchi wa Arusha waje kupata burudani ya michezo mbalimbali na kuwaona wanamichezo wa Rais Mama Samia wanavyojikinga na magonjwa na maradi yasiyoambukizwa kwa njia ya michezo” Bw. Temba.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa mashabiki wa Simba na Katibu wa Mawasiliano Sports Klab Bw. Aliko Mwaiteleke amesema wanaamini timu yao ya Simba bado ni imara na mengine ni ya kupita.

“Sisi tumejiandaa kama Simba, ndiyo maana unaona tumejiandaa kama Simba na tumeshinda goli 2 – 0, watu wetu bado wana moyo sana na Simba sports Klab, angalia jezi zetu, ni lazima tuoneshe thamani ya timu yetu ndiyo maana tunasema Simba Nguvu Moja” Bw. Aliko.

Naye Mratibu wa mashabiki wa Yanga na Katibu wa Timu ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Kamna Shomary amesema viongozi wameamua na kupanga siku moja ya wao kucheza bonanza ambalo wamelitumia kama njia ya kufahamiana na kuimarisha udugu.

Kwa upande wa netiboli, viongozi mashabiki wa timu ya Sim ana Yanga na wakiongozwa na Jacqueline Sikozi shabiki wa timu ya Simba na Nyabuchwenza Metusela, Mwenyekiti wa timu ya Shirika la Viwango Tanzania (TBS) wamewasisitiza wachezaji na watumishi wa umma kuendelea kufanya mazoezi kwa kuwa michezo ni furaha, tiba, udugu n ani namna ya kuimarisha afya zao ili wanaporudi kazini wakafanye kazi kwa tija zaidi

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad