Na Mwandishi Wetu
SERIKALI ya Awamu ya Sita inayoongozwa na
Rais Dk.Samia Suluhu Hassan imekabidhi dawa na vifaa tiba vyenye thamani
ya zaidi ya Sh.bilioni 1.61 katika Wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro.
Hayo
yamesemwa leo Desemba 6, 2023 na Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Judithi
Nguli wakati Bohari ya Dawa (MSD), ikikabidhi dawa na vifaa tiba vya
zaidi ya sh. bilioni 1.61 kwa vituo vya afya na hospitali za wilaya hiyo
huku akieleza hatua hiyo ya Rais Dk.Samia kwa Mvomero ni funga kazi
kwani haijawahi kutokea.
Amesema Rais Samia ameonyesha uzalendo
na utendaji wa vitendo katika kumaliza kero ya kukosekana kwa dawa na
vifaa tiba katika hospitali za umma na binafsi.“Tunaomba tumshukuru
mheshimiwa Rais ametushusha mzigo wa maswali wasaidizi wake.
"Tunatamani
Watanzania wajue kuwa wana Mvomero tuna furaha sana jambo hili ni kubwa
pia ameturahisishia utendaji kazi na kutujengea heshima kwa
wananchi.Wilaya hii Jiografia yake kila mmoja anaitambua kwanza ni ya
kimkakati na pia ni wilaya inayozungukwa na maeneo mengi muhimu ya
kiuchumi.
“Wingi wa wananchi wanaohitaji huduma na mahitaji ni
makubwa sana tulikuwa tunasubiri kwa hamu vifaa hivi aliwahi kusema kuwa
vilio vya dawa sasa basi ametimiza ahadi kwa kusikiliza kilio cha
wananchi na kutenda kupitia MSD,”amesema.
Amewataka watendaji wa
halmashari na hospitali kwa ujumla kuzingatia maadili ya utendaji kazi
na kutomuangusha Rais kwa kuhudumia wananchi ipasavyo.
Ametumia
nafasi hiy kuhimiza utunzaji wa vifaa tiba vilivyotolewa kwani maboresho
ya afya yanayofanyika ni muhimu kwa maendeleo ya kiuchumi.
Ameongeza
hatua ya MSD kutoa dawa na vifaa tiba hivyo kwa mkopo imeacha alama kwa
wilaya hiyo, kwani maeneo ya Mvomero ukitoka Gairo hakuna hospitali
nyingine ya wilaya.
Ameeleza kuwa maeneo ya karibu ikiwemo Dumila
na Tuliani yanategemea huduma hizo Mvomero na vipo viwanda kikiwemo
cha Mkulazi kilichopo Kilosa, Nguruira na Mtibwa ambapo watumishi wake
inapotokea changamoto wanatibiwa katika hospitali hiyo.
“Mbali na
viwanda kuna magereza matatu na wananchi wengi wanaokuja kwa ajili ya
kilimo ambapo kuna mashamba makubwa ya umwagiliaji huku pia inapotokea
ajali katika barabara kubwa inayounganisha Mvomero na mikoa mingine
hakuna huduma katika chumba cha kuhifadhia maiti hivyo ujio wa majokofu
ya kuhifadhi maiti ya kisasa katika hospitali tatu za Mvomero ikiwemo ya
wilaya ni muhimu sana sana,”amesema
Kwa upande wake Mbunge wa
Mvomero Jonas Zeeland amesema wananchi wa Mvomero wana deni kubwa kwa
Rais Dk.Samia mwaka kwani ujio wa dawa na vifaa tiba hivyo vya zaidi ya
sh. bilioni 1 utasaidia kutatua changamoto za wilaya hiyo.
Amesema
kwa muda mrefu kulikuwa na majengo ya vituo vya afya vilivyojengwa na
wananchi na vile vilivyojengwa na serikali lakini hakukuwa na huduma
kutokana na kukosa vifaa tiba.
“Ujio wa vifaa hivi vitasambazwa
maeneo yote hususani ya vijijini na baada ya muda mfupi vitaanza kufanya
kazi na wananchi kupata huduma huku pia majokofu yaliyoletwa kwa ajili
ya kuhifadhia maiti ni muhimu kutokana na jiografia yetu ambapo tumekuwa
tukipokea majeruhi na vifo vingi vya ajali ambapo maiti zilikuwa
zikipelekwa mkoani,”amesema.
Zeeland amesisitiza majokofu hayo
yatatolewa katika maeneo mbalimbali na vifaa tiba vingine na dawa
zitasambazwa hadi katika vituo vya afya vipya ambavyo ujenzi wake
unaendelea kukamilika kikiwemo kituo cha Mlali, Dakawa na Mziha.
Ameongeza
mabadiliko makubwa yanayofanywa na Serikali ya Rais Dk.Samia katika
bohari ya dawa matunda yake yameanza kuonekana hivyo wanampongeza
Mkurugenzi Mkuu wa MSD Mavere Tukai kwa kukubali mabadiliko na
kuyafanyia kazi kwa maslahi ya wananchi
Wakati huo huo Meneja wa
MSD Kanda ya Dar es Salaam, Betie Kaema, amesema mbali na dawa na vifaa
tiba hivyo Mvomero na maeneo mengine watarajie mambo makubwa zaidi
kutokana na maboresho sekta ya afya yanayoendelea kufanywa na Wizara.
“Chini
ya Rais Dk.Samia tutarajie makubwa zaidi mpango mkakati uliopo ni kuona
dawa na vifaa tiba vinakuwa vya kutosha na kuwapo na akiba katika
hospitali na vituo vyetu vya kutolea huduma, kwa sasa tumeanza kuleta
vifaa vya afya mara sita kwa mwaka huku maboresho mengine
yakiendelea,”amesema
Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Wilaya hiyo
Dk.Philipina Philipo aliahidi kwenda kusimamia watoa huduma ipasavyo
hususani kwa huduma ambazo zilikuwa hazijawahi kutolewa tangu Uhuru
ikiwemo za chumba cha kuhifadhia maiti, oparesheni kwa baadhi ya maeneo
na huduma za kibingwa katika afya ya uzazi kwa mama na mtoto.
Tags
# HABARI
Share This
Jiachie Blog
HABARI
Labels:
HABARI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Author Details
A Tanzanian blog operating since 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.
No comments:
Post a Comment